1治好病了三十八年的人
1Baada ya hayo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, naye Yesu akaenda Yerusalemu.
2在耶路撒冷靠近羊门有一个水池,希伯来话叫作毕士大,池边有五处走廊。
2Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, kulikuwa na bwawa la maji liitwalo kwa Kiebrania Bethzatha, ambalo lilikuwa na baraza tano zenye matao.
3在那里躺着许多病人,有瞎眼的、瘸腿的和瘫痪的。
3Humo barazani mlikuwa na wagonjwa wengi wamekaa: vipofu, viwete na waliopooza. Walikuwa wakingojea maji yatibuliwe,
4(有些抄本有以下一段:“他们等候水动,4因为有主的使者按时下去搅动池水,水动之后,谁先下去,无论什么病,必得痊愈。”)
4maana mara kwa mara malaika alishuka majini nyakati fulani na kuyatibua. Mtu yeyote aliyekuwa wa kwanza kuingia majini baada ya maji kutibuliwa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.
5那里有一个人,病了三十八年。
5Basi, hapo palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane.
6耶稣看见他躺着,知道他病了很久,就问他:“你要痊愈吗?”
6Naye alipomwona huyo mtu amelala hapo, akatambua kwamba alikuwa amekaa hapo kwa muda mrefu, akamwuliza, "Je, wataka kupona?"
7病人回答:“先生,水动的时候,没有人把我放在池里;自己想去的时候,总是给别人抢先。”
7Naye akajibu, "Mheshimiwa, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia."
8耶稣对他说:“起来,拿着你的褥子走吧。”
8Yesu akamwambia, "Inuka, chukua mkeka wako utembee."
9那人立刻痊愈,就拿起褥子走了。那天正是安息日。
9Mara huyo mtu akapona, akachukua mkeka wake, akatembea. Jambo hili lilifanyika siku ya Sabato.
10因此犹太人对那医好了的人说:“今天是安息日,你拿着褥子是不可以的。”
10Kwa hiyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia huyo mtu aliyeponywa, "Leo ni Sabato, si halali kubeba mkeka wako."
11他却回答:“那使我痊愈的对我说:‘拿起你的褥子走吧’。”
11Lakini yeye akawaambia, "Yule mtu aliyeniponya ndiye aliyeniambia: Chukua mkeka wako, tembea."
12他们就问:“那对你说‘拿起来走吧’的是谁?”
12Nao wakamwuliza, "Huyo mtu aliyekwambia: Chukua mkeka wako, tembea, ni nani?"
13那医好了的人不知道他是谁,因为那里人很多,耶稣已经避开了。
13Lakini yeye hakumjua huyo mtu aliyemponya, maana Yesu alikuwa amekwisha ondoka mahali hapo, kwani palikuwa na umati mkubwa wa watu.
14后来,耶稣在殿里遇见那人,对他说:“你已经痊愈了,不可再犯罪,免得招来更大的祸患。”
14Basi, baadaye Yesu alimkuta huyo aliyeponywa Hekaluni, akamwambia, "Sasa umepona; usitende dhambi tena, usije ukapatwa na jambo baya zaidi."
15那人就去告诉犹太人,使他痊愈的就是耶稣。
15Huyo mtu akaenda, akawaambia viongozi wa Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemponya.
16从此犹太人就迫害耶稣,因为他常常在安息日作这些事。
16Kwa vile Yesu alifanya jambo hilo siku ya Sabato, Wayahudi walianza kumdhulumu.
17耶稣却对他们说:“我父作工直到现在,我也作工。”
17Basi, Yesu akawaambia, "Baba yangu anafanya kazi daima, nami pia nafanya kazi."
18因此犹太人就更想杀耶稣,因为他不但破坏安息日,而且称 神为自己的父,把自己与 神当作平等。
18Kwa sababu ya maneno haya, viongozi wa Wayahudi walizidi kutafuta njia ya kumwua Yesu: si kwa kuwa aliivunja Sheria ya Sabato tu, bali pia kwa kuwa alisema kwamba Mungu ni Baba yake, na hivyo akajifanya sawa na Mungu.
19人子的权柄耶稣又对他们说:“我实实在在告诉你们,子靠着自己不能作什么,只能作他看见父所作的;因为父所作的事,子也照样作。
19Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mwana hawezi kufanya kitu peke yake; anaweza tu kufanya kile anachomwona Baba akikifanya. Maana kile anachofanya Baba, Mwana hukifanya vilevile.
20父爱子,把自己所作的一切指示给他看,还要把比这些更大的事指示给他看,使你们惊奇。
20Baba ampenda Mwana, na humwonyesha kila kitu anachokifanya yeye mwenyewe, tena atamwonyesha mambo makuu kuliko haya, nanyi mtastaajabu.
21父怎样叫死人复活,使他们得生命,子也照样随自己的意思使人得生命。
21Kama vile Baba huwafufua wafu na kuwapa uzima, vivyo hivyo naye Mwana huwapa uzima wale anaopenda.
22父不审判人,却已经把审判的权柄完全交给子,
22Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana,
23使所有的人尊敬子好像尊敬父一样。不尊敬子的,就是不尊敬那差他来的父。
23ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba ambaye amemtuma.
