1耶稣不定犯奸淫妇人的罪
1lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.
2黎明的时候,他又到圣殿去,众人都来到他那里,他就坐下教导他们。
2Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena Hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.
3经学家和法利赛人带了一个行淫时被抓到的妇人来,叫她站在中间,
3Basi, walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.
4就对耶稣说:“先生,这妇人是正在犯奸淫的时候被抓到的。
4Kisha wakamwuliza Yesu, "Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.
5摩西在律法上吩咐我们把这样的妇人用石头打死,你怎样说呢?”
5Katika Sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?"
6他们说这话是要试探耶稣,要找把柄来控告他。耶稣却弯下身,用指头在地上写字。
6Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole.
7他们不住地问耶稣,他就挺起身来,说:“你们中间谁是没有罪的,他就可以先拿起石头打她。”
7Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, "Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe."
8于是又弯下身在地上写字。
8Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini.
9他们听了这话,就从年老的开始,一个一个地都离开了,留下的只有耶稣和那个还站在那里的妇人。
9Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitanguliwa na wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale.
10耶稣挺起身来,问她:“妇人,他们在哪里?没有人定你的罪吗?”
10Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, "Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?"
11她说:“主啊!没有。”耶稣说:“我也不定你的罪。走吧,从现在起不要再犯罪了。”
11Huyo mwanamke akamjibu, "Mheshimiwa, hakuna hata mmoja!" Naye Yesu akamwambia, "Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena."
12耶稣是世界的光耶稣又对众人说:“我是世界的光,跟从我的,必定不在黑暗里走,却要得着生命的光。”
12Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, "Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu. Anayenifuata mimi hatembei kamwe gizani, bali atakuwa na mwanga wa uzima."
13法利赛人对他说:“你为自己作证,你的见证不是真实的。”
13Basi, Mafarisayo wakamwambia, "Wewe unajishuhudia mwenyewe; kwa hiyo ushahidi wako si halali."
14耶稣回答:“即使我为自己作证,我的见证还是真实的,因为我知道我从哪里来,往哪里去,但你们却不知道我从哪里来,往哪里去。
14Yesu akawajibu, "Hata kama ninajishuhudia mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli kwa sababu mimi najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15你们按着外貌判断人,我却不判断人。
15Ninyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.
16即使我判断人,我的判断也是正确的,因为我不是独自一人,而是差我来的父和我在一起。
16Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.
17你们的律法上也写着:‘两个人的见证才是真的。’
17Imeandikwa katika Sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.
18我为自己作证,差我来的父也为我作证。”
18Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia."
19他们问:“你的父在哪里?”耶稣回答:“你们不认识我,也不认识我的父;如果你们认识我,也就认识我的父了。”
19Hapo wakamwuliza, "Baba yako yuko wapi?" Yesu akawajibu "Ninyi hamnijui mimi wala hamumjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia."
20这些话是耶稣在殿里教导人的时候,在银库的院中说的。当时没有人逮捕他,因为他的时候还没有到。
20Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha Hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
21不信基督的必在罪中死亡耶稣又对他们说:“我要去了,你们要寻找我,并且要在自己的罪中死亡;我去的地方,你们不能到。”
21Yesu akawaambia tena, "Naenda zangu nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kufika."
22于是犹太人说:“他说‘我去的地方,你们不能到’,难道他要自杀吗?”
22Basi, viongozi wa Wayahudi wakasema, "Je, atajiua? Mbona anasema: Niendako ninyi hamwezi kufika?"
23耶稣说:“你们是从地上来的,我是从天上来的;你们属这世界,我却不属这世界,
23Yesu akawaambia, "Ninyi mmetoka papa hapa chini, mimi nimetoka juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24所以我对你们说,你们要在自己的罪中死亡;你们若不信我就是‘那一位’,就要在自己的罪中死亡。”
24Ndiyo maana niliwaambieni mtakufa katika dhambi zenu. Kama msipoamini kwamba Mimi ndimi, mtakufa katika dhambi zenu."
25他们就问:“你是谁?”耶稣说:“我不是从起初就告诉你们吗?
25Nao wakamwuliza, "Wewe ni nani?" Yesu akawajibu, "Nimewaambieni tangu mwanzo!
26关于你们,我有许多事要说,要判断;但那差我来的是真实的,我从他那里听见的,就告诉世人。”
26Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake."
27他们不明白耶稣是对他们讲论父的事。
27Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
28所以耶稣说:“你们举起了人子以后,必定知道我就是‘那一位’,并且知道我不凭着自己作什么事;我说的这些话,是照着父所教导我的。
28Basi, Yesu akawaambia, "Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
29那差我来的和我同在,他没有留下我独自一人,因为我常作他喜悦的事。”
29Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza."
30耶稣说这些话的时候,就有许多人信了他。
30Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
31真理必使人自由于是耶稣对信了他的犹太人说:“你们若持守我的道,就真是我的门徒了;
31Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, "Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
32你们必定认识真理,真理必定使你们自由。”
32Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru."
33他们说:“我们是亚伯拉罕的后裔,从来没有被谁奴役过,你怎么说‘你们必得自由’呢?”
33Nao wakamjibu, "Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?"
