聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

7

1耶稣的弟弟也不信他
1Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2犹太人的住棚节快到了,
2Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3耶稣的弟弟就对他说:“你应当离开这里上犹太去,好让你的门徒也可以看见你所行的事;
3Basi ndugu zake wakamwambia, "Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4因为没有人想引人注目,却在暗处行事的。你既然行这些事,就应该向世人显明自己。”
4Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu."
5原来连他的弟弟也不信他。
5(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6耶稣就对他们说:“我的时候还没有到,你们的时候却常常是方便的。
6Basi, Yesu akawaambia, "Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7世人不能恨你们,却憎恨我,因为我指证他们的行为是邪恶的。
7Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8你们上去过节吧!我现在不上去,因为我的时机还没有成熟。”
8Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika."
9他说了这些话以后,仍然住在加利利。
9Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10住棚节时在殿里教导人然而,他的弟弟上去过节以后,他也上去过节,不是公开地去,却是暗中地去。
10Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11过节的时候,犹太人寻找耶稣,说:“那人在哪里呢?”
11Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: "Yuko wapi?"
12群众因他纷纷议论,有的说:“他是好人。”有的说:“不,他是欺骗众人的。”
12Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, "Ni mtu mwema." Wengine walisema, "La! Anawapotosha watu."
13但没有人敢公开讲论他,因为怕犹太人。
13Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14节期当中,耶稣上圣殿去教导人。
14Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15犹太人就希奇,说:“这个人没有学过,怎会通晓经书呢?”
15Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema "Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?"
16耶稣说:“我的教训不是我自己的,而是出于那差我来的。
16Hapo Yesu akawajibu, "Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17人若愿意遵行 神的旨意,就会知道这教训是出于 神,还是我凭着自己的意思说的。
17Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18那凭着自己的意思说的,是求自己的荣誉;但那寻求差他来者的荣耀的,才是真诚的人,在他里面没有不义。
18Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19摩西不是曾经把律法传给你们吗?你们竟然没有一个人遵行律法。你们为什么想要杀我呢?”
19Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?"
20群众回答:“你是鬼附的,谁想要杀你呢?”
20Hapo watu wakamjibu, "Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?"
21耶稣说:“我行了一件事,你们都以为希奇。
21Yesu akawajibu, "Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22摩西曾经把割礼传给你们(其实割礼不是从摩西开始的,而是从列祖开始的),因此,你们在安息日也给人行割礼。
22Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23如果人在安息日行割礼,为的是要遵守摩西的律法,那么我在安息日使一个人痊愈,你们就向我生气吗?
23Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24不要按外貌判断人,总要公公平平地判断人。”
24Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki."
25他是基督吗?当时,有些耶路撒冷人说:“这不是他们想要杀的人吗?
25Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, "Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26你看,他还在公开地讲话,竟然没有人对他说什么,难道官长们真的认为这个人就是基督吗?
26Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27可是我们知道这个人是从哪里来的,只是基督来的时候,没有人知道他是从哪里来的!”
27Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!"
28当时耶稣在殿里教导人,大声说:“你们以为认识我,也知道我从哪里来,其实我不是凭着自己的意思来的,但那差我来的是真实的,你们却不认识他。
28Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, "Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29然而我认识他,因为我从他那里来,也是他差我来的。”
29Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma."
30于是他们想逮捕他,只是没有人下手,因为他的时候还没有到。
30Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31群众中有许多人信了他。他们说:“基督来的时候,他所行的神迹,能比这人所行的更多吗?”
31Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, "Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?"
32法利赛人等想逮捕耶稣法利赛人听见群众纷纷议论这些关于耶稣的事,祭司长和法利赛人就派差役去逮捕耶稣。
32Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33于是耶稣说:“我跟你们在一起的时候不多了,我要回到那差我来的那里去。
33Yesu akasema, "Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34你们要寻找我,却找不着;我所在的地方,你们是不能去的。”
34Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika."
35犹太人彼此说:“这个人要到哪里去,使我们找不着他呢?难道他要到散居在希腊人中的犹太人那里,去教导希腊人吗?
35Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, "Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36他说‘你们要寻找我,却找不着;我所在的地方,你们是不能去的’这话,是什么意思呢?”
36Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?"
37信的人要接受圣灵节期的最后一天,就是最隆重的那一天,耶稣站着高声说:“人若渴了,可以到我这里来喝!
37Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, "Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38信我的人,就像圣经所说的,从他的腹中要涌流出活水的江河来。”
38Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!"
39他这话是指着信他的人要接受圣灵说的;那时圣灵还没有降临,因为耶稣还没有得着荣耀。
39(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40群众因耶稣起了纷争群众中有人听了这些话,就说:“这真是‘那位先知’!”
40Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, "Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!"
41另有人说:“他是基督。”还有人说:“基督是从加利利出来的吗?
41Wengine wakasema, "Huyu ndiye Kristo!" Lakini wengine walisema, "Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42圣经不是说基督是大卫的后裔,是从大卫本乡伯利恒出来的吗?”
42Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!"
43群众因为耶稣的缘故,就起了纷争。
43Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44他们中间有人想逮捕耶稣,只是没有人下手。
44Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45官长不信耶稣差役回到祭司长和法利赛人那里。他们就问差役:“你们为什么没有把他带来?”
45Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, "Kwa nini hamkumleta?"
46差役回答:“从来没有人像他这样讲话的!”
46Walinzi wakawajibu, "Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!"
47法利赛人说:“连你们也受了欺骗吗?
47Mafarisayo wakawauliza, "Je, nanyi pia mmedanganyika?
48官长或法利赛人中间有谁是信他的呢?
48Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49至于这群不明白律法的人,他们是可咒诅的。”
49Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!"
50他们当中有一个人,就是以前来见耶稣的尼哥德慕,对他们说:
50Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51“如果不先听取人的口供,查明他所作的事,我们的律法怎能把他定罪呢?”
51"Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?"
52他们回答:“你也是从加利利出来的吗?你去考查一下,就知道先知是不会从加利利兴起的。”
52Nao wakamjibu, "Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!"
53于是各人都回家去了。(后期抄本才加上7:53-8:11)
53Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;