24我实实在在告诉你们,那听见我的话又信那差我来的,就有永生,不被定罪,而是已经出死入生了。
24"Kweli nawaambieni, anayesikia neno langu, na kumwamini yule aliyenituma, anao uzima wa milele. Hatahukumiwa kamwe, bali amekwisha pita kutoka kifo na kuingia katika uzima.
25我实实在在告诉你们,时候将到,现在就是了,死人要听见 神儿子的声音,听见的人就要活了。
25Kweli nawaambieni, wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wafu wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu, nao watakaoisikia, wataishi.
26就如父是生命的源头,照样他也使子成为生命的源头,
26Kama vile Baba alivyo asili ya uhai, ndivyo pia alivyomjalia Mwanawe kuwa asili ya uhai.
27并且把执行审判的权柄赐给他,因为他是人子。
27Tena amempa mamlaka ya kuhukumu kwa sababu yeye ni Mwana wa Mtu.
28你们不要把这事看作希奇,因为时候将到,那时所有在坟墓里的都要听见他的声音,
28Msistaajabie jambo hili; maana wakati unakuja ambapo wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake,
29并且都要出来;行善的复活得生命,作恶的复活被定罪。
29nao watafufuka: wale waliotenda mema watafufuka na kuishi, na wale waliotenda maovu watafufuka na kuhukumiwa.
30给耶稣作见证的“我靠着自己不能作什么,我怎样听见,就怎样审判。我的审判是公义的,因为我不寻求自己的意思,只求那差我来者的旨意。
30"Mimi siwezi kufanya kitu kwa uwezo wangu mwenyewe. Mimi nina hukumu kama ninavyosikia kutoka kwa Baba, nayo hukumu yangu ni ya haki. Nia yangu si kufanya nipendavyo mwenyewe, bali apendavyo yule aliyenituma.
31我若为自己作证,我的见证就不真。
31Nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushahidi wangu hauwezi kukubaliwa kuwa wa kweli.
32然而另有一位为我作证的,我知道他为我作的见证是真的。
32Lakini yuko mwingine ambaye hutoa ushahidi juu yangu, nami najua kwamba yote anayosema juu yangu ni ya kweli.
33你们曾经派人到约翰那里,他为真理作过见证。
33Ninyi mlituma ujumbe kwa Yohane naye aliushuhudia ukweli.
34我不接受从人而来的见证,但我说这些事,是要你们得救。
34Si kwamba mimi nautegemea ushahidi wa wanadamu, lakini nasema mambo haya ili mpate kuokolewa.
35约翰是一盏点亮的灯,你们情愿暂时在他的光中欢乐。
35Yohane alikuwa kama taa iliyokuwa ikiwaka na kuangaza, nanyi mlikuwa tayari kufurahia mwanga huo kwa kitambo.
36但我有比约翰更大的见证,因为父赐给我要我完成的工作,就是我所要作的,证明我是父所差来的。
36Lakini mimi nina ushahidi juu yangu ambao ni mkuu zaidi kuliko ule wa Yohane. Kwa maana kazi ninazofanya, kazi alizonipa Baba nizifanye, ndizo zinazonishuhudia kwamba Baba ndiye aliyenituma.
37差我来的父亲自为我作了见证。他的声音,你们从没有听过;他的容貌,你们从没有见过;
37Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Ninyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake,
38他的道,你们也不放在心里,因为你们不信他所差来的那一位。
38na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma.
39你们研究圣经,因为你们认为圣经中有永生,其实为我作证的就是这圣经,
39Ninyi huyachunguza Maandiko Matakatifu mkidhani kwamba ndani yake mtapata uzima wa milele; na kumbe maandiko hayohayo yananishuhudia!
40然而你们却不肯到我这里来得生命。
40Hata hivyo, ninyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima.
41“我不接受从人而来的称赞;
41"Shabaha yangu si kupata sifa kutoka kwa watu.
42我知道你们心里没有 神的爱。
42Lakini nawajua ninyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.
43我奉我父的名而来,你们不接待我;如果有别人以自己的名义而来,你们倒接待他。
43Mimi nimekuja kwa mamlaka ya Baba yangu, lakini hamnipokei; bali mtu mwingine akija kwa mamlaka yake mwenyewe, mtampokea.
44你们彼此接受称赞,却不寻求从独一的 神而来的称赞,怎么能信呢?
44Mwawezaje kuamini, hali ninyi mnapenda kupokea sifa kutoka kwenu ninyi wenyewe, wala hamtafuti sifa kutoka kwake yeye aliye peke yake Mungu?
45不要以为我要向父控告你们,有一位控告你们的,就是你们所仰赖的摩西。
45Msifikiri kwamba mimi nitawashtaki kwa Baba. Mose ambaye ninyi mmemtumainia ndiye atakayewashtaki.
46你们若信摩西,也必信我,因为他所写的书曾论及我。
46Kama kweli mngemwamini Mose, mngeniamini na mimi pia; maana Mose aliandika juu yangu.
47你们若不信他所写的,怎能信我的话呢?”
47Lakini hamuyaamini yale aliyoandika, mtawezaje basi, kuamini maneno yangu?"