1税吏长撒该
1Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2有一个人名叫撒该,是税吏长,又很富有。
2Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3他想看看耶稣是怎么样的,因为人多,他又身材矮小,就看不见。
3Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4于是他跑到前头,爬上一棵桑树,要看看耶稣,因为耶稣就要从那里经过。
4Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5耶稣到了那里,往上一看,对他说:“撒该,快下来,今天我要住在你家里。”
5Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, "Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako."
6他就赶快下来,欢欢喜喜地接待耶稣。
6Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7众人看见就纷纷议论说:“他竟到罪人家里去住宿!”
7Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, "Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi."
8撒该站着对主说:“主啊,请看,我要把家财的一半分给穷人,我若敲诈了谁,就还他四倍。”
8Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, "Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne."
9耶稣说:“今天救恩到了这家,他也是亚伯拉罕的子孙。
9Yesu akamwambia, "Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10因为人子来,是要寻找拯救失丧的人。”
10Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea."
11十个仆人的比喻(参太25:14-30)众人听这些话的时候,因为耶稣已经接近耶路撒冷,又因他们以为 神的国快要出现,他就讲了一个比喻,
11Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12说:“有一个贵族往远方去要接受王位,然后回来。
12Hivyo akawaambia, "Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13他叫了自己的十个仆人来,给他们一千银币,说:‘你们拿去作生意,等到我回来。’
13Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14他本国的人却恨他,就派使者跟着去说:‘我们不愿意这个人作王统治我们。’
14Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15他得了王位回来,就吩咐把那些领了钱的仆人召来,要知道他们作生意赚了多少。
15"Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16第一个走过来说:‘主啊,你的一百银币,已经赚了一千。’
16Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17主人说:‘好,良善的仆人,你既然在最小的事上忠心,可以有权管理十座城。’
17Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18第二个来说:‘主啊,你的一百银币,已经赚了五百。’
18Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19主人说:‘你可以管理五座城。’
19Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20另一个来说:‘主啊,你看,你的一百银币,我一直保存在手巾里,
20"Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21因为我怕你,你一向是严厉的人,没有存的要提取,没有种的要收割。’
21kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22主人说:‘可恶的仆人!我要凭你的口定你的罪。你知道我是严厉的人,没有存的要提取,没有种的要收割吗?
22Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23那你为什么不把我的钱存入银行,等我回来的时候,把它连本带利取回来呢?’
23Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24他就对侍卫说:‘夺过他的一百银币,给那有一千的。’
24Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25他们说:‘主啊,他已经有一千银币了。’
25Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26主人说:‘我告诉你们,凡是有的,还要给他;没有的,就算他有什么也要拿去。
26Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27至于我那些仇敌,就是不愿意我作王统治他们的,把他们拉到这里来,在我面前杀掉!’”
27Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu."
28骑驴进耶路撒冷(太21:1-9;可11:1-10;约12:12-15)耶稣讲完这些话,就往前走,上耶路撒冷去。
28Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29将到伯法其和伯大尼,就在橄榄山那里,他差派两个门徒,
29Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30说:“你们往对面的村子里去,就会看见一头从来没有人骑过的小驴,拴在那里,把它解开牵来。
30akawaambia: "Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31如果有人问为什么解开它,你们要这样说:‘主需要它。’”
31Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye."
32被差的人去了,发现和主所说的一样。
32Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33他们解开小驴的时候,主人问他们:“你们为什么解开它?”
33Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, "Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?"
34他们说:“主需要它。”
34Nao wakawajibu, "Bwana anamhitaji."
35他们把小驴牵到耶稣那里,把自己的衣服搭在上面,扶着耶稣上去。
35Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36耶稣前行的时候,众人把自己的衣服铺在路上。
36Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37他走近耶路撒冷,快要下橄榄山的时候,全体门徒因为所看见的一切神迹,就欢乐起来,大声赞美 神,
37Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38说:“奉主名来的王,是应当称颂的!在天上有和平,在至高之处有荣耀!”
38wakawa wanasema: "Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!"
39群众中有几个法利赛人对他说:“先生,责备你的门徒吧!”
39Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, "Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!"
40耶稣说:“我告诉你们,他们若不出声,石头都要呼叫了。”
40Yesu akawajibu, "Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti."
41为耶路撒冷哀哭耶稣走近耶路撒冷的时候,看见了城,就为城哀哭,
41Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42说:“巴不得你在这日子,知道关于你平安的事,但现在这事在你眼前是隐藏的。
42akisema: "Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43日子将到,你的仇敌必筑垒攻击你,周围环绕你,四面困住你,
43Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44要摧毁你和你里面的儿女,没有一块石头留在另一块石头上面,因为你不知道那眷顾你的时期。”
44Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa."
45洁净圣殿(太21:12-17;可11:15-19;约2:13-22)耶稣进了圣殿,就赶走作买卖的人,
45Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46对他们说:“经上记着:‘我的殿是祷告的殿’,你们竟把它弄成贼窝了。”
46akisema, "Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi."
47他天天在圣殿里教导人,祭司长、经学家和民间的首领,都想杀害他;
47Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48但他们不知道要怎样下手,因为众人都围着他,听他的教训。
48lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.