聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Mark

5

1治好鬼附的格拉森人(太8:28-34;路8:26-39)
1Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
2耶稣一下船,就有一个被污灵附着的人,从墓地里迎面而来。
2Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
3那人经常住在坟墓中间,从来没有人能绑住他,甚至用锁链都不能。
3Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
4曾经有很多次,人用脚镣和锁链捆绑他,锁链却被他挣断,脚镣也被他弄碎,始终没有人能制伏他。
4Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
5他昼夜在坟墓里和山野间喊叫,又用石头砍自己。
5Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
6他远远地看见耶稣,就跑过去拜他,
6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
7大声呼叫,说:“至高 神的儿子耶稣,我跟你有什么关系呢?我指着 神恳求你,不要叫我受苦。”
7akisema kwa sauti kubwa, "Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!"
8因为当时耶稣吩咐他:“你这污灵,从这人身上出来!”
8(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, "Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.")
9耶稣问他:“你叫什么名字?”他回答:“我名叫‘群’,因为我们众多。”
9Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Naye akajibu, "Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi."
10他再三央求耶稣,不要把他们从那地方赶走。
10Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
11附近的山坡上有一大群猪正在吃东西;
11Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
12污灵求耶稣说:“打发我们到猪群那里附在猪身上吧。”
12Basi, hao pepo wakamsihi, "Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie."
13耶稣准了他们。污灵就出来,进到猪群里去,于是那群猪闯下山崖,掉在海里淹死了,猪的数目约有两千。
13Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
14放猪的人都逃跑了,到城里和各乡村去报告,大家就来看发生了什么事。
14Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
15他们来到耶稣跟前,看见那被鬼附过的人,就是曾被名叫‘群’的鬼附过的人,坐在那里,穿上了衣服,神志清醒,他们就害怕。
15Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
16看见的人把被鬼附过的人所遭遇的和那群猪的事,告诉了他们。
16Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
17他们就要求耶稣离开他们的地区。
17Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
18耶稣上船的时候,那被鬼附过的人来求他,要和他在一起。
18Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
19耶稣不许,却对他说:“你回家到你的亲属那里去,把主为你作了多么大的事,并他怎样怜悯你,都告诉他们。”
19Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, "Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma."
20那人就走了,开始在低加波利传讲耶稣为他所作的大事,众人都希奇。
20Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
21治好血漏病的女人(太9:18-26;路8:40-56)耶稣又坐船渡到那边;还在海边的时候,有一大群人向他围拢过来。
21Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
22当时来了一位会堂的主管,名叫叶鲁。他一看见耶稣,就俯伏在他脚前,
22Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
23迫切地求他说:“我的小女儿快要死了,请你来按手在她身上,把她救活。”
23akamsihi akisema, "Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi."
24耶稣就和他一起去了。一大群人跟着他,拥挤着他。
24Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
25有一个女人,患了十二年的血漏病,
25Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26在好些医生手中受了许多痛苦,又花尽了她一切所有的,不仅毫无起色,反而更加沉重。
26Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27她听见耶稣的事,就从后面来杂在人群中间,摸耶稣的衣服。
27Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
28因为她说:“只要摸到他的衣服,我就必痊愈。”
28Alifanya hivyo, maana alijisemea, "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
29于是她血漏的源头立刻干了,她在身体上感觉到病已经得了医治。
29Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
30耶稣自己立刻觉得有能力从他里面出去,就转过身来对群众说:“谁摸了我的衣服?”
30Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, "Nani aliyegusa mavazi yangu?"
31门徒对他说:“你看,这么多人拥挤你,你还问‘谁摸我’吗?”
31Wanafunzi wake wakamjibu, "Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?"
32耶稣周围观看,要看作这事的女人。
32Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
33那女人知道在她身上所成就的事,就恐惧战兢地前来向耶稣俯伏,把实情全告诉了他。
33Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
34耶稣对她说:“女儿,你的信使你痊愈了,平安地回去吧,你的病已经好了。”
34Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako."
35使女孩复活耶稣还在说话的时候,有人从会堂主管的家里来说:“你的女儿已经死了,何必还劳动老师呢?”
35Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, "Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?"
36耶稣听见所说的话,就对会堂主管说:“不要怕!只要信!”
36Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, "Usiogope, amini tu."
37于是他不许别人跟他一起去,只带了彼得、雅各和雅各的弟弟约翰。
37Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
38他们来到会堂主管的家,耶稣看见许多人哭泣哀号,一片混乱,
38Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
39就走进去,对众人说:“为什么大哭大嚷呢?孩子不是死了,是睡着了。”
39Akaingia ndani, akawaambia, "Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu."
40众人就嘲笑他。耶稣把众人都赶出去,带着孩子的父母和跟随他的门徒,进入孩子所在的房间。
40Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
41耶稣拉着孩子的手,对她说:“大利大,古米!”翻译出来就是:“小女孩,我吩咐你起来!”
41Kisha akamshika mkono, akamwambia, "Talitha, kumi," maana yake, "Msichana, nakwambia, amka!"
42那女孩子就立刻起来行走;那时她已经十二岁了。众人就非常惊奇。
42Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
43耶稣再三嘱咐他们,不要让人知道这事,又吩咐给她东西吃。
43Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.