34耶稣说:“我实实在在告诉你们,凡犯罪的都是罪的奴隶。
34Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35奴隶不能永远住在家里,唯有儿子才可以永远住在家里。
35Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu.
36所以, 神的儿子若使你们自由,你们就真的得自由了。
36Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
37我知道你们是亚伯拉罕的后裔;但你们想杀我,因为你们心里不能容纳我的道。
37Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.
38我所说的,是我在父那里看见的;但你们所作的,却是从你们的父那里听见的。”
38Mimi nasema yale aliyonionyesha Baba, lakini ninyi mwafanya yale aliyowaambieni baba yenu."
39魔鬼的儿女不肯听主的道他们说:“我们的祖宗是亚伯拉罕。”耶稣说:“你们若是亚伯拉罕的子孙,就必作亚伯拉罕所作的。
39Wao wakamjibu, "Baba yetu ni Abrahamu!" Yesu akawaambia, "Kama ninyi mngekuwa watoto wa Abrahamu, mngefanya kama alivyofanya Abrahamu,
40现在我把从 神那里听见的真理告诉了你们,你们竟然想杀我,这不是亚伯拉罕所作的。
40Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu; hata hivyo, ninyi mwataka kuniua. Abrahamu hakufanya hivyo!
41你们要作的,正是你们的父要作的。”他们说:“我们不是从淫乱生的;我们只有一位父,就是 神。”
41Ninyi mnafanya mambo yaleyale aliyofanya babu yenu." Wao wakamwambia, "Sisi si watoto haramu! Tunaye baba mmoja tu, yaani Mungu."
42耶稣说:“如果 神是你们的父,你们就必爱我,因为我是从 神那里来的;我已经来到这里。我不是凭着自己来的,而是 神差了我来。
42Yesu akawaambia, "Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, maana mimi nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43你们为什么不明白我的话呢?因为我的道你们听不进去。
43Kwa nini hamwelewi hayo ninayosema? Ni kwa kuwa hamwezi kuusikiliza ujumbe wangu.
44你们是出于你们的父魔鬼,喜欢按着你们的父的私欲行事。他从起初就是杀人的凶手,不守真理,因为他心里没有真理。他说谎是出于本性,因为他本来就是说谎者,也是说谎的人的父。
44Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; hana msimamo katika ukweli, kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uongo, husema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uongo.
45我讲真理,你们却因此不信我。
45Mimi nasema ukweli, na ndiyo maana ninyi hamniamini.
46你们中间有谁能指证我有罪呢?我既然讲真理,你们为什么不信我呢?
46Nani kati yenu awezaye kuthibitisha kuwa mimi nina dhambi? Ikiwa basi nasema ukweli, kwa nini hamniamini?
47出于 神的,就听 神的话;你们不听,因为你们不是出于 神的。”
47Aliye wa Mungu husikiliza maneno ya Mungu. Lakini ninyi hamsikilizi kwa sababu ninyi si (watu wa) Mungu."
48亚伯拉罕以前耶稣已存在犹太人对耶稣说:“我们说你是撒玛利亚人,并且是鬼附的,不是很对吗?”
48Wayahudi wakamwambia, "Je, hatukusema kweli kwamba wewe ni Msamaria, na tena una pepo?"
49耶稣回答:“我不是鬼附的。我尊敬我的父,你们却侮辱我。
49Yesu akajibu, "Mimi sina pepo; mimi namheshimu Baba yangu, lakini ninyi hamniheshimu.
50我不求自己的荣耀,但有一位是为我求荣耀,并且是审判人的。
50Mimi sijitafutii utukufu wangu mwenyewe; yuko mmoja mwenye kuutafuta utukufu huo, naye ni hakimu.
51我实实在在告诉你们,人若遵守我的道,必定永远不见死亡。”
51Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele."
52犹太人对他说:“现在我们知道你的确是鬼附的。亚伯拉罕死了,先知们也死了,你还说‘人若遵守我的道,必定永远不尝死味’,
52Basi, Wayahudi wakasema, "Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele!
53难道你比我们的祖宗亚伯拉罕还大吗?他死了,先知们也死了;你把自己当作什么人呢?”
53Je, unajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa? Hata na manabii walikufa. Wewe unajifanya kuwa nani?"
54耶稣回答:“如果我荣耀自己,我的荣耀就算不得什么;那使我得荣耀的是我的父,就是你们说是你们的 神的那一位。
54Yesu akawajibu, "Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye ninyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.
55可是你们不认识他,我却认识他。如果我说我不认识他,我就像你们一样是说谎的;然而我认识他,也遵守他的道。
55Ninyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.
56你们的祖宗亚伯拉罕,因为可以看见我的日子就欢喜,既然看见了,他就很快乐。”
56Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi."
57犹太人对他说:“你还不到五十岁,怎会见过亚伯拉罕呢?”
57Basi, Wayahudi wakamwambia, "Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?"
58耶稣说:“我实实在在告诉你们,亚伯拉罕出生以前,我已经存在了。”
58Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko."
59于是他们拿起石头要打他。耶稣却躲起来,从殿里出去了。
59Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka Hekaluni.