1寡妇与法官的比喻
1Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2他说:“某城里有一个法官,不惧怕 神,也不尊敬人。
2Alisema: "Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3那城里有一个寡妇,常常来到他那里,说:‘求你给我伸冤,使我脱离我的对头!’
3Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4他多次不肯,后来心里说:‘我虽然不惧怕 神,也不尊敬人,
4Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5只是因为这寡妇常常来麻烦我,就给她伸冤吧,免得她不断地来缠扰我。’”
5lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!"
6主说:“你们听听这不义的法官所说的话吧。
6Basi, Bwana akaendelea kusema, "Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7难道 神不会为昼夜呼吁他的选民伸冤吗?难道 神会耽误他们吗?
7Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8我告诉你们,他要快快地给他们伸冤。然而人子来的时候,在世上找得到这种信心吗?”
8Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?"
9税吏和法利赛人的祷告耶稣向那些自恃为义、轻视别人的人,讲了这个比喻:
9Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10“有两个人上圣殿去祈祷,一个是法利赛人,一个是税吏。
10"Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11法利赛人站着,祷告给自己听,这样说:‘ 神啊,我感谢你,我不像别人,勒索、不义、奸淫,也不像这个税吏。
11Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12我一个礼拜禁食两次,我的一切收入都奉献十分之一。’
12Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13税吏却远远站着,连举目望天也不敢,只捶着胸说:‘ 神啊,可怜我这个罪人!’
13Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14我告诉你们,这个人回去,比那个倒算为义了。因为高抬自己的,必要降卑;自己谦卑的,必要升高。”
14Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa."
15让小孩子到我这里来(太19:13-15;可10:13-16)有人抱着婴孩到耶稣面前,要他抚摩他们。门徒看见了,就责备那些人。
15Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16耶稣却叫他们过来,说:“让小孩子到我这里来,不要禁止他们,因为 神的国正属于这样的人。
16Lakini Yesu akawaita kwake akisema: "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17我实在告诉你们,凡不像小孩子一样接受 神的国的,决不能进去。”
17Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo."
18有钱的人难进 神的国(太19:16-29;可10:17-30)有一个官长问耶稣:“良善的老师,我当作什么,才可以承受永生?”
18Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, "Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?"
19耶稣对他说:“你为什么称我是良善的呢?除了 神一位以外,没有良善的。
19Yesu akamwambia, "Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20诫命你是知道的:不可奸淫,不可杀人,不可偷盗,不可作假证供,当孝敬父母。”
20Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako."
21他说:“这一切我从小都遵守了。”
21Yeye akasema, "Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu."
22耶稣听了,就告诉他:“你还缺少一件,应当变卖你一切所有的,分给穷人,你就必定有财宝在天上,而且你还要来跟从我。”
22Yesu aliposikia hayo akamwambia, "Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate."
23他听见这话,非常忧愁,因为他十分富有。
23Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24耶稣见他这样,就说:“富有的人要进 神的国,是多么难哪!
24Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, "Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25骆驼穿过针眼,比有钱的人进 神的国还容易呢。”
25Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."
26听见的人说:“这样,谁可以得救呢?”
26Wale watu waliposikia hayo, wakasema, "Nani basi, atakayeokolewa?"
27耶稣说:“人所不能的,在 神却是可能的。”
27Yesu akajibu, "Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu."
28彼得说:“你看,我们已舍弃自己所有的,跟从你了!”
28Naye Petro akamwuliza, "Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!"
29耶稣说:“我实在告诉你们,人为 神的国撇下房屋、妻子、弟兄、父母或儿女,
29Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30没有不在今世得许多倍,来世得永生的。”
30atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao."
31第三次预言受难及复活(太20:17-19;可10:32-34)耶稣把十二门徒带到一边,对他们说:“我们现在上耶路撒冷去,先知所写的一切,都要成就在人子身上。
31Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, "Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32他要被交给外族人,受戏弄,被凌辱,他们要向他吐唾沫,
32Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33鞭打他,杀害他;第三日他要复活。”
33Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka."
34这些话的含义对门徒是隐藏的。他们听了,一点也不明白,不知道他说的是什么。
34Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35治好瞎眼的人(太20:29-34;可10:46-52)耶稣走近耶利哥的时候,有一个瞎眼的人坐在路旁讨饭,
35Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36他听见人群经过,就问是什么事。
36Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, "Kuna nini?"
37别人告诉他,是拿撒勒人耶稣经过。
37Wakamwambia, "Yesu wa Nazareti anapita."
38他就喊叫说:“大卫的子孙耶稣啊,可怜我吧!”
38Naye akapaza sauti akisema, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"
39在前头走的人责备他,叫他不要出声;但他越发喊叫:“大卫的子孙,可怜我吧!”
39Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: "Mwana wa Daudi, nihurumie;"
40耶稣站住,吩咐领他过来。等他走近,就问他:
40Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41“你要我为你作什么?”他说:“主啊,叫我能看见!”
41"Unataka nikufanyie nini?" Naye akamjibu, "Bwana, naomba nipate kuona tena."
42耶稣说:“你就看见吧!你的信使你痊愈了。”
42Yesu akamwambia, "Ona! Imani yako imekuponya."
43他立刻看见了,就跟随耶稣,颂赞 神。众人看见这事,也赞美 神。
43Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.