1穷寡妇的奉献(可12:41-44)
1Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
2他又看见一个穷寡妇,投入两个小钱,
2akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
3就说:“我实在告诉你们,这个穷寡妇所投的,比众人投的更多。
3Basi, akasema, "Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
4因为这些人都是把自己剩余的投进去作奉献,这寡妇是自己不足,却把所有养生的都投进去了。”
4Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi."
5预言圣殿被毁(太24:1-2;可13:1-2)有人在谈论圣殿,是用美丽的石头和供物装饰的。耶稣说:
5Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
6“你们看见的这些,到了日子,必没有一块石头留在另一块石头上面,每一块都要拆下来。”
6"Haya yote mnayoyaona--zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
7这世代终结的预兆(太10:17-22,24:3-14;可13:3-13)那些人问他:“老师,什么时候会有这些事呢?这些事要发生的时候,有什么预兆呢?”
7Basi, wakamwuliza, "Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?"
8他说:“你们要小心,不要被人迷惑。因为有许多人要来,假冒我的名说:‘我就是基督’,又说:‘时候近了。’你们不要跟从这些人。
8Yesu akawajibu, "Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
9你们要听见战乱和暴动,但不要惊慌,因为这些事是必先发生的,不过结局却不会立刻就到。”
9Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado."
10过了一会儿,耶稣又对他们说:“一个民族要起来攻打另一个民族,一个国家要起来攻打另一个国家。
10Halafu akaendelea kusema: "Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
11到处必有大地震、饥荒和瘟疫,天上必有又恐怖又巨大的预兆。
11Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
12但在这一切以先,人必为我的名,下手拘捕、迫害你们,把你们交给会堂,下在监里,甚至押到君王和总督面前,
12Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
13结果却成了你们见证的机会。
13Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
14所以,你们应当心里镇定,用不着预先思虑怎样申辩。
14Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
15因为我必赐给你们口才、智慧,是你们所有的敌人不能抵抗,也不能驳倒的。
15kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
16你们也会被父母、弟兄、亲戚、朋友出卖,他们又要害死你们一些人。
16Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
17你们要因我的名,被众人恨恶,
17Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
18然而连你们的一根头发,也必不失落。
18Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
19你们要以坚忍的心志,赢取自己的灵魂。
19Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
20预言耶路撒冷被毁(太24:15-21;可13:14-19)“当你们看见耶路撒冷被军队围困的时候,就知道它荒凉的日子近了。
20"Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
21那时,住在犹太的,应该逃到山上;住在城里的,要离开;住在乡下的,不要进城。
21Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
22因为这是报仇的日子,使经上的一切话都得应验。
22Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
23当那些日子,怀孕的和乳养孩子的有祸了!因为大灾难要临到这地,烈怒要临到这民。
23Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
24他们将倒在刀下,被掳到各国,耶路撒冷必被外族人践踏,直到外族人的日期满足。
24Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
25人子必驾云降临(太24:29-35;可13:24-31)“日月星辰将有异兆;在地上,各国也要因着海洋波涛的咆哮而困苦不安。
25"Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
26天上的万象震动,人因为等待即将临到世界的事,都吓昏了。
26Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27那时,他们要看见人子,带着能力,满有荣耀,驾着云降临。
27Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
28一有这些事,你们就当挺身昂首,因为你们的救赎近了。”
28Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia."
29耶稣又给他们讲了一个比喻:“你们看看无花果树和各样的树。
29Kisha akawaambia mfano: "Angalieni mtini na miti mingine yote.
30它们什么时候发芽,你们看见了,就知道夏天近了。
30Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
31同样,你们什么时候看见这些事发生,也应该知道 神的国近了。
31Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32我实在告诉你们,这一切都必定发生,然后这世代才会过去。
32Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
33天地都过去,但我的话决不会废去。
33Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
34警醒祈求“你们应当自己小心,免得在贪食醉酒和生活的挂虑压住你们的心的时候,那日子突然临到你们,
34"Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
35正如网罗临到全地的所有居民。
35Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
36你们要时刻警醒,常常祈求,好让你们能逃避这一切要发生的事,可以站在人子面前。”
36Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu."
37耶稣白天在殿里教导人,晚上就到橄榄山上去过夜。
37Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
38群众清早起来上圣殿,到他那里要听他讲道。
38Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.