聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Mark

15

1耶稣被押交彼拉多(太27:1-2、11-14;路23:1-3;约18:29-37)
1Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
2彼拉多问他:“你是犹太人的王吗?”耶稣回答:“你说的是。”
2Pilato akamwuliza Yesu, "Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?" Yesu akajibu, "Wewe umesema."
3祭司长控告了他许多事。
3Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4彼拉多又问他:“你看,他们控告你这么多的事!你什么都不回答吗?”
4Pilato akamwuliza tena Yesu, "Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako."
5耶稣还是一言不答,使彼拉多非常惊奇。
5Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
6彼拉多判耶稣钉十字架(太27:15-26;路23:13-25;约18:38-19:16)每逢这节期,彼拉多按着众人所要求的,照例给他们释放一个囚犯。
6Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7有一个人名叫巴拉巴,和作乱的人囚禁在一起,他们作乱的时候,曾杀过人。
7Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8群众上去,要求彼拉多援例给他们办理。
8Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
9彼拉多回答他们:“你们要我给你们释放这个犹太人的王吗?”
9Pilato akawauliza, "Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?"
10他知道祭司长是因为嫉妒才把耶稣交了来。
10Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11祭司长却煽动群众,宁可要总督释放巴拉巴给他们。
11Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12彼拉多又对他们说:“那么,你们称为犹太人的王的,你们要我怎样处置他呢?”
12Pilato akawauliza tena, "Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?"
13他们就喊着说:“把他钉十字架!”
13Watu wote wakapaaza sauti tena: "Msulubishe!"
14彼拉多说:“他作了什么恶事呢?”众人却更加大声喊叫:“把他钉十字架!”
14Lakini Pilato akawauliza, "Kwa nini! Amefanya kosa gani?" Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, "Msulubishe!"
15彼拉多有意讨好群众,就释放了巴拉巴给他们,把耶稣鞭打了,交给他们钉十字架。
15Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
16士兵戏弄耶稣(太27:27-31)士兵把耶稣带进总督府的院子里,召集了全队士兵。
16Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17他们给他披上紫色的外袍,又用荆棘编成冠冕给他戴上;
17Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
18就向他祝贺说:“犹太人的王万岁!”
18Wakaanza kumsalimu, "Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!"
19又用一根芦苇打他的头,向他吐唾沫,并且跪下来拜他。
19Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
20他们戏弄完了,就把他的紫色的外袍脱下,给他穿回自己的衣服,带他出去,要钉十字架。
20Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
21耶稣被钉十字架(太27:32-44;路23:26-43;约19:17-24)有一个古利奈人西门,就是亚历山大和鲁孚的父亲,从乡下来到,经过那里,士兵就强迫他背着耶稣的十字架。
21Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
22他们把耶稣带到各各他地方(这地名译出来就是“髑髅地”),
22Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la Kichwa."
23拿没药调和的酒给他,他却不接受。
23Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
24他们就把他钉了十字架;又抽签分他的衣服,看谁得着什么。
24Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25他们钉他十字架的时候,是在上午九点钟。
25Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26耶稣的罪状牌上写着“犹太人的王”。
26Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: "Mfalme wa Wayahudi."
27他们又把两个强盗和他一同钉十字架,一个在右,一个在左。
27Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
28(有些抄本有第28节:“这就应验了经上所说的:‘他和不法者同列。’”)
28Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, "Aliwekwa kundi moja na waovu."
29过路的人讥笑他,摇着头说:“哼,你这个要拆毁圣所,三日之内又把它建造起来的,
29Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, "Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
30从十字架上把自己救下来吧!”
30Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!"
31祭司长和经学家也同样讥笑他,彼此说:“他救了别人,却不能救自己;
31Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, "Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
32以色列的王基督啊,现在可以从十字架上下来,让我们看见就信吧。”那和他同钉十字架的人也侮辱他。
32Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini." Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
33耶稣死时的情形(太27:45-56;路23:44-49;约19:28-30)从正午到下午三点钟,遍地都黑暗了。
33Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
34下午三点的时候,耶稣大声呼号:“以罗伊,以罗伊,拉马撒巴各大尼?”这句话译出来就是:“我的 神,我的 神,你为什么离弃我?”
34Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eloi, Eloi, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
35有些站在旁边的人听见了就说:“看,他呼叫以利亚呢。”
35Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, "Sikiliza! Anamwita Eliya!"
36有一个人跑去拿海绵浸满了酸酒,绑在芦苇上,递给他喝,说:“等一等,我们看看以利亚来不来救他。”
36Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, "Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!"
37耶稣大叫一声,气就断了。
37Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
38圣所里的幔子,从上到下裂成两半。
38Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
39站在他对面的百夫长,看见他这样断气,就说:“这人真是 神的儿子!”
39Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, "Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!"
40也有些妇女远远地观看,她们之中有抹大拉的马利亚,小雅各和约西的母亲马利亚,以及撒罗米。
40Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
41这些妇女,当耶稣在加利利的时候,就一直跟随他、服事他。此外,还有许多和他一同上耶路撒冷的妇女。
41Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
42耶稣葬在坟墓里(太27:57-61;路23:50-56;约19:38-42)到了晚上,因为是预备日,就是安息日的前一日,
42Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
43一个一向等候 神国度的尊贵的议员,亚利马太的约瑟来了,就放胆地进去见彼拉多,求领耶稣的身体。
43Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
44彼拉多惊讶耶稣已经死了,就叫百夫长前来,问他耶稣是不是死了很久。
44Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
45他从百夫长知道了实情以后,就把尸体给了约瑟。
45Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
46约瑟买了细麻布,把耶稣取下,用细麻布裹好,安放在一个从磐石凿出来的坟墓里,又辊过一块石头来挡住墓门。
46Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
47抹大拉的马利亚和约西的母亲马利亚都看见安放他的地方。
47Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.