聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

10

1耶稣是好牧人
1Yesu alisema "Kweli nawaambieni, yeyote yule asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia mlangoni, bali hupenya na kuingia kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyang'anyi.
2那从门进去的,才是羊的牧人。
2Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo.
3看门的给他开门,羊也听他的声音;他按着名字呼叫自己的羊,领它们出来。
3Mngoja mlango wa zizi humfungulia, na kondoo husikia sauti yake, naye huwaita kondoo wake kila mmoja kwa jina lake na kuwaongoza nje.
4他把自己的羊领出来以后,就走在前头,羊也跟随他,因为认得他的声音。
4Akisha watoa nje huwatangulia mbele nao kondoo humfuata, kwani wanaijua sauti yake.
5它们决不会跟随陌生人,反而逃避他,因为不认得陌生人的声音。”
5Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake."
6耶稣对他们说了这个譬喻,他们却不明白他所说的是什么。
6Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.
7于是耶稣又说:“我实实在在告诉你们,我就是羊的门。
7Basi, akasema tena, "Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo.
8所有在我以先来的,都是贼和强盗;羊却不听从他们。
8Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyang'anyi, nao kondoo hawakuwasikiliza.
9我就是门,如果有人借着我进来,就必定得救,并且可以出、可以入,也可以找到草场。
9Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho.
10贼来了,不过是要偷窃、杀害、毁坏;我来了,是要使羊得生命,并且得的更丰盛。
10Mwizi huja kwa shabaha ya kuiba, kuua na kuharibu. Mimi nimekuja mpate kuwa na uzima--uzima kamili.
11我是好牧人,好牧人为羊舍命。
11"Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake.
12那作雇工不是牧人的,羊也不是自己的,他一见狼来,就把羊撇下逃跑,狼就抓住羊群,把他们驱散了;
12Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwa mwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia. Kisha mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya.
13因为他是个雇工,对羊群漠不关心。
13Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu.
14我是好牧人,我认识我的羊,我的羊也认识我,
14Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi,
15好像父认识我,我也认识父一样;并且我为羊舍命。
15kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Mimi nayatoa maisha yangu kwa ajili yao.
16我还有别的羊,不在这羊圈里;我必须把它们领来,它们也要听我的声音,并且要合成一群,归于一个牧人。
16Tena ninao kondoo wengine ambao hawamo zizini humu. Inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu, na kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.
17父爱我,因为我把生命舍去,好再把它取回来。
17"Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena.
18没有人能夺去我的生命,是我自己舍去的。我有权把生命舍去,也有权把它取回来;这是我从我的父所领受的命令。”
18Hakuna mtu anayeninyang'anya uhai wangu; mimi na nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye."
19犹太人因着这些话又起了纷争。
19Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
20他们当中有许多人说:“他是鬼附的,他发疯了;为什么要听他呢?”
20Wengi wao wakasema, "Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?"
21另外有人说:“这话不是鬼附的人所说的。鬼怎能使瞎子的眼睛开了呢?”
21Wengine wakasema, "Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?"
22犹太人弃绝耶稣在耶路撒冷,献殿节到了,那时是冬天。
22Huko Yerusalemu kulikuwa na sikukuu ya Kutabaruku. Wakati huo ulikuwa wa baridi.
23耶稣在殿的所罗门廊上走过,
23Naye Yesu akawa anatembea Hekaluni katika ukumbi wa Solomoni.
24犹太人围着他,对他说:“你使我们心里悬疑不定,要到几时呢?如果你是基督,就公开地告诉我们吧!”
24Basi, Wayahudi wakamzunguka, wakamwuliza, "Utatuacha katika mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo, basi, tuambie wazi."
25耶稣对他们说:“我已经告诉你们,你们却不相信;我奉我父的名所作的事,可以为我作证。
25Yesu akawajibu, "Nimewaambieni, lakini hamsadiki. Kazi ninazozifanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia.
26只是你们不信,因为你们不是我的羊。
26Lakini ninyi hamsadiki kwa sababu ninyi si kondoo wangu.
27我的羊听我的声音,我也认识他们,他们也跟随我。
27Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.
28我赐给他们永生,他们永不灭亡,谁也不能把他们从我手里夺去。
28Mimi nawapa uzima wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu.
29那位把羊群赐给我的父比一切都大,也没有人能把他们从我父的手里夺去。
29Baba yangu ambaye ndiye aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote, wale hakuna awezaye kuwatoa mikononi mwake Baba.
30我与父原为一。”
30Mimi na Baba, tu mmoja."
31犹太人又拿起石头要打他。
31Basi, Wayahudi wakachukua mawe ili wamtupie.
32耶稣对他们说:“我把许多从父那里来的善事显给你们看,你们因哪一件要用石头打我呢?”
32Yesu akawaambia, "Nimewaonyesheni kazi nyingi kutoka kwa Baba. Ni ipi kati ya hizo inayowafanya mnipige mawe?"
33犹太人对他说:“我们不是因为善事用石头打你,而是因为你说了僭妄的话;又因为你是个人,竟然把自己当作 神。”
33Wayahudi wakamjibu, "Hatukupigi mawe kwa ajili ya tendo jema, ila kwa sababu ya kukufuru! Maana wajifanya kuwa Mungu hali wewe ni binadamu tu."
34耶稣说:“你们的律法上不是写着‘我说你们是神’吗?
34Yesu akawajibu, "Je, haikuandikwa katika Sheria yenu: Mimi nimesema, ninyi ni miungu?
35圣经是不能废除的,如果那些承受 神的道的人, 神尚且称他们是神,
35Mungu aliwaita miungu wale waliopewa neno lake; nasi twajua kwamba Maandiko Matakatifu yasema ukweli daima.
36那么父所分别为圣又差到世上来的,他自称是 神的儿子,你们就说他说了僭妄 神的话吗?
36Je, yeye ambaye Baba alimweka wakfu na kumtuma ulimwenguni, mnamwambia: Unakufuru, eti kwa sababu nilisema: Mimi ni Mwana wa Mungu?
37我若不作我父的事,你们就不必信我;
37Kama sifanyi kazi za Baba yangu msiniamini.
38我若作了,你们纵然不信我,也应当信这些事,好使你们确实知道,我父是在我里面,我也在父里面。”
38Lakini ikiwa ninazifanya, hata kama hamniamini, walau ziaminini hizo kazi mpate kujua na kutambua kwamba Baba yuko ndani yangu, nami niko ndani yake."
39他们又要逮捕耶稣,他却从他们的手中逃脱了。
39Wakajaribu tena kumkamata lakini akachopoka mikononi mwao.
40耶稣又往约旦河东去,到约翰从前施洗的地方,住在那里。
40Yesu akaenda tena ng'ambo ya mto Yordani, mahali Yohane alipokuwa akibatiza, akakaa huko.
41许多人到他那里去,说:“约翰没有行过一件神迹,但约翰指着这人所说的一切话,都是真实的。”
41Watu wengi walimwendea wakasema, "Yohane hakufanya ishara yoyote. Lakini yale yote Yohane aliyosema juu ya mtu huyu ni kweli kabisa."
42在那里就有许多人信了耶稣。
42Watu wengi mahali hapo wakamwamini.