聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Luke

22

1商议怎样杀害耶稣(太26:1-5;可14:1-2、10-11。参约11:45-53)
1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2祭司长和经学家设法怎样杀害耶稣,因为他们惧怕群众。
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3那时,撒但已经进入加略人犹大的心,他原是十二门徒中的一个。
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4他去与祭司长和守殿官商量怎样把耶稣交给他们。
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5他们很高兴,约定了给他银子。
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6他答应了,就寻找机会,要趁群众不在的时候,把耶稣交给他们。
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7预备逾越节的筵席(太26:17-19;可14:12-16)除酵日到了,在这一天应当宰杀逾越节的羊羔。
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8耶稣差派彼得和约翰,说:“你们去为我们预备逾越节的晚餐给我们吃。”
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
9他们说:“你要我们在哪里预备呢?”
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
10他说:“你们进了城,必有一个人顶着水罐,迎面而来,你们就跟着他,到他所进的那一家,
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11对家主说,老师问你:‘客厅在哪里?我和门徒好在那里吃逾越节的晚餐。’
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12他必指示你们楼上一间布置整齐的大房子,你们就在那里预备。”
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
13他们去了,所遇见的正像耶稣所说的一样,就预备好了逾越节的晚餐。
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14最后的晚餐(太26:20-24、26-29;可14:17-21;约13:21-30。参林前11:23-25)到了时候,耶稣和使徒一同吃饭。
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15他说:“我十分愿意在受难以前,跟你们吃这逾越节的晚餐。
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16我告诉你们,我决不再吃这晚餐,直到它成就在 神的国里。”
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
17耶稣接过杯来,感谢了,说:“你们拿这个,大家分着喝。
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18我告诉你们,从今以后,我决不再喝这葡萄酒,直到 神的国来临。”
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
19他拿起饼来,感谢了,擘开递给他们,说:“这是我的身体,为你们舍的,你们应当这样行,为的是记念我。”
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
20饭后,他照样拿起杯来,说:“这杯是用我的血所立的新约,这血是为你们流的。
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21你看,出卖我的人的手和我一同在桌子上,
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22人子固然要照所预定的离世,但出卖人子的那人有祸了!”
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
23于是,门徒彼此对问,他们中间谁要作这事。
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24门徒再争论谁最大门徒中间又起了争论:他们中间谁是最大的。
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25耶稣对他们说:“各国都有君王统治他们,他们的掌权者称为恩主,
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26但你们却不要这样;你们中间最大的,应当像最小的;作首领的,应当像服事人的。
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27哪一个大呢?是坐着吃喝的还是服事人的呢?不是坐着吃喝的吗?然而我在你们中间,如同服事人的。
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28我在磨炼之中,常常和我同在的就是你们。
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29父怎样把王权赐给我,我也照样赐给你们,
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30叫你们在我的国里坐在我的席上吃喝,又坐在宝座上审判以色列的十二支派。
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31预言彼得不认主(太26:31-35;可14:27-31;约13:36-38)“西门,西门,撒但设法要得着你们,好筛你们像筛麦子一样;
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32但我已经为你祈求,叫你的信心不至失掉。你回头的时候,要坚固你的弟兄。”
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
33彼得说:“主啊!我已经准备好要跟你一同下监,一同死。”
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
34耶稣说:“彼得,我告诉你,今天鸡叫以前,你会三次说不认得我。”
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
35要带钱囊、口袋和刀耶稣又对他们说:“从前我差你们出去,没有带钱囊、口袋、鞋子,你们缺乏什么没有?”他们说:“没有。”
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
36耶稣说:“但现在,有钱囊的应当带着,有口袋的也是这样;没有刀的,要卖掉衣服去买刀。
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37我告诉你们,‘他被列在不法者之中’这句经文,必定应验在我身上,因为关于我的事必然成就。”
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
38他们说:“主啊,请看,这里有两把刀。”耶稣说:“够了。”
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
39在客西马尼祷告(太26:36-46;可14:32-42)耶稣照常到橄榄山去,门徒也跟着他。
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40到了那里,他对门徒说:“你们应当祷告,免得陷入试探。”
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
41于是耶稣离开他们约有扔一块石头那么远,跪下祷告说:
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42“父啊,如果你愿意,就把这杯拿走!但不要成就我的意思,只要成就你的旨意。”
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
43(有些抄本有第43、44节:“有一位天使从天上显现,加给他力量。耶稣非常伤痛,祷告更加恳切,汗如大血点滴在地上。”)
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45他祷告完了,就起来到门徒那里,看见他们因为忧愁都睡着了,
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46就说:“你们为什么睡觉呢?起来祷告!免得陷入试探。”
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
47耶稣被捕(太26:47-56;可14:43-50;约18:3-11)耶稣还在说话的时候,来了一群人,十二门徒中的犹大走在前头,到了耶稣跟前要用嘴亲他。
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48耶稣对他说:“犹大,你用亲嘴作暗号出卖人子吗?”
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
49左右的人见了,就说:“主啊,我们用刀砍好吗?”
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
50他们中间有一个人砍了大祭司的仆人一刀,削掉他的右耳。
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51耶稣说:“由他们吧!”就摸那人的耳朵,医好了他。
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52耶稣对那些前来捉拿他的祭司长、守殿官和长老说:“你们带着刀棒出来,把我当作强盗捉拿吗?
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53我天天跟你们在殿里,你们不向我下手;但现在是你们的时候了,也是黑暗掌权的时候了。”
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
54彼得三次不认主(太26:57-58、69-75;可14:53-54、66-72;约18:12-18、25-27)他们拿住耶稣,押到大祭司家里,彼得远远地跟着。
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55他们在院内生了火,一同坐着,彼得也坐在他们中间。
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56有一个使女,见他面向火光坐着,就注视他,说:“这人是和他一伙的。”
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
57彼得却否认,说:“你这个女人,我不认得他。”
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
58不久,另一个人看见他,就说:“你也是他们中间的一个。”彼得说:“你这个人,我不是。”
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
59大约过了一小时,又有一个人肯定地说:“这人真是和他一伙的,因为他也是加利利人。”
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
60彼得说:“你这个人,我不知道你说的是什么!”他还在说话的时候,鸡就叫了。
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61主转过身来看彼得,彼得就想起主对他说过的话:“今天鸡叫以前,你要三次说不认得我。”
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
62他就出去痛哭。
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
63公议会审问耶稣(太26:59-68;可14:55-65;约18:19-24)看管耶稣的人戏弄他,
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64蒙住他的眼睛问他:“你说预言吧,说打你的是谁。”
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
65他们还说了许多别的辱骂他的话。
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66天一亮,民间的长老、祭司长和经学家就都聚集,把他带到他们的公议会里,说:
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67“你若是基督,就告诉我们吧。”耶稣说:“就算我告诉你们,你们也决不相信。
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68如果我问你们,你们也决不回答。
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69从今以后,人子要坐在 神权能的右边。”
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
70他们说:“那么你是 神的儿子吗?”耶稣说:“你们说了,我是。”
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
71他们说:“我们还需要什么证供呢?我们亲自听见他所说的话了。”
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."