聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

6

1给五千人吃饱的神迹(太14:13-21;可6:32-44;路9:10-17)
1Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
2有一大群人,因为看见了他在病人身上所行的神迹,就跟随了他。
2Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
3耶稣上了山,同门徒坐在那里。
3Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
4那时犹太人的逾越节近了。
4Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
5耶稣举目观看,见一大群人向他走过来,就对腓力说:“我们从哪里买饼给这些人吃呢?”
5Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, "Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?"
6他说这话,是要试验腓力,因他自己早已知道要怎样作。
6(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
7腓力回答:“就算二百银币买的饼,每人分一点,也是不够的。”
7Filipo akamjibu, "Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!"
8有一个门徒,就是西门.彼得的弟弟安得烈,对耶稣说:
8Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
9“这里有个小孩子,带着五个大麦饼、两条鱼;只是分给这么多人,有什么用呢?”
9"Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?"
10耶稣吩咐他们:“你们叫众人坐下。”原来那地方的草很多,众人就坐下,单是男人的数目约有五千。
10Yesu akasema, "Waketisheni watu." Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
11耶稣拿起饼来,祝谢了,就分给坐着的人;分鱼也是这样,都是随着他们所要的。
11Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12他们吃饱了之后,耶稣对门徒说:“把剩下的零碎收拾起来,免得浪费。”
12Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee."
13门徒就把众人吃剩那五个大麦饼的零碎收拾起来,装满了十二个篮子。
13Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
14众人看见耶稣所行的神迹,就说:“这真是那要到世上来的先知。”
14Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, "Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni."
15耶稣知道群众要来强迫他作王,就独自又退到山上去了。
15Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
16耶稣在海面上行走(太14:22-33;可6:47-51)到了晚上,他的门徒下到海边去。
16Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
17他们上了船,要渡海往迦百农去。那时天已经黑了,耶稣还没有到他们那里。
17wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
18忽然海上起了狂风,波浪翻腾。
18Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19门徒摇橹约行了五六公里,看见耶稣在海面上行走,渐渐靠近船,就害怕起来。
19Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
20耶稣对他们说:“是我,不要怕。”
20Yesu akawaambia, "Ni mimi, msiogope!"
21他们这才把他接上船,船就立刻到了他们要去的地方。
21Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
22耶稣是生命的食物第二天,站在海那边的群众,看见只有一只小船留在那里,并且知道耶稣没有和他的门徒一同上船,门徒是自己去的;
22Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
23不过有几只从提比里亚来的船停在那里,靠近他们在主祝谢以后吃饼的地方。
23Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
24群众见耶稣和门徒都不在那里,就上船往迦百农去找耶稣。
24Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
25他们在对岸找到了耶稣,就问他:“拉比,你几时到这里来的?”
25Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, "Mwalimu, ulifika lini hapa?"
26耶稣回答:“我实实在在告诉你们,你们找我,不是因为看见了神迹,而是因为吃了饼又吃饱了。
26Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27不要为那必朽坏的食物操劳,却要为那存到永生的食物操劳,就是人子所要赐给你们的,因为人子是父 神所印证的。”
27Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho."
28众人又问他:“我们应该作什么,才算是作 神的工作呢?”
28Wao wakamwuliza, "Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?"
29耶稣回答:“信 神所差来的,就是作 神的工了。”
29Yesu akawajibu, "Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma."
30于是他们就说:“你要行什么神迹,让我们看了就信你呢?你到底能作什么呢?
30Hapo wakamwambia, "Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
31我们的祖宗在旷野吃过吗哪,正如经上所记:‘他把从天上来的食物赐给他们吃。’”
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni."
32耶稣对他们说:“我实实在在告诉你们,不是摩西把那从天上来的食物赐给你们,而是我父把天上来的真食物赐给你们;
32Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
33因为 神的食物就是从天上降下来,把生命赐给世人的那一位。”
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima."
34他们对耶稣说:“主啊,求你常把这食物赐给我们。”
34Basi, wakamwambia, "Mheshimiwa, tupe daima mkate huo."
