聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

9

1治好生来瞎眼的人
1Yesu alipokuwa akipita alimwona mtu mmoja, kipofu tangu kuzaliwa.
2他的门徒问他:“拉比,这人生下来就瞎眼,是谁犯了罪?是他呢,还是他的父母呢?”
2Basi, wanafunzi wakamwuliza, "Mwalimu! Ni nani aliyetenda dhambi: mtu huyu, ama wazazi wake, hata akazaliwa kipofu?"
3耶稣回答:“不是他犯了罪,也不是他的父母犯了罪,而是要在他身上彰显 神的作为。
3Yesu akajibu, "Jambo hili halikutukia kwa sababu ya dhambi zake yeye, wala dhambi za wazazi wake; ila alizaliwa kipofu ili nguvu ya Mungu ionekane ikifanya kazi ndani yake.
4趁着白昼,我们必须作那差我来者的工;黑夜一到,就没有人能作工了。
4Kukiwa bado mchana yatupasa kuendelea kufanya kazi za yule aliyenituma; maana usiku unakuja ambapo mtu hawezi kufanya kazi.
5我在世上的时候,是世界的光。”
5Wakati ningali ulimwenguni, mimi ni mwanga wa ulimwengu."
6说了这话,就吐唾沫在地上,用唾沫和了一点泥,把泥抹在瞎子的眼睛上,
6Baada ya kusema hayo, akatema mate chini, akafanyiza tope, akampaka yule kipofu machoni,
7对他说:“你去西罗亚池洗一洗吧。”(西罗亚就是“奉差遣”的意思。)于是他就去了,洗完了,走的时候,就看见了。
7akamwambia, "Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu." (maana ya jina hili ni "aliyetumwa"). Basi, huyo kipofu akaenda, akanawa, kisha akarudi akiwa anaona.
8那时,邻居和以前常常见他讨饭的人说:“这不是那一向坐着讨饭的人吗?”
8Basi, jirani zake na wale waliokuwa wanajua kwamba hapo awali alikuwa maskini mwombaji, wakasema, "Je, huyu siye yule maskini aliyekuwa akiketi na kuomba?"
9有的说:“是他。”有的说:“不是他,只是像他。”他自己说:“是我。”
9Baadhi yao wakasema, "Ndiye." Wengine wakasema, "La! Ila anafanana naye." Lakini huyo aliyekuwa kipofu akasema, "Ni mimi!"
10他们就问他:“你的眼睛是怎样开的呢?”
10Basi, wakamwuliza, "Sasa, macho yako yalipataje kufumbuliwa?"
11他回答:“那名叫耶稣的人和了一点泥,抹在我的眼上,对我说:‘你去西罗亚池洗一洗吧。’我去一洗,就看见了。”
11Naye akawajibu, "Yule mtu aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka machoni na kuniambia: Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu. Basi, mimi nikaenda, nikanawa, nikapata kuona."
12他们说:“那人在哪里?”他说:“我不知道。”
12Wakamwuliza, "Yeye yuko wapi?" Naye akawajibu, "Mimi sijui!"
13法利赛人查问瞎眼的人他们就把那个从前瞎眼的人带到法利赛人那里。
13Kisha wakampeleka huyo mtu aliyekuwa kipofu kwa Mafarisayo.
14耶稣和了泥开他眼睛的那一天,正是安息日。
14Siku hiyo Yesu alipofanya tope na kumfumbua macho mtu huyo, ilikuwa siku ya Sabato.
15法利赛人又问他是怎样可以看见的。他告诉他们:“耶稣把泥抹在我的眼上,我一洗就看见了。”
15Basi, Mafarisayo wakamwuliza mtu huyo, "Umepataje kuona?" Naye akawaambia, "Alinipaka tope machoni, nami nikanawa na sasa naona."
16有几个法利赛人说:“那个人不是从 神那里来的,因为他不守安息日。”另外有些人说:“一个罪人怎能行这样的神迹呢?”他们就起了纷争。
16Baadhi ya Mafarisayo wakasema, "Mtu huyu hakutoka kwa Mungu, maana hashiki sheria ya Sabato." Lakini wengine wakasema, "Mtu mwenye dhambi awezaje kufanya ishara za namna hii?" Kukawa na mafarakano kati yao.
17他们再对瞎子说:“他既然开了你的眼睛,你说他是什么人?”他说:“他是个先知。”
17Wakamwuliza tena huyo mtu aliyekuwa kipofu, "Maadam yeye amekufungua macho, wasemaje juu yake?" Naye akawaambia, "Yeye ni nabii!"
18犹太人不信他从前是瞎眼,现在才能看见的,于是把他的父母叫来,
18Viongozi wa Wayahudi hawakusadiki kwamba mtu huyo alikuwa kipofu hapo awali na sasa anaona mpaka walipowaita wazazi wake.
19问他们:“这是你们所说那生下来就瞎眼的儿子吗?现在他怎么又能看见呢?”
19Basi, wakawauliza hao wazazi, "Je, huyu ndiye mtoto wenu ambaye ninyi mwasema alizaliwa kipofu? Sasa amepataje kuona?"
