聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Luke

20

1质问耶稣凭什么权柄作事(太21:23-27;可11:27-33)
1Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2对他说:“告诉我们,你凭着什么权柄作这些事?给你这权柄的是谁?”
2wakasema, "Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?"
3他回答他们:“我也要问你们一句话,你们告诉我:
3Yesu akawaambia, "Na mimi nitawaulizeni swali:
4约翰的洗礼是从天上来的,还是从人来的呢?”
4mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?"
5他们就彼此议论说:“如果我们说:‘是从天上来的’,他就会问:‘那你们为什么不相信他呢?’
5Lakini wao wakajadiliana hivi: "Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6如果我们说:‘是从人来的’,众人都会用石头打我们,因为他们都认定约翰是先知。”
6Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii."
7于是他们回答耶稣:“我们不知道是从哪里来的。”
7Basi, wakamwambia, "Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi."
8耶稣说:“我也不告诉你们,我凭着什么权柄作这些事。”
8Yesu akawaambia, "Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
9佃户的比喻(太21:33-46;可12:1-12)于是耶稣向众人讲了这个比喻:“有一个人栽种了一个葡萄园,租给佃户,就远行去了很久。
9Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10到了时候,园主派了一个仆人到佃户那里,叫他们把葡萄园当纳的果子交给他。佃户却打了他,放他空手回去。
10Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11园主又派另一个仆人去,佃户又打了他,并且侮辱他,也叫他空手回去。
11Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12于是他又派第三个去,佃户把他打伤,赶他走了。
12Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13葡萄园的主人说:‘怎么办呢?我要派我的爱子去,也许这一个他们会尊敬的。’
13Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14佃户一看他,就彼此商议说:‘这是继承产业的,让我们杀了他,那么,产业就成为我们的了。’
14Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15于是他们把园主的爱子推出葡萄园外杀了。主人要怎样对待他们呢?
15Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua." Yesu akauliza, "Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16他要来除掉这些佃户,把葡萄园租给别人。”他们听见了就说:“千万不要有这样的事发生!”
16Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu." Watu waliposikia maneno hayo, walisema: "Hasha! Yasitukie hata kidogo!"
17耶稣看着他们,说:“那么,‘建筑工人所弃的石头,成了房角的主要石头’,这经文是什么意思呢?
17Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, "Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18凡是跌在那石头上的,就必摔碎;那石头掉在谁的身上,就必把他压得粉碎。”
18Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa."
19经学家和祭司长知道这比喻是针对他们说的,当时就想动手拿他,可是又害怕群众。
19Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20以纳税的事问难耶稣(太22:15-22;可12:13-17)经学家和祭司长差派奸细伪装好人去窥探耶稣,要抓着他的把柄,好把他交由总督全权裁决。
20Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21奸细问他:“老师,我们知道你所说所教的都对,并且不讲情面,只照着真理把 神的道教导人。
21Hao wapelelezi wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22我们纳税给凯撒可以不可以?”
22Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!"
23耶稣看透他们的诡计,就对他们说:
23Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24“给我一个银币看看,上面是谁的像,谁的名号?”他们说:“凯撒的。”
24"Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?"
25耶稣说:“这样,凯撒的应当归给凯撒, 神的应当归给 神。”
25Nao wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu."
26他们在群众面前,不能抓住耶稣的把柄,又希奇他的回答,就沉默下来。
26Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27人复活后不娶不嫁(太22:23-33;可12:18-27)撒都该人向来否认有复活的事,他们当中有几个人来问耶稣:
27Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28“老师,摩西曾写给我们说:‘如果一个人娶了妻子,还没有儿女就死了,他弟弟就应当娶他的妻子,为哥哥立后。’
28"Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29从前有兄弟七人,头一个娶了妻子,没有孩子就死了。
29Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30第二个、
30Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31第三个,也娶过她;七个都是这样,都没有留下孩子就死了。
31na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba--wote walikufa bila kuacha watoto.
32后来那女人也死了。
32Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33那么,这女人在复活的时候,要作哪一个的妻子呢?因为七个人都娶过她。”
33Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba."
34耶稣说:“这世界的人又娶又嫁,
34Yesu akawaambia, "Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;
35但配得那世界的,又配从死人中复活的人,也不娶也不嫁。
35lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.
36他们和天使一样,不能再死;既然是复活了的人,就是 神的儿女了。
36Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37至于死人复活的事,摩西在荆棘篇上提过,他称主是亚伯拉罕的 神、以撒的 神、雅各的 神;
37Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 神不是死人的 神,而是活人的 神,因为在他那里的人都是活的。”
38Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye."
39经学家中有几个说:“老师,你说得好。”
39Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, "Mwalimu, umejibu vema kabisa."
40从此他们再不敢问他什么了。
40Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41大卫称基督为主(太22:41-45;可12:35-37)耶稣问他们:“人怎么能说基督是大卫的子孙呢?
41Yesu akawauliza, "Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42大卫自己在诗篇上说:‘主对我的主说:你坐在我的右边,
42Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43等我使你的仇敌作你的脚凳。’
43mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44大卫既然称他为主,他又怎会是大卫的子孙呢?”
44Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?"
45提防经学家(太23:1-36;可12:38-40)众人听着的时候,耶稣对门徒说:
45Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46“你们要提防经学家,他们好穿长袍走来走去,喜欢人在巿中心向他们问安,并且喜欢会堂里的高位、筵席上的首座。
46"Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47他们吞没了寡妇的房产,又用冗长的祷告作掩饰。这等人必受更重的刑罚。”
47Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!"