35耶稣说:“我就是生命的食物,到我这里来的,必定不饿;信我的,永远不渴。
35Yesu akawaambia, "Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
36但我告诉你们,你们虽然见了我,还是不信。
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
37凡是父赐给我的人,必到我这里来;到我这里来的,我决不丢弃他,
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
38因为我从天上降下来,不是要行自己的意思,而是要行那差我来者的旨意。
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
39那差我来者的旨意就是:他所赐给我的人,我连一个也不失落,并且在末日我要使他们复活。
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
40因为我父的旨意,是要使所有看见了子而信的人有永生,并且在末日我要使他们复活。”
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho."
41犹太人因为耶稣说“我是从天上降下来的食物”,就纷纷议论他。
41Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: "Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni."
42他们说:“这不是约瑟的儿子耶稣吗?他的父母我们不都认识吗?他现在怎么说‘我是从天上降下来的’呢?”
42Wakasema, "Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?"
43耶稣回答:“你们不要彼此议论。
43Yesu akawaambia, "Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
44如果不是差我来的父吸引人,就没有人能到我这里来;到我这里来的,在末日我要使他复活。
44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
45先知书上记着:‘众人都必受 神的教导。’凡听见从父那里来的教训而又学习的,必到我这里来。
45Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
46这不是说有人见过父;只有从 神那里来的那一位,他才见过父。
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47我实实在在告诉你们,信的人有永生。
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
48我就是生命的食物,
48Mimi ni mkate wa uzima.
49你们的祖宗在旷野吃过吗哪,还是死了。
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
50这是从天上降下来的食物,使人吃了就不死。
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
51我就是从天上降下来生命的食物,人若吃了这食物,就必活到永远。我要赐的食物就是我的肉,是为了世人的生命而赐的。”
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu."
52于是,犹太人彼此争论,说:“这个人怎能把他的肉给我们吃呢?”
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
53耶稣就对他们说:“我实实在在告诉你们,你们若不吃人子的肉,不喝人子的血,就没有生命在你们里面。
53Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
54吃我肉、喝我血的,就有永生,在末日我要使他复活;
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
55因为我的肉是真正的食物,我的血是真正的饮料。
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56吃我肉、喝我血的人,就住在我里面,我也住在他里面。
56Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
57正如永活的父差遣了我,我也因父活着;照样,吃我肉的人也必因我而活。
57Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
58这就是从天上降下来的食物,不像吗哪,你们的祖宗吃过,还是死了;吃这食物的,必活到永远。”
58Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele."
59这些话是耶稣在迦百农会堂里教导人的时候说的。
59Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
60永生之道他的门徒中,有许多人听了,就说:“这话很难,谁能接受呢?”
60Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, "Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?"
61耶稣心里知道门徒为了这事议论纷纷,就对他们说:“这话使你们动摇吗?
61Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, "Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
62如果你们看见人子升到他原来所在的地方,又怎样呢?
62Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
63使人活的是灵,肉体是无济于事的。我对你们所说的话是灵、是生命。
63Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
64然而你们中间却有不信的人。”原来从起初耶稣就知道那些不信的是谁,那要把他出卖的又是谁。
64Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini." (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
65耶稣跟着说:“所以我对你们说过,如果不是父所赐的,没有人能到我这里来。”
65Kisha akasema, "Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu."
66从此,他的门徒中有许多人退去了,不再与他同行。
66Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
67于是耶稣对十二门徒说:“你们也想离去吗?”
67Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, "Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?"
68西门.彼得回答:“主啊,你有永生之道,我们还跟从谁呢?
68Simoni Petro akamjibu, "Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele.
69我们已经相信,并且知道你是 神的圣者。”
69Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu."
70耶稣说:“我不是拣选了你们十二个人吗?但你们中间有一个是魔鬼。”
70Yesu akawaambia, "Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!"
71耶稣这话是指着加略人西门的儿子犹大说的,因为他虽然是十二门徒之一,却要出卖耶稣。
71Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.