1拉撒路死了
1Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
2这马利亚就是后来用香膏抹主,并且用头发把主的脚擦干的那人;患病的拉撒路是她的兄弟。
2Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
3姊妹二人派人到耶稣那里去,说:“主啊,你所爱的人病了。”
3Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: "Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!"
4耶稣听见,就说:“这病不至于死,而是为了 神的荣耀,使 神的儿子因此得到荣耀。”
4Yesu aliposikia hivyo akasema, "Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe."
5耶稣向来爱马大和她的妹妹马利亚,以及拉撒路。
5Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
6他听说拉撒路病了,仍然在原来的地方住了两天,
6Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
7然后对门徒说:“我们再到犹太去吧。”
7Kisha akawaambia wanafunzi wake, "Twendeni tena Yudea!"
8门徒对他说:“拉比,近来犹太人要拿石头打你,你还到那里去吗?”
8Wanafunzi wakamwambia, "Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?"
9耶稣说:“白昼不是有十二小时吗?人若在白昼行走,就不会跌倒,因为他看见这世上的光;
9Yesu akajibu, "Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
10人若在夜间行走,就会跌倒,因为他没有光。”
10Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake."
11耶稣说完了这些话,跟着又对他们说:“我们的朋友拉撒路睡了,我要去唤醒他。”
11Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, "Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha."
12门徒说:“主啊,如果他睡了,就会好过来的。”
12Wanafunzi wake wakamwambia, "Bwana, ikiwa amelala, basi atapona."
13其实耶稣是指着拉撒路的死说的,门徒却以为他是指正常的睡眠说的。
13Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
14于是,耶稣公开地告诉他们:“拉撒路死了。
14Basi, Yesu akawaambia waziwazi, "Lazaro amekufa;
15我为你们欢喜,因为我不在那里,是要使你们相信。现在我们到他那里去吧。”
15Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake."
16那称为“双生子”的多马,对其他的门徒说:“我们也去跟他一同死吧!”
16Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, "Twendeni nasi tukafe pamoja naye!"
17耶稣是复活是生命耶稣到了,知道拉撒路在坟墓里已经四天了。
17Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
18伯大尼靠近耶路撒冷,相距约有三公里。
18Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
19有许多犹太人来到马大和马利亚那里,为了拉撒路的死来安慰她们。
19Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
20马大听见耶稣来了,就去迎接他,马利亚却仍然坐在家里。
20Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
21马大对耶稣说:“主啊,如果你早在这里,我的兄弟就不会死了!
21Martha akamwambia Yesu, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
22就是现在,我也知道无论你向 神求什么, 神必赐给你。”
22Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa."
23耶稣对她说:“你的兄弟必会复活。”
23Yesu akamwambia, "Kaka yako atafufuka."
24马大说:“我知道在末日复活的时候,他必会复活。”
24Martha akamjibu, "Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho."
25耶稣说:“我就是复活和生命;信我的人,虽然死了,也要活着。
25Yesu akamwambia, "Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
26所有活着又信我的人,必定永远不死,你信这话吗?”
26na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?"
27她说:“主啊,我信;我已经信了,你是基督,是 神的儿子,是那要到世上来的。”
27Martha akamwambia, "Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni."
28耶稣使拉撒路复活马大说了这些话,就回去暗暗地叫她妹妹马利亚,说:“老师来了,他叫你。”
28Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, "Mwalimu yuko hapa, anakuita."
29马利亚一听见,就急忙起来,到耶稣那里去。
29Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
30那时,耶稣还没有进入村子,仍然在马大迎接他的地方。
30Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
31那些在房子和马利亚在一起安慰她的犹太人,见她匆忙地起来出去,就跟着她,以为她要到坟墓那里去哭。
31Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
32马利亚来到耶稣那里,一看见他,就俯伏在他脚前,说:“主啊,如果你早在这里,我的兄弟就不会死了!”
32Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!"
33耶稣看见她在哭,和她一同来的犹太人也在哭,就心里激动,难过起来,
33Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
34说:“你们把他安放在哪里?”他们说:“主啊,请来看。”
34Kisha akawauliza, "Mlimweka wapi?" Wakamwambia, "Bwana, njoo uone."
35耶稣哭了。
35Yesu akalia machozi.
36于是犹太人说:“你看,他多么爱这个人!”
36Basi, Wayahudi wakasema, "Tazameni jinsi alivyompenda!"
37他们中间有人说:“他既然开了瞎子的眼睛,难道不能使这个人不死吗?”
37Lakini baadhi yao wakasema, "Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?"
38耶稣又再心里激动,来到坟墓前面。那坟墓是一个洞穴,洞口有块石头堵住。
38Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
39耶稣说:“把这块石头挪开!”死者的姊姊马大对他说:“主啊,已经四天了,他必定臭了。”
39Yesu akasema, "Ondoeni hilo jiwe!" Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, "Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!"
40耶稣说:“我不是对你说过‘如果你信,就必定看见 神的荣耀’吗?”
40Yesu akamwambia, "Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?"
41于是他们把石头挪开。耶稣举目向天,说:“父啊,我感谢你,因为你垂听了我,
41Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, "Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
42我知道你常常听我,但我说这话,是为了周围站着的群众,叫他们信是你差了我来。”
42Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma."
43说了这话,就大声呼喊:“拉撒路,出来!”
43Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: "Lazaro! Toka nje!"
44那死了的人就出来,他的手脚都缠着布,脸上裹着巾。耶稣说:“解开他,让他走!”
44Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, "Mfungueni, mkamwache aende zake."
45祭司长等想杀害耶稣有许多到马利亚那里去的犹太人,看见了耶稣所作的事,就信了他。
45Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
46但他们中间有些人到法利赛人那里去,把耶稣所作的事都告诉他们。
46Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
47于是祭司长和法利赛人召开公议会,说:“这个人行了许多神迹,我们怎么办呢?
47kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, "Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
48我们若让他这样,所有的人都会信他,罗马人就会来,夺取我们的圣地,除灭我们的民族。”
48Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!"
49他们当中有一位该亚法,是那年作大祭司的,对他们说:“你们什么都不知道,
49Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, "Ninyi hamjui kitu!
50也不去想想,一个人代替人民死,免得整个民族灭亡,这对你们是有益的。”
50Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?"
51他说这话不是由于自己,而是因为他是那年的大祭司,所以预言耶稣要替犹太民族死;
51Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
52不但替犹太民族死,也要把散居各地的 神的儿女招聚成为一体。
52na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
53从那天起,他们就想杀害耶稣。
53Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
54因此,耶稣不再在犹太人中间公开活动,却离开那里,到旷野附近的地方去;到了一座名叫以法莲的城,就和门徒住在那里。
54Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
55犹太人的逾越节快到了,有许多人在过节前从各乡上耶路撒冷去,要在那里洁净自己。
55Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
56他们到处找寻耶稣,站在圣殿里的时候,彼此说:“你们认为怎样?他不会来过节吧?”
56Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, "Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?"
57祭司长和法利赛人早已下了命令:如果有人知道耶稣在哪里,就要前来报告,好去逮捕他。
57Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.