1不可因传统废弃 神的诫命(太15:1-20)
1Baadhi ya Mafarisayo na walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu walikusanyika mbele ya Yesu.
2他们看见他的门徒有人用不洁的手,就是没有洗过的手吃饭,
2Waliona kwamba baadhi ya wanafunzi wake walikula mikate kwa mikono najisi, yaani bila kunawa.
3(原来法利赛人和所有的犹太人都拘守古人的传统,如果不认真洗手,就不吃东西;
3Maana Mafarisayo na Wayahudi wengine wote huzingatia mapokeo ya wazee wao: hawali kitu kabla ya kunawa mikono ipasavyo.
4从街市回来,不先洗手,也不吃东西,还有许多别的传统,他们都沿袭拘守,例如洗杯、洗罐、洗铜器等等。)
4Tena hawali kitu chochote kutoka sokoni mpaka wamekiosha kwanza. Kuna pia desturi nyingine walizopokea kama vile namna ya kuosha vikombe, sufuria na vyombo vya shaba.
5法利赛人和经学家问耶稣:“你的门徒为什么不遵行古人的传统,用不洁的手吃饭呢?”
5Basi, Mafarisayo na walimu wa Sheria wakamwuliza Yesu, "Mbona wanafunzi wako hawayajali mapokeo tuliyopokea kwa wazee wetu, bali hula chakula kwa mikono najisi?"
6耶稣对他们说:“以赛亚指着你们这班伪君子所说的预言是对的,经上记着:‘这人民用嘴唇尊敬我,心却远离我;
6Yesu akawajibu, "Wanafiki ninyi! Nabii Isaya alitabiri ukweli juu yenu alipoandika: Watu hawa, asema Mungu, huniheshimu kwa maneno matupu, lakini mioyoni mwao wako mbali nami.
7他们把人的规条当作道理去教导人,所以拜我也是徒然。’
7Kuniabudu kwao hakufai, maana mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu.
8你们拘守着人的传统,却离弃了 神的诫命。”
8Ninyi mnaiacha amri ya Mungu na kushikilia maagizo ya watu."
9耶稣又对他们说:“你们为了坚守自己的传统,而巧妙地把 神的诫命拒绝了。
9Yesu akaendelea kusema, "Ninyi mnajua kuepa kwa ujanja sheria ya Mungu kwa ajili ya kufuata mapokeo yenu.
10因为摩西说:‘当孝敬父母’,又说:‘咒骂父母的,必被处死。’
10Maana Mose aliamuru: Waheshimu baba yako na mama yako, na, Anayemlaani baba au mama, lazima afe.
11你们倒说:‘人对父母说,我应该给你的供奉,已经作了各耳板’(各耳板意思是奉给 神的供物),
11Lakini ninyi mwafundisha, Kama mtu anacho kitu ambacho angeweza kuwasaidia nacho baba au mama yake, lakini akasema kwamba kitu hicho ni Korbani (yaani ni zawadi kwa Mungu),
12你们就不让那人再为父母作什么。
12basi, halazimiki tena kuwasaidia wazazi wake.
13这样,你们借着所领受的传统,把 神的话废弃了。你们还作了许多这一类的事。”
13Hivyo ndivyo mnavyodharau neno la Mungu kwa ajili ya mafundisho mnayopokezana. Tena mnafanya mambo mengi ya namna hiyo."
14于是耶稣又把群众叫过来,对他们说:“你们大家都要听我说,也要明白:
14Yesu aliuita tena ule umati wa watu, akawaambia, "Nisikilizeni nyote, mkaelewe.
15从外面进去的,不能使人污秽,从里面出来的,才能使人污秽。”
15Hakuna kitu kinachoingia ndani ya mtu toka nje ambacho chaweza kumtia mtu najisi. Lakini kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia mtu najisi."
16(有些抄本有第16节:“有耳可听的,就应该听。”)
16Mwenye masikio na asikie!
17耶稣离开群众,进了屋子,门徒就来问他这比喻的意思。
17Alipouacha umati wa watu na kuingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza maana ya huo mfano.
18他对他们说:“连你们也是这样不明白吗?难道不知道从外面进去的,不能使人污秽吗?
18Naye akawaambia, "Je, hata ninyi hamwelewi? Je, hamwelewi kwamba kitu kinachomwingia mtu toka nje hakiwezi kumtia unajisi,
19因为不是进到他的心,而是进到他的肚腹,再排泄到外面去。”(他这样说是表示各样食物都是洁净的。)
19kwa maana hakimwingii moyoni, ila tumboni, na baadaye hutolewa nje chooni?" (Kwa kusema hivyo, Yesu alivihalalisha vyakula vyote.)
20接着他又说:“从人里面出来的,才会使人污秽。
20Akaendelea kusema, "Kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia najisi.
21因为从里面,就是从人的心里,发出恶念、淫乱、偷盗、凶杀、
21Kwa maana kutoka ndani, katika moyo wa mtu, hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji,
22奸淫、贪心、邪恶、诡诈、放荡、嫉妒、毁谤、骄傲、愚妄;
22uzinzi, uchoyo, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, kashfa, kiburi na upumbavu.
23这一切恶事,是从人里面出来的,都能使人污秽。”
23Maovu hayo yote yatoka ndani ya mtu, nayo humtia mtu najisi."
24叙利亚妇人的信心(太15:21-28)耶稣从那里动身到推罗(有些抄本在此有“和西顿”)境内去。进了一所房子,本来不想让人知道,却隐藏不住。
24Yesu aliondoka hapo, akaenda hadi wilaya ya Tiro. Huko aliingia katika nyumba moja na hakutaka mtu ajue; lakini hakuweza kujificha.
25有一个女人,她的小女儿被污灵附着,她听见了耶稣的事,就来俯伏在他脚前。
25Mwanamke mmoja ambaye binti yake alikuwa na pepo, alisikia habari za Yesu. Basi, akaja akajitupa chini mbele ya miguu yake.
26这女人是外族人,属于叙利亚的腓尼基族。她求耶稣把鬼从她女儿身上赶出去。
26Mama huyo alikuwa Mgiriki, mwenyeji wa Sirofoinike. Basi, akamwomba Yesu amtoe binti yake pepo mchafu.
27耶稣对她说:“应该先让儿女吃饱。拿儿女的饼去丢给小狗吃是不好的。”
27Yesu akamwambia, "Kwanza watoto washibe; kwa maana si vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa."
28那女人回答他:“主啊,是的,不过小狗在桌子底下,也可以吃孩子们掉下来的碎渣。”
28Lakini huyo mama akasema, "Sawa, Bwana, lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto."
29耶稣对她说:“就凭这句话,你回去吧,鬼已经从你女儿身上出去了。”
29Yesu akamwambia, "Kwa sababu ya neno hilo, nenda. Pepo amemtoka binti yako!"
30她回到家里,看见小孩子躺在床上,鬼已经出去了。
30Basi, akaenda nyumbani kwake, akamkuta mtoto amelala kitandani, na pepo amekwisha mtoka.
31治好又聋又哑的人(太15:29-31)耶稣从推罗境内出去,经过西顿,回到低加波利地区的加利利海。
31Kisha Yesu aliondoka wilayani Tiro, akapitia Sidoni, akafika ziwa Galilaya kwa kupitia nchi ya Dekapoli.
32有人带着一个又聋又哑的人到他那里,求耶稣按手在他身上。
32Basi, wakamletea bubu-kiziwi, wakamwomba amwekee mikono.
33耶稣把他从人群中带到一边,用指头探他的耳朵,吐唾沫抹他的舌头,
33Yesu akamtenga na umati wa watu, akamtia vidole masikioni, akatema mate na kumgusa ulimi.
34然后望着天,长长地叹了一口气,对他说:“以法大!”意思是“开了吧”。
34Kisha akatazama juu mbinguni, akapiga kite, akamwambia, "Efatha," maana yake, "Funguka."
35那人的耳朵就开了,舌头也松了,说话也准确了。
35Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukafunguliwa, akaanza kusema sawasawa.
36耶稣嘱咐他们不要告诉人。但他越是嘱咐,他们却越发传扬。
36Yesu akawaamuru wasimwambie mtu juu ya jambo hilo. Lakini kadiri alivyowakataza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari hiyo.
37众人非常惊讶说:“他所作的一切事都好极了;他竟然使聋子听见,又使哑巴说话。”
37Watu walishangaa sana, wakasema, "Amefanya yote vyema: amewajalia viziwi kusikia, na bubu kusema!"