20他的父母回答:“我们知道他是我们的儿子,生下来就瞎眼;
20Wazazi wake wakajibu, "Tunajua kwamba huyu ni mtoto wetu, na kwamba alizaliwa kipofu.
21现在他是怎样可以看见的,我们不知道;谁开了他的眼睛,我们也不知道。你们问他吧;他已经长大成人,可以替自己讲话了。”
21Lakini amepataje kuona, hatujui; na wala hatumjui yule aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima, anaweza kujitetea mwenyewe."
22他的父母这样说,是因为怕犹太人,原来犹太人已经定好了,不论谁承认耶稣是基督,就要把那人赶出会堂。
22Wazazi wake walisema hivyo kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi kwani viongozi hao walikuwa wamepatana ya kwamba mtu yeyote atakayekiri kwamba Yesu ni Kristo atafukuzwa nje ya sunagogi.
23因此他的父母说:“他已经长大成人,你们问他吧。”
23Ndiyo maana wazazi wake walisema: "Yeye ni mtu mzima, mwulizeni."
24于是法利赛人第二次把那从前瞎眼的人叫来,对他说:“你应当归荣耀给 神,我们知道这人是个罪人。”
24Basi, wakamwita tena aliyekuwa kipofu, wakamwambia, "Sema ukweli mbele ya Mungu! Sisi tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi."
25那人回答:“他是不是个罪人,我不知道;我只知道一件事,就是我本来是瞎眼的,现在能看见了。”
25Yeye akajibu, "Kama ni mwenye dhambi mimi sijui. Lakini kitu kimoja najua: Nilikuwa kipofu, na sasa naona."
26他们就问:“他向你作了什么呢?他怎样开了你的眼睛呢?”
26Basi, wakamwuliza, "Alikufanyia nini? Alikufumbuaje macho yako?"
27他回答:“我已经告诉你们,但是你们不听;为什么现在又想听呢?你们也想成为他的门徒吗?”
27Huyo mtu akawajibu, "Nimekwisha waambieni, nanyi hamkusikiliza; kwa nini mwataka kusikia tena? Je, ninyi pia mnataka kuwa wafuasi wake?"
28他们就骂他,说:“你才是他的门徒,我们是摩西的门徒。
28Lakini wao wakamtukana wakisema, "Wewe ni mfuasi wake; sisi ni wafuasi wa Mose.
29我们知道 神曾对摩西说话;只是这个人,我们不知道他从哪里来。”
29Sisi tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini mtu huyu hatujui ametoka wapi!"
30那人对他们说:“这就奇怪了,他开了我的眼睛,你们竟然不知道他从哪里来。
30Naye akawajibu, "Hili ni jambo la kushangaza! Ninyi hamjui ametoka wapi, lakini amenifumbua macho yangu!
31我们知道 神不听罪人的祈求,只听那敬畏 神,遵行他旨意的人。
31Tunajua kwamba Mungu hawasikilizi watu wenye dhambi, ila humsikiliza yeyote mwenye kumcha na kutimiza mapenzi yake.
32自古以来,没有人听过生下来就是瞎眼的,有人可以开他们的眼睛。
32Tangu mwanzo wa ulimwengu haijasikika kwamba mtu ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu.
33这人若不是从 神那里来的,他就不能作什么。”
33Kama mtu huyu hakutoka kwa Mungu, hangeweza kufanya chochote!"
34他们说:“你的确是在罪中生的,还敢教训我们吗?”就把他赶出去。
34Wao wakamjibu, "Wewe ulizaliwa na kulelewa katika dhambi; unawezaje kutufundisha sisi?" Basi, wakamfukuzia mbali.
35耶稣听见他们把他赶出去,后来遇见他的时候,就对他说:“你信人子吗?”
35Yesu alisikia kwamba walikuwa wamemfukuzia mbali, naye alipomkuta akamwuliza, "Je, wewe unamwamini Mwana wa Mtu?"
36他说:“先生,谁是人子,好让我信他呢?”
36Huyo mtu akajibu, "Mheshimiwa, niambie yeye ni nani, ili nipate kumwamini."
37耶稣说:“你已经见过他,现在跟你说话的就是他。”
37Yesu akamwambia, "Umekwisha mwona, naye ndiye anayesema nawe sasa."
38那人说:“主啊,我信。”就向他下拜。
38Basi, huyo mtu akasema, "Ninaamini Bwana!" Akamsujudia.
39耶稣说:“我到这世上来是为了审判,使那看不见的能够看见,能看见的反而成了瞎眼的。”
39Yesu akasema, "Mimi nimekuja ulimwenguni kutoa hukumu, kusudi wasioona wapate kuona, na wale wanaoona wawe vipofu."
40有些和耶稣在一起的法利赛人听了这话,就说:“难道我们也是瞎眼的吗?”
40Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye walisikia maneno hayo, wakamwuliza, "Je, sisi pia ni vipofu?"
41耶稣对他们说:“如果你们是瞎眼的,就没有罪了;但现在你们说‘我们能看见’,所以你们还是有罪的。”
41Yesu akawajibu, "Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na hatia; lakini sasa ninyi mwasema: Sisi tunaona, na hiyo yaonyesha kwamba mna hatia bado.