聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Mark

4

1撒种的比喻(太13:1-9;路8:4-8)
1Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
2他用比喻教训他们许多事,在教训中他说:
2Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
3“你们听着!有一个撒种的出去撒种,
3"Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4撒的时候,有的落在路旁,小鸟飞来就吃掉了。
4Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5有的落在泥土不多的石地上,因为泥土不深,很快就长起来。
5Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6但太阳一出来,就把它晒干,又因为没有根就枯萎了。
6Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7有的落在荆棘里,荆棘长起来,把它挤住,它就结不出果实来。
7Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
8有的落在好土里,就生长繁茂,结出果实,有三十倍的、有六十倍的、有一百倍的。”
8Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia."
9耶稣又说:“有耳可听的,就应当听。”
9Kisha akawaambia, "Mwenye masikio na asikie!"
10用比喻的目的(太13:10-17;路8:9-10)耶稣独自一人的时候,那些经常跟着他的人和十二门徒,来问这些比喻的意义。
10Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
11耶稣对他们说:“ 神的国的奥秘,只给你们知道,但对于外人,一切都用比喻,
11Naye akawaambia, "Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
12叫他们‘看是看见了,却不领悟,听是听见了,却不明白,免得他们回转过来,得到赦免。’”
12ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe."
13解释撒种的比喻(太13:18-23;路8:11-15)耶稣又对他们说:“你们不明白这个比喻,怎能明白一切比喻呢?
13Basi, Yesu akawauliza, "Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
14撒种的人所撒的就是道。
14Mpanzi hupanda neno la Mungu.
15那撒在路旁的,就是人听了道,撒但立刻来,把撒在他心里的道夺去。
15Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
16照样,那撒在石地上的,就是人听了道,立刻欢欢喜喜地接受了;
16Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
17可是他们里面没有根,只是暂时的;一旦为道遭遇患难,受到迫害,就立刻跌倒了。
17Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
18那撒在荆棘里的,是指另一些人;他们听了道,
18Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
19然而今世的忧虑、财富的迷惑,以及种种的欲望,接连进来,把道挤住,就结不出果实来。
19lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda.
20那撒在好土里的,就是人听了道,接受了,并且结出果实,有三十倍的、有六十倍的、有一百倍的。”
20Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja."
21隐藏的事终必显露(路8:16-18)耶稣又对他们说:“灯难道是拿来放在量器底下或床底下的吗?它不是该放在灯台上吗?
21Yesu akaendelea kuwaambia, "Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
22因为没有什么隐藏的事不被显明出来,没有什么掩盖的事不被揭露的。
22Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
23有耳可听的,就应当听。”
23Mwenye masikio na asikie!"
24耶稣又对他们说:“要留心你们所听到的,你们用什么尺度量给人, 神也要用什么尺度量给你们,并且要超过尺度给你们。
24Akawaambia pia, "Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
25因为那有的,还要给他;那没有的,就算他有什么也要拿去。”
25Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa."
26种子发芽生长的比喻耶稣说:“ 神的国好像人在地里撒种,
26Yesu akaendelea kusema, "Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
27他夜里睡觉,白天起来,种子发芽生长,自己也不知道怎么会这样的。
27Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
28地生五谷是自然的,先长苗,后吐穗,最后穗上结满了子粒。
28Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
29庄稼熟了,就派人用镰刀割下,因为收成的时候到了。”
29Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika."
30芥菜种的比喻(太13:31-35;路13:18-19)又说:“我们要把 神的国比作什么呢?我们可以用什么比喻来形容它呢?
30Tena, Yesu akasema, "Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
31它好像一粒芥菜种,刚种下去的时候,比地上的一切种子都小,
31Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
32种下以后,生长起来,却比一切蔬菜都大,长出大枝子,甚至天空的飞鸟都可以在它的荫下搭窝。”
32Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake."
33耶稣用许多这样的比喻,照着他们所能听懂的,向他们讲道;
33Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
34不用比喻,就不对他们讲。只有单独和自己的门徒在一起的时候,才把一切解释给他们听。
34Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
35平静风浪(太8:18、23-27;路8:22-25)当天黄昏,耶稣对门徒说:“我们渡到海那边去吧。”
35Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, "Tuvuke ziwa, twende ng'ambo."
36门徒离开群众,耶稣已经在船上,他们就载他过去,也有别的船和他同去。
36Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
37忽然起了狂风,波浪不断地打进船来,舱里积满了水。
37Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
38耶稣却在船尾靠着枕头睡着了。门徒把他叫醒,对他说:“老师,我们要死了,你不管吗?”
38Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, "Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?"
39耶稣起来,斥责了风,又对海说:“不要作声!安静吧!”风就停止,大大地平静了。
39Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, "Kimya! Tulia!" Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
40然后对他们说:“为什么这样胆怯呢?你们怎么没有信心呢?”
40Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?"
41门徒非常惧怕,彼此说:“这到底是谁,连风和海都听从他?”
41Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, "Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?"