1佃户的比喻(太21:33-46;路20:9-19)
1Yesu alianza kusema nao kwa mifano: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu. Akalizungushia ukuta, na katikati yake akachimba kisima cha kusindikia divai, akajenga mnara pia. Akalikodisha shamba hilo kwa wakulima, akasafiri hadi nchi ya mbali.
2到了时候,园主派了一个仆人到佃户那里,向佃户收取葡萄园一部分的果子。
2Wakati wa mavuno, alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima akamletee sehemu ya mazao ya shamba lake.
3佃户抓住他,打了他,放他空手回去。
3Wale wakulima wakamkamata, wakampiga, wakamrudisha mikono mitupu.
4园主再派另外一个仆人到他们那里,他们打伤了他的头,并且侮辱他。
4Akatuma tena mtumishi mwingine; huyu wakamuumiza kichwa na kumtendea vibaya.
5园主又派另一个去,他们就把他杀了。后来又派去许多仆人,有的给他们打了,有的给他们杀了。
5Mwenye shamba akatuma mtumishi mwingine tena, na huyo wakamuua. Wengine wengi waliotumwa, baadhi yao walipigwa, na wengi wakauawa.
6还有一个,就是园主的爱子,最后园主派他到那里去,说:‘他们必尊敬我的儿子。’
6Alibakiwa bado na mtu mmoja, yaani mwanawe mpendwa. Mwishowe akamtuma huyo akisema, Watamheshimu mwanangu.
7那些佃户却彼此说:‘这是继承产业的;来,我们杀了他,产业就是我们的了。’
7Lakini hao wakulima wakaambiana, Huyu ndiye mrithi, basi, tumuue ili urithi wake uwe wetu!
8于是抓住他,把他杀了,扔在葡萄园外。
8Kwa hiyo wakamkamata, wakamuua na kumtupa nje ya lile shamba la mizabibu.
9这样,葡萄园的主人要怎么办呢?他要来除掉那些佃户,把葡萄园租给别人。
9"Basi, mwenye shamba atafanya nini? Atakuja kuwaangamiza hao wakulima na kulikodisha hilo shamba la mizabibu kwa watu wengine.
10你们没有念过这段圣经吗:‘建筑工人所弃的石头,成了房角的主要石头;
10Je, hamjasoma Maandiko haya? Jiwe walilokataa waashi sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.
11这是主所作的,在我们眼中看为希奇。’”
11Bwana ndiye aliyefanya jambo hili, nalo ni la ajabu sana kwetu."
12他们知道他这比喻是针对他们说的,就想要捉拿他,但因为害怕群众,只好离开他走了。
12Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee walifahamu ya kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu. Kwa hiyo walijaribu kumtia nguvuni, lakini waliogopa umati wa watu. Basi, wakamwacha wakaenda zao.
13以纳税的事问难耶稣(太22:15-22;路20:19-26)后来,他们派了几个法利赛人和希律党的人到耶稣那里去,要找他的把柄来陷害他。
13Basi, baadhi ya Mafarisayo na wafuasi wa kikundi cha Herode walitumwa ili wamtege Yesu kwa maneno yake.
14他们来到了,就对他说:“老师,我们知道你为人诚实,不顾忌任何人,因为你不徇情面,只照着真理把 神的道教导人。请问纳税给凯撒可以不可以?我们该纳不该纳呢?”
14Wakamwendea, wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwaminifu unayesema ukweli mtupu, wala humjali mtu yeyote. Wala cheo cha mtu si kitu kwako, lakini wafundisha ukweli kuhusu njia ya Mungu. Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la? Tulipe au tusilipe?"
15耶稣看出他们的假意,就对他们说:“你们为什么试探我呢?拿一个银币来给我,让我看看。”
15Lakini Yesu alijua unafiki wao, akawaambia, "Mbona mnanijaribu? Nionyesheni sarafu."
16他们就拿来了。耶稣问他们:“这是谁的像,谁的名号?”他们回答他:“凯撒的。”
16Wakamwonyesha. Naye akawauliza, "Sura na chapa hii ni ya nani?" Wakamjibu, "Ni ya Kaisari."
17耶稣说:“凯撒的应当归给凯撒, 神的应当归给 神。”他们就对他十分惊奇。
17Basi, Yesu akawaambia, "Mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari na Mungu yaliyo yake Mungu." Wakashangazwa sana naye.
18人复活后不娶不嫁(太22:23-33;路20:27-38)撒都该人向来认为没有复活的事,他们来到耶稣那里,问他:
18Masadukayo wasemao kwamba hakuna ufufuo walimwendea Yesu, wakamwuliza,
19“老师,摩西曾写给我们说:‘如果一个人死了,留下妻子,没有儿女,他的弟弟就应当娶他的妻子,为哥哥立后。’
19"Mwalimu, Mose alituagiza hivi: Mtu akifa na kuacha mke bila mtoto, ndugu yake lazima amchukue huyo mama mjane amzalie watoto ndugu yake marehemu.
20从前有兄弟七人,头一个娶了妻子,死了,没有留下孩子;
20Basi, kulikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa, akafa bila kuacha mtoto.
21第二个娶了她,也没有留下孩子,就死了;第三个也是这样。
21Ndugu wa pili akamwoa huyo mjane, naye pia akafa bila kuacha mtoto; na ndugu watatu hali kadhalika.
22那七个人都没有留下孩子,最后那女人也死了。
22Wote saba walikufa bila kuacha mtoto. Mwishowe yule mama mjane naye akafa.
23到了复活的时候,他们都要复活,她是哪一个的妻子呢?因为七个人都娶过她。”
23Basi, siku watu watakapofufuka, mama huyo atakuwa mke wa nani? Maana wote saba walikuwa wamemwoa."
