聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

12

1马利亚用香膏膏主(太26:6-13;可14:3-9;路7:37-39)
1Siku sita kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu alifika Bethania alikoishi Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka wafu.
2有人在那里为耶稣预备了筵席。马大在那里侍候,拉撒路也和一些人与耶稣一同吃饭。
2Huko walimwandalia chakula cha jioni, naye Martha akawa anawatumikia. Lazaro alikuwa mmoja wa wale waliokuwa mezani pamoja na Yesu.
3马利亚拿了半公斤珍贵纯正的哪哒香膏,抹耶稣的脚,又用自己的头发去擦;屋里就满了香膏的香气。
3Basi, Maria alichukua chupa ya marashi ya nardo safi ya thamani kubwa, akampaka Yesu miguu na kuipangusa kwa nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marashi.
4耶稣的一个门徒,就是那要出卖他的加略人犹大,说:
4Basi, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
5“为什么不把这香膏卖三百银币,赒济穷人呢?”
5"Kwa nini marashi hayo hayakuuzwa kwa fedha dinari mia tatu, wakapewa maskini?"
6他说这话,并不是因为他关怀穷人,而是因为他是个贼,又带着钱囊,常取其中所存的。
6Alisema hivyo, si kwa kuwa alijali chochote juu ya maskini, bali kwa sababu alikuwa mweka hazina, na kwa kuwa alikuwa mwizi, mara kwa mara aliiba kutoka katika hiyo hazina.
7耶稣就说:“由她吧,这香膏是她留下来为我安葬的日子用的。
7Lakini Yesu akasema, "Msimsumbue huyu mama! Mwacheni ayaweke kwa ajili ya siku ya mazishi yangu.
8你们常常有穷人跟你们在一起,却不常有我。”
8Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini hamtakuwa nami siku zote."
9有一大群犹太人知道耶稣在那里,就都来了,然而他们不单是为了耶稣的缘故,也是要看看耶稣使他从死人中复活的拉撒路。
9Wayahudi wengi walisikia kwamba Yesu alikuwa Bethania. Basi, wakafika huko si tu kwa ajili ya kumwona Yesu, ila pia wapate kumwona Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka wafu.
10于是祭司长想把拉撒路也杀掉,
10Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,
11因为有许多犹太人为了拉撒路的缘故,离开他们,信了耶稣。
11Maana kwa sababu ya Lazaro Wayahudi wengi waliwaasi viongozi wao, wakamwamini Yesu.
12骑驴进耶路撒冷(太21:4-9;可11:7-10;路19:35-38)第二天,有一大群上来过节的人,听见耶稣要来耶路撒冷,
12Kesho yake, kundi kubwa la watu waliokuja kwenye sikukuu walisikia kuwa Yesu alikuwa njiani kuja Yerusalemu.
13就拿着棕树枝出去迎接他,欢呼说:“和散那,奉主名来的以色列王,是应当称颂的!”
13Basi, wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki; wakapaaza sauti wakisema: "Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana. Abarikiwe mfalme wa Israeli."
14耶稣找到一头小驴,就骑在上面,正如经上所记的:
14Yesu akampata mwana punda mmoja akapanda juu yake kama yasemavyo Maandiko:
15“锡安的居民哪,不要惧怕;看哪,你的王来了,他骑着小驴来了。”
15"Usiogope mji wa Sioni! Tazama, Mfalme wako anakuja, Amepanda mwana punda."
16门徒起初不明白这些事,可是到耶稣得了荣耀以后,他们才想起这些话是指着他说的,并且人们果然向他这样行了。
16Wakati huo wanafunzi wake hawakuelewa mambo hayo, lakini Yesu alipokwisha tukuzwa, ndipo walipokumbuka kwamba hayo yalikuwa yameandikwa juu yake, na kwamba watu walikuwa wamemtendea hivyo.
17那些和耶稣在一起,看见他叫拉撒路从坟墓出来,又使他从死人中复活的群众,都为这事作见证。
17Kundi la watu wale waliokuwa pamoja naye wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, akamfufua kutoka wafu, walisema yaliyotukia.
18群众因为听见他行了这神迹,就去迎接他。
18Kwa hiyo umati huo wa watu ulimlaki, maana wote walisikia kwamba Yesu alikuwa amefanya ishara hiyo.
19于是法利赛人彼此说:“你们看,你们都是徒劳无功,世人都去跟随他了!”
19Basi, Mafarisayo wakaambiana, "Mnaona? Hatuwezi kufanya chochote! Tazameni, ulimwengu wote unamfuata."
20主被举起来就吸引万人上去过节作礼拜的人中,有些是希腊人。
20Kulikuwa na Wagiriki kadhaa miongoni mwa watu waliokuwa wamefika Yerusalemu kuabudu wakati wa sikukuu hiyo.
21他们来到加利利的伯赛大人腓力那里,请求他,说:“先生,我们想见耶稣。”
21Hao walimwendea Filipo, mwenyeji wa Bethsaida katika Galilaya, wakasema, "Mheshimiwa, tunataka kumwona Yesu."
22腓力去告诉安得烈,安得烈就和腓力去告诉耶稣。
22Filipo akaenda akamwambia Andrea, nao wawili wakaenda kumwambia Yesu.
23耶稣对他们说:“人子得荣耀的时候到了!
23Yesu akawaambia, "Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mtu imefika!
24我实实在在告诉你们,一粒麦子若不落在地里死了,仍旧是一粒;如果死了,就结出许多果实来。
24Kweli nawaambieni, punje ya ngano hubaki punje tu isipokuwa ikianguka katika udongo na kufa. Kama ikifa, basi huzaa matunda mengi.
25爱惜自己生命的,就丧掉生命;在这世上恨恶自己生命的,必会保全生命到永远。
25Anayependa maisha yake, atayapoteza; anayeyachukia maisha yake katika ulimwengu huu, atayaweka kwa ajili ya uzima wa milele.
26如果有人服事我,就应当跟从我;我在哪里,服事我的人也会在哪里;如果有人服事我,我父必尊重他。
26Anayetaka kunitumikia ni lazima anifuate, hivyo kwamba popote pale nilipo mimi ndipo na mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu yeyote anayenitumikia Baba yangu atampa heshima.
27“我现在心里烦乱,我应该说什么呢?说‘父啊,救我脱离这时刻’吗?然而我正是为了这个缘故来的,要面对这时刻。
27"Sasa roho yangu imefadhaika, na niseme nini? Je, niseme: Baba, usiruhusu saa hii inifikie? Lakini ndiyo maana nimekuja--ili nipite katika saa hii.
28父啊,愿你荣耀你的名!”当时有声音从天上来,说:“我已经荣耀了我的名,还要再荣耀。”
28Baba, ulitukuze jina lako." Hapo sauti ikasema kutoka mbinguni, "Nimelitukuza, na nitalitukuza tena."
29站在旁边的群众听见了,就说:“打雷了。”另外有人说:“有天使对他说话。”
29Umati wa watu waliokuwa wamesimama hapo walisikia sauti hiyo, na baadhi yao walisema, "Malaika ameongea naye!"
30耶稣说:“这声音不是为了我,而是为了你们发出的。
30Lakini Yesu akawaambia, "Sauti hiyo haikutokea kwa ajili yangu mimi, ila kwa ajili yenu.
31现在是这世界受审判的时候了,现在这世界的王要被赶出去。
31Sasa ndio wakati wa ulimwengu huu kuhukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu huu atapinduliwa.
32我若从地上被举起来,就要吸引万人归向我。”
32Nami nitakapoinuliwa juu ya nchi nitamvuta kila mmoja kwangu."
33他说这话,是指着自己将要怎样死说的。
33(Kwa kusema hivyo alionyesha atakufa kifo gani).
34于是群众对他说:“我们从律法上知道基督是永远常存的,你怎么说‘人子必须被举起来’呢?这人子是谁呢?”
34Basi, umati huo ukamjibu, "Sisi tunaambiwa na Sheria yetu kwamba Kristo atadumu milele. Wawezaje basi, kusema ati Mwana wa Mtu anapaswa kuinuliwa? Huyo Mwana wa Mtu ni nani?"
35耶稣说:“光在你们中间的时间不多了。你们应当趁着有光的时候行走,免得黑暗追上你们。在黑暗中行走的人,不知道往哪里去。
35Yesu akawaambia, "Mwanga bado uko nanyi kwa muda mfupi. Tembeeni mngali mnao huo mwanga ili giza lisiwapate; maana atembeaye gizani hajui aendako.
36你们应当趁着有光的时候信从这光,使你们成为光明的儿女。”耶稣说完了这些话,就离开他们隐藏起来。
36Basi, wakati mnao huo mwanga uaminini ili mpate kuwa watu wa mwanga." Baada ya kusema maneno hayo, Yesu alikwenda zake na kujificha mbali nao.
37主的道要审判不信的人耶稣在他们面前行了许多神迹,但是他们仍然不信他。
37Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini.
38这是要应验以赛亚先知所说的话:“主啊,我们所传的,有谁信呢?主的膀臂向谁显露呢?”
38Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia: "Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu? Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?"
39他们不能相信,因为以赛亚又说:
39Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya tena alisema:
40“ 神使他们瞎了眼,硬了心,免得他们眼睛看见,心里明白而回转过来;我就医好他们。”
40"Mungu ameyapofusha macho yao, amezipumbaza akili zao; wasione kwa macho yao, wasielewe kwa akili zao; wala wasinigeukie, asema Bwana, ili nipate kuwaponya."
41以赛亚说这些话,是因为看见了他的荣耀,就指着他说的。
41Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliuona utukufu wa Yesu, akasema habari zake.
42虽然这样,官长当中也有许多人信了耶稣。但是因为法利赛人的缘故,他们不敢公开承认,免得被赶出会堂;
42Hata hivyo, wengi wa viongozi wa Wayahudi walimwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakumkiri hadharani kwa kuogopa kwamba watatengwa na sunagogi.
43因为他们爱人的荣耀,过于爱 神的荣耀。
43Walipendelea kusifiwa na watu kuliko kusifiwa na Mungu
44耶稣大声说:“信我的,不单是信我,也是信那差我来的。
44Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, "Mtu aliyeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma.
45看见我的,就是看见那差我来的。
45Anayeniona mimi anamwona pia yule aliyenituma.
46我是光,我到世上来,叫所有信我的不住在黑暗里。
46Mimi ni mwanga, nami nimekuja ulimwenguni ili wote wanaoniamini wasibaki gizani.
47人若听见我的话却不遵守的,我不审判他,因为我来不是要审判世人,而是要拯救世人。
47Anayeyasikia maneno yangu lakini hayashiki mimi sitamhukumu; maana sikuja kuhukumu ulimwengu bali kuuokoa.
48弃绝我又不接受我的话的人,自有审判他的。我所讲的道在末日要定他的罪;
48Asiyeyashika maneno yangu anaye wa kumhukumu: neno lile nililosema ni hakimu wake siku ya mwisho.
49因为我没有凭着自己说话,而是差我来的父给了我命令,要我说什么,讲什么。
49Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini.
50我知道他的命令就是永生。所以,我所讲的,正是父吩咐我要我讲的。”
50Nami najua kuwa amri yake huleta uzima wa milele. Basi, mimi nasema tu yale Baba aliyoniagiza niyaseme."