1耶稣在本乡遭人厌弃(太13:53-58;路4:16-30)
1Yesu aliondoka hapo akaenda katika kijiji chake, akifuatwa na wanafunzi wake.
2到了安息日,他开始在会堂里教导人;很多人听见了,都惊奇地说:“这个人从哪里得来这一切呢?所赐给他的是怎么样的智慧,竟然借着他的手行出这样的神迹?
2Siku ya Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika sunagogi. Wengi waliomsikia walishangaa, wakasema, "Je, ameyapata wapi mambo haya? Ni hekima gani hii aliyopewa? Tena, anatendaje maajabu haya anayoyafanya?
3这不是那木匠吗?不是马利亚的儿子,雅各、约西、犹大、西门的哥哥吗?他的妹妹们不也在我们这里吗?”他们就厌弃耶稣。
3Je, huyu si yule seremala mwana wa Maria, na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simoni; Je, dada zake si wanaishi papa hapa kwetu?" Basi, wakawa na mashaka naye.
4耶稣对他们说:“先知除了在自己的本乡、本族、本家之外,没有不受人尊敬的。”
4Yesu akawaambia, "Nabii hakosi heshima isipokuwa katika nchi yake, kwa jamaa zake na nyumbani mwake."
5耶稣不能在那里行什么神迹,只给几个病人按手,医好了他们。
5Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache, akawaponya.
6对于那些人的不信,他感到诧异。耶稣到周围的乡村去继续教导人。
6Alishangaa sana kwa sababu ya kutoamini kwao. Kisha Yesu alivitembelea vijiji vya pale karibu akiwafundisha watu.
7差遣十二使徒(太10:1-14;路9:1-6)他把十二门徒叫来,差遣他们两个两个地出去,赐给他们胜过污灵的权柄;
7Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawiliwawili. Aliwapa uwezo wa kuwatoa pepo wachafu,
8吩咐他们说:“除了手杖以外,路上什么都不要带,不要带干粮,不要带口袋,腰袋里也不要带钱,
8na kuwaamuru, "Msichukue chochote mnapokwenda isipokuwa fimbo tu. Msichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni.
9只穿一双鞋,不要穿两件衣服。”
9Vaeni viatu lakini msivae kanzu mbili."
10又对他们说:“你们无论到哪里,进了一家就住在那家,直到离开那个地方。
10Tena aliwaambia, "Popote mtakapokaribishwa nyumbani, kaeni humo mpaka mtakapoondoka mahali hapo.
11什么地方不接待你们,不听你们,你们离开那地方的时候,就要把脚上的灰尘跺下去,作为反对他们的见证。”
11Mahali popote ambapo watu watakataa kuwakaribisheni au kuwasikiliza, ondokeni hapo na kuyakung'uta mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao."
12门徒就出去传道,叫人悔改,
12Basi, wakaondoka, wakahubiri watu watubu.
13赶出许多鬼,用油抹了许多病人,医好他们。
13Waliwafukuza pepo wengi wabaya; wakawapaka mafuta wagonjwa wengi, wakawaponya.
14施洗约翰被杀(太14:1-12;路9:7-9)当时耶稣的名声传扬出去,希律王也听到了。有人说:“施洗的约翰从死人中复活了,所以他身上有行神迹的能力。”
14Basi, mfalme Herode alisikia juu ya hayo yote, maana sifa za Yesu zilienea kila mahali. Baadhi ya watu walikuwa wakisema, "Yohane Mbatizaji amefufuka kutoka wafu, ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
15又有人说:“他是以利亚。”还有人说:“他是先知,像古时先知中的一位。”
15Wengine walisema, "Mtu huyu ni Eliya." Wengine walisema, "Huyu ni nabii kama mmojawapo wa manabii wa kale."
16希律听见就说:“是约翰,我砍了他的头,他又活了!”
16Lakini Herode alipopata habari hizi alisema, "Huyu ni Yohane! Nilimkata kichwa, lakini amefufuka."
17原来希律曾亲自派人去捉拿约翰,把他捆锁在监里。他这样作,是为了他弟弟的妻子希罗底的缘故,因为他娶了希罗底为妻,
17Hapo awali Herode mwenyewe alikuwa ameamuru Yohane atiwe nguvuni, akamfunga gerezani. Herode alifanya hivyo kwa sababu ya Herodia ambaye Herode alimwoa ingawaje alikuwa mke wa Filipo, ndugu yake.
18而约翰曾对希律说:“你占有你兄弟的妻子是不合理的。”
18Yohane alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kumchukua mke wa ndugu yako."
19于是希罗底怀恨在心,想要杀他,只是不能。
19Basi Herodia alimchukia sana Yohane, akataka kumwua, asiweze.
20因为希律惧怕约翰,知道他是公义圣洁的人,就保护他。希律听了约翰的话,就非常困扰,却仍然喜欢听他。
20Herode alimwogopa Yohane kwa maana alijua kwamba yeye ni mtu mwema na mtakatifu, na hivyo akamlinda. Herode alipenda kumsikiliza Yohane, ingawaje baada ya kumsikiliza, alifadhaika sana.
21有一天,机会来了。在希律生日的那一天,他为大臣、千夫长和加利利的要人摆设了筵席。
21Ikapatikana nafasi, wakati wa sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode. Herode aliwafanyia karamu wazee wa baraza lake, majemadari na viongozi wa Galilaya.
22希罗底的女儿进来跳舞,使希律和在座的宾客都很开心。王就对女孩子说:“你无论想要什么,只管向我求,我一定给你!”
22Basi, binti yake Herodia aliingia, akacheza, akawafurahisha sana Herode na wageni wake. Mfalme akamwambia huyo msichana, "Niombe chochote utakacho, nami nitakupa."
23并且对她再三起誓:“你无论向我求什么,就是我国的一半,我也一定给你!”
23Tena akamwapia, "Chochote utakachoniomba, nitakupa: hata ikiwa ni nusu ya ufalme wangu."
24于是她出去问母亲:“我该求什么呢?”希罗底告诉她:“施洗的约翰的头!”
24Hapo huyo msichana akatoka, akamwuliza mama yake, "Niombe nini?" Naye akamjibu, "Kichwa cha Yohane mbatizaji."
25她急忙到王面前,向王要求说:“愿王立刻把施洗的约翰的头放在盘子上给我!”
25Msichana akamrudia mfalme mbio akamwomba, "Nataka unipe sasa hivi katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
26希律王非常忧愁,但是因为他的誓言和在座的宾客,就不愿拒绝她。
26Mfalme akahuzunika sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake, na kwa ajili ya wale wageni wake karamuni, hakutaka kumkatalia.
27希律王立刻差遣一个侍卫,吩咐把约翰的头拿来。侍卫就去了,在监里斩了约翰的头,
27Basi, mfalme akamwamuru askari kukileta kichwa cha Yohane. Askari akaenda, akamkata kichwa Yohane mle gerezani,
28把头放在盘子上,拿来交给那女孩子,女孩子又交给她的母亲。
28akakileta katika sinia, akampa msichana naye msichana akampa mama yake.
29约翰的门徒听见了,就来把他的尸体领去,安放在坟墓里。
29Wanafunzi wa Yohane walipopata habari, walikwenda wakachukua mwili wake, wakauzika kaburini.
30给五千人吃饱的神迹(太14:13-21;路9:10-17;约6:1-13。参可8:1-9)使徒们回来聚集在耶稣跟前,把他们所作和所教导的一切都报告给他听。
30Wale mitume walirudi, wakakusanyika mbele ya Yesu wakamwarifu yote waliyotenda na kufundisha.
31耶稣对他们说:“来,你们自己到旷野去休息一下。”因为来往的人多,他们甚至没有时间吃饭。
31Alisema hivyo kwa kuwa kulikuwa na watu wengi mno walikuwa wanafika hapo na kuondoka hata Yesu na wanafunzi wake hawakuweza kupata nafasi ya kula chakula. Basi, Yesu akawaambia, "Twendeni peke yetu mahali pa faragha kula chakula, mkapumzike kidogo."
32他们就悄悄地上了船,到旷野去了。
32Basi, Wakaondoka peke yao kwa mashua, wakaenda mahali pa faragha.
33群众看见他们走了,有许多人认出了他们,就从各城出来,跑到那里,比他们先赶到。
33Lakini watu wengi waliwaona wakienda, wakawatambua. Hivyo wengi wakatoka katika kila mji, wakakimbilia huko Yesu na wanafunzi wake walikokuwa wanakwenda, wakawatangulia kufika.
34耶稣一下船,看见一大群人,就怜悯他们,因为他们好像羊没有牧人一样,就开始教导他们许多事。
34Waliposhuka pwani, Yesu aliona umati mkubwa wa watu, akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji. Akaanza kuwafundisha mambo mengi.
35天晚了,门徒前来对他说:“这里是旷野的地方,天已经很晚了,
35Saa za mchana zilikwisha pita. Basi, wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwambia, "Hapa ni nyikani, na sasa kunakuchwa.
36请叫他们散开,好让他们往周围的田舍村庄去,自己买点东西吃。”
36Afadhali uwaage watu waende mashambani na katika vijiji vya jirani, wanunue chakula."
37耶稣回答他们:“你们给他们吃吧!”门徒说:“要我们去买两百银币的饼给他们吃吗?”
37Lakini Yesu akawaambia, "Wapeni ninyi chakula." Nao wakamwuliza, "Je, twende kununua mikate kwa fedha dinari mia mbili, na kuwapa chakula?"
38耶稣说:“去看看你们有多少饼!”他们知道了,就说:“五个饼,还有两条鱼。”
38Yesu akawauliza, "Mnayo mikate mingapi? Nendeni mkatazame." Walipokwisha tazama, wakamwambia, "Kuna mikate mitano na samaki wawili."
39耶稣吩咐他们叫大家分组坐在青草地上。
39Basi, Yesu akawaamuru wanafunzi wawaketishe watu wote makundimakundi penye nyasi.
40他们就一排一排地坐了下来,有一百的,有五十的。
40Nao wakaketi makundimakundi ya watu mia moja na ya watu hamsini.
41耶稣拿起这五个饼、两条鱼,望着天,祝谢了;然后把饼擘开,递给门徒摆在群众面前,又把两条鱼也分给群众。
41Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu, akaimega mikate, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu. Na wale samaki wawili pia akawagawia wote.
42大家都吃了,并且吃饱了。
42Watu wote wakala, wakashiba.
43他们把剩下的零碎捡起来,装满了十二个篮子,
43Wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
44吃饼的人,男人就有五千。
44Nao waliokula hiyo mikate walikuwa wanaume elfu tano.
45耶稣在海面上行走(太14:22-33;约6:15-21)事后耶稣立刻催门徒上船,叫他们先渡到对岸的伯赛大去,等他自己叫众人散开。
45Mara Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie kwenda Bethsaida, ng'ambo ya ziwa, wakati yeye anauaga umati wa watu.
46他离开了他们,就上山去祷告。
46Baada ya kuwaaga watu alikwenda mlimani kusali.
47到了晚上,船在海中,耶稣独自在岸上,
47Ilipokuwa jioni, mashua ilikuwa katikati ya ziwa, naye alikuwa peke yake katika nchi kavu.
48看见门徒辛辛苦苦地摇橹,因为风不顺。天快亮的时候(“天快亮的时候”原文作“夜里四更天”),耶稣在海面上向他们走去,想要赶过他们。
48Basi, akawaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kupiga makasia, maana upepo ulikuwa unawapinga. Karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea akitembea juu ya maji. Alitaka kuwapita.
49门徒看见他在海面上走,以为是鬼怪,就喊叫起来;
49Lakini walimwona akitembea juu ya maji, wakadhani ni mzimu, wakapiga yowe.
50因为他们都看见了他,非常恐惧。耶稣立刻对他们说:“放心吧!是我,不要怕。”
50Maana wote walipomwona waliogopa sana. Mara Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
51于是上了船,和他们在一起,风就平静了。门徒心里十分惊奇,
51Kisha akapanda mashuani walimokuwa, na upepo ukatulia. Nao wakashangaa sana.
52因为他们还不明白分饼这件事的意义,他们的心还是迟钝。
52maana hawakuwa bado wameelewa maana ya ile mikate. Akili zao zilikuwa bado zimepumbazika.
53治好革尼撒勒的病人(太14:34-36)他们渡过了海,就在革尼撒勒靠岸,
53Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti, wakatia nanga.
54一下船,众人立刻认出耶稣来,
54Walipotoka mashuani, mara watu wakamtambua Yesu.
55就跑遍那一带地方,把有病的人放在褥子上,听见他在哪里,就抬到哪里。
55Basi, kwa haraka wakazunguka katika nchi ile yote, wakaanza kuwachukua wagonjwa wamelala juu ya mikeka yao, wakawapeleka kila mahali waliposikia Yesu yupo.
56耶稣无论到什么地方,或村庄,或城市,或乡野,众人都把病人放在街上,求耶稣准他们摸他衣服的繸子,摸着的人就都好了。
56Kila mahali Yesu alipokwenda, vijijini, mijini, au mashambani, watu waliwaweka wagonjwa uwanjani, wakamsihi waguse walau pindo la vazi lake. Nao wote waliomgusa walipona.