24耶稣对他们说:“你们错了,不正是因为你们不明白圣经,也不晓得 神的能力吗?
24Yesu akawaambia, "Ninyi mmekosea sana, kwa sababu hamjui Maandiko Matakatifu wala nguvu ya Mungu.
25因为人从死里复活以后,也不娶,也不嫁,而是像天上的天使一样。
25Maana wafu watakapofufuka, hawataoa wala kuolewa; watakuwa kama malaika wa mbinguni.
26关于死人复活的事,摩西的经卷中荆棘篇上, 神怎样对他说:‘我是亚伯拉罕的 神,以撒的 神,雅各的 神’,你们没有念过吗?
26Lakini kuhusu kufufuliwa kwa wafu, je, hamjasoma kitabu cha Mose katika sehemu inayohusu kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto? Mungu alimwambia Mose, Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.
27他不是死人的 神,而是活人的 神。你们是大错特错了!”
27Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai. Ninyi mmekosea sana!"
28最重要的诫命(太22:34-40;路10:25-28)有一个经学家,听到他们的辩论,觉得耶稣回答得好,就来问他:“诫命中哪一条是第一重要的呢?”
28Mmojawapo wa walimu wa Sheria alifika, akasikia mabishano yao. Alipoona kwamba Yesu aliwajibu vyema, akajitokeza akamwuliza, "Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza?"
29耶稣回答:“第一重要的是:‘以色列啊,你要听!主我们的 神是独一的主。
29Yesu akamjibu, "Ya kwanza ndiyo hii: Sikiliza, Israeli! Bwana Mungu wetu ndiye peke yake Bwana.
30你要全心、全性、全意、全力,爱主你的 神。’
30Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.
31其次是:‘要爱人如己。’再没有别的诫命比这两条更重要的了。”
31Na ya pili ndiyo hii: Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi."
32那经学家对耶稣说:“老师,是的,你说的很对, 神是独一的,除了他以外再没有别的 神。
32Basi, yule mwalimu wa Sheria akamwambia, "Vyema Mwalimu! Umesema kweli kwamba Mungu ni mmoja tu wala hakuna mwingine ila yeye.
33我们要用全心、全意、全力去爱他,并且要爱人如己,这就比一切燔祭和各样祭物好得多了。”
33Na ni lazima mtu kumpenda Mungu kwa moyo wote, kwa akili yote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani yake kama anavyojipenda mwenyewe. Jambo hili ni muhimu zaidi kuliko dhabihu na sadaka zote za kuteketezwa."
34耶稣见他回答得有智慧,就对他说:“你距离 神的国不远了。”从此再也没有人敢问他了。
34Yesu alipoona kwamba huyu mtu alimjibu kwa ujasiri, akamwambia, "Wewe huko mbali na Ufalme wa Mungu." Baada ya hayo, hakuna mtu aliyethubutu tena kumwuliza kitu.
35大卫称基督为主(太22:41-46;路20:41-44)耶稣在殿里教训人,说:“经学家怎么说基督是大卫的子孙呢?
35Wakati Yesu alipokuwa akifundisha Hekaluni, aliuliza, "Mbona walimu wa Sheria wanasema ya kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
36大卫自己被圣灵感动却说:‘主对我的主说:你坐在我的右边,等我把你的仇敌放在你的脚下(有些抄本作“等我使你的仇敌作你的脚凳”)。’
36Daudi mwenyewe akiongozwa na Roho Mtakatifu alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia, Mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako."
37大卫自己既然称他为主,他又怎么会是大卫的子孙呢?”群众都喜欢听他。
37"Daudi mwenyewe anamwita Kristo Bwana. Basi, Kristo atakuwaje mwanae?" Umati wa watu ulikuwa ukimsikiliza kwa furaha.
38耶稣叫人提防经学家(太23:1-7;路20:45-47)耶稣教导人的时候,说:“你们要提防经学家,他们喜欢穿长袍走来走去,喜欢人在市中心向他们问安,
38Katika mafundisho yake, Yesu alisema, "Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamejivalia kanzu ndefu na kusalimiwa na watu kwa heshima sokoni; hupenda kuketi mahali pa heshima katika masunagogi,
39又喜欢会堂里的高位,筵席上的首座。
39na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
40他们吞没了寡妇的房产,又假装作冗长的祷告。这些人必受更重的刑罚。”
40Huwanyonya wajane huku wakijisingizia kusali sala ndefu. Siku ya hukumu watapata adhabu kali!"
41穷寡妇的奉献(路21:1-4)耶稣面对银库坐着,看着大家怎样把钱投入库中。许多有钱的人投入很多的钱。
41Yesu alikuwa ameketi karibu na sanduku la hazina. Akawa anatazama jinsi watu wengi walivyokuwa wakitoa fedha na kuzitia katika hazina ya Hekalu. Matajiri wengi walitoa fedha nyingi.
42后来,有一个穷寡妇来投入了两个小钱,就是一个铜钱。
42Hapo akaja mama mmoja mjane maskini, akatoa sarafu mbili ndogo za fedha.
43耶稣把门徒叫过来,对他们说:“我实在告诉你们,这穷寡妇投入库里的,比众人投的更多。
43Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, "Kweli nawaambieni, huyu mama mjane maskini ametoa zaidi kuliko wengine wote waliotia fedha katika sanduku la hazina.
44因为他们都是把自己剩余的投入,这寡妇是自己不足,却把她一切所有的,就是全部养生的,都投进去了。”
44Maana wote walitoa kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa yote aliyokuwa nayo, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi."