聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Mark

16

1耶稣复活(太28:1-8;路24:1-10;约20:1-10)
1Baada ya siku ya Sabato, Maria Magdalene, Salome na Maria mama yake Yakobo walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu.
2礼拜日的大清早,出太阳的时候,她们就来到坟墓那里,
2Basi, alfajiri na mapema siku ya Jumapili, jua lilipoanza kuchomoza, walienda kaburini.
3彼此说:“谁可以给我们辊开墓门的石头呢?”
3Nao wakawa wanaambiana, "Nani atakayetuondolea lile jiwe mlangoni mwa kaburi?"
4原来那块石头非常大,她们抬头一看,却见石头已经辊开了。
4Lakini walipotazama, waliona jiwe limekwisha ondolewa. (Nalo lilikuwa kubwa mno.)
5她们进了坟墓,看见一位身穿白袍的青年,坐在右边,就非常惊恐。
5Walipoingia kaburini, walimwona kijana mmoja aliyevaa vazi jeupe, ameketi upande wa kulia; wakashangaa sana.
6那青年对她们说:“不要惊慌!你们寻找那钉十字架的拿撒勒人耶稣,他不在这里,已经复活了;请看他们安放他的地方。
6Lakini huyo kijana akawaambia, "Msishangae. Mnamtafuta Yesu wa Nazareti aliyesulubiwa. Amefufuka, hayumo hapa. Tazameni mahali walipokuwa wamemlaza.
7你们去告诉他的门徒和彼得:他要比你们先到加利利去,你们在那里必定看见他,正如他从前告诉你们的。”
7Nendeni mkawaambie wanafunzi wake pamoja na Petro ya kwamba anawatangulieni kule Galilaya. Huko mtamwona kama alivyowaambieni."
8因为惊恐战栗,她们一从坟墓出来就逃跑;由于害怕,她们什么也没有告诉人。(有些抄本无第9至20节)
8Basi, wakatoka pale kaburini mbio, maana walitetemeka kwa hofu na kushangaa. Hawakumwambia mtu yeyote kitu, kwa sababu waliogopa mno.
9主向抹大拉的马利亚显现(约20:11-18)礼拜日的清早,耶稣复活了,先向抹大拉的马利亚显现,耶稣曾经从她身上赶出七个鬼。
9Yesu alipofufuka mapema Jumapili, alijionyesha kwanza kwa Maria Magdalene, ambaye Yesu alikuwa amemtoa pepo saba.
10她就去告诉那些向来和耶稣在一起的人,那时他们正在悲哀哭泣。
10Maria Magdalene akaenda, akawajulisha wale waliokuwa pamoja na Yesu, na wakati huo walikuwa wanaomboleza na kulia.
11他们听见耶稣活了,又被马利亚看见了,却不相信。
11Lakini waliposikia ya kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria Magdalene amemwona, hawakuamini.
12向两个门徒显现(路24:13-35)这事以后,门徒中有两个人往乡下去,正走路的时候,耶稣用另外的形象,向他们显现,
12Baadaye Yesu aliwatokea wanafunzi wawili akiwa na sura nyingine. Wanafunzi hao walikuwa wanakwenda shambani.
13他们就去告诉其他的人,那些人也不相信。
13Nao pia wakaenda wakawaambia wenzao. Hata hivyo hawakuamini.
14吩咐门徒往普天下传福音(太28:16-20;路24:36-49;约20:19-23;徒1:6-8)后来,十一个门徒吃饭的时候,耶稣向他们显现,责备他们的不信和心硬,因为他们不信那些在他复活以后见过他的人。
14Mwishowe, Yesu aliwatokea wanafunzi kumi na mmoja walipokuwa pamoja mezani. Akawakemea sana kwa sababu ya kutoamini kwao na ukaidi wao, maana hawakuwaamini wale waliokuwa wamemwona baada ya kufufuka.
15他又对他们说:“你们到全世界去,向所有的人传福音。
15Basi, akawaambia, "Nendeni ulimwenguni kote mkahubiri Habari Njema kwa kila mtu.
16信而受洗的必定得救,不信的必被定罪。
16Anayeamini na kubatizwa ataokolewa; asiyeamini atahukumiwa.
17信的人必有神迹随着他们,就是奉我的名赶鬼,用新方言说话,
17Na ishara hizi zitaandamana na wale wanaoamini: kwa jina langu watatoa pepo na watasema kwa lugha mpya.
18用手握蛇,喝了什么毒物也不受害,手按病人就必好了。”
18Wakishika nyoka au wakinywa kitu chochote chenye sumu, hakitawadhuru. Watawawekea wagonjwa mikono, nao watapona."
19耶稣升天(路24:50-53;徒1:9-11)主耶稣向门徒讲完了话,就被接到天上,坐在 神的右边。
19Basi, Bwana Yesu alipokwisha sema nao, akachukuliwa mbinguni, akaketi upande wa kulia wa Mungu.
20门徒出去,到处传扬福音,主和他们同工,借着相随的神迹,证实所传的道。(有少数抄本有〔较短的结语〕:9“那些妇女把耶稣所吩咐的一切都告诉彼得和他的同伴。10这些事以后,耶稣借着他们亲自把那神圣不朽、永远救恩的信息从东到西传扬出去。阿们。”放在第8节之后;另有少数抄本把它放在第20节之后。)
20Wanafunzi wakaenda wakihubiri kila mahali. Bwana akafanya kazi pamoja nao na kuimarisha ujumbe huo kwa ishara zilizoandamana nao.