聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Mark

8

1给四千人吃饱的神迹(太15:32-39)
1Wakati huo umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena, na hawakuwa na chakula. Basi, Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia,
2“我怜悯这一群人,因为他们和我在一起已经有三天,没有什么吃的了。
2"Nawahurumia watu hawa kwa sababu wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu, wala hawana chakula.
3如果我叫他们散开,饿着肚子回家去,他们会在路上晕倒,因为有人是从很远的地方来的。”
3Nikiwaacha waende nyumbani wakiwa na njaa watazimia njiani, maana baadhi yao wametoka mbali."
4门徒回答:“在这旷野地方,从哪里能找食物叫这些人吃饱呢?”
4Wanafunzi wake wakamwuliza, "Hapa nyikani itapatikana wapi mikate ya kuwashibisha watu hawa wote?"
5他问他们:“你们有多少饼?”他们说:“七个。”
5Yesu akawauliza, "Mnayo mikate mingapi?" Nao wakamjibu, "Saba."
6耶稣吩咐群众坐在地上;拿起那七个饼,祝谢了,擘开递给门徒,叫他们摆开;门徒就摆在众人面前,
6Basi, akawaamuru watu wakae chini. Akaitwaa ile mikate saba, akamshukuru Mungu, akaimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu, nao wakawagawia.
7他们还有几条小鱼,耶稣祝了福,就吩咐把这些也摆开。
7Walikuwa pia na visamaki vichache. Yesu akavibariki, akaamuru vigawiwe watu vilevile.
8众人都吃了,并吃饱了。他们把剩下的零碎收拾起来,装满了七个大篮子。
8Watu wakala, wakashiba. Wakaokota mabaki yaliyosalia wakajaza makapu saba.
9当时人数约有四千。耶稣解散了群众,
9Nao waliokula walikuwa watu wapatao elfu nne. Yesu akawaaga,
10就立刻和门徒上了船,来到大玛努他地区。
10na mara akapanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda wilaya ya Dalmanutha.
11求耶稣显神迹(太16:1-4)法利赛人出来,跟耶稣辩论;他们想试探他,求他显个从天上来的神迹。
11Mafarisayo walikuja, wakaanza kujadiliana na Yesu. Kwa kumjaribu, wakamtaka awafanyie ishara kuonyesha anayo idhini kutoka mbinguni.
12耶稣灵里深深地叹息,说:“这世代为什么总是寻求神迹?我实在告诉你们,决不会有神迹显给这个世代的!”
12Yesu akahuzunika rohoni, akasema, "Mbona kizazi hiki kinataka ishara? Kweli nawaambieni, kizazi hiki hakitapewa ishara yoyote!"
13于是他离开他们,又上船往对岸去了。
13Basi, akawaacha, akapanda tena mashua, akaanza safari kwenda ng'ambo ya pili ya ziwa.
14提防法利赛人和希律的酵(太16:5-12)门徒忘了带饼,船上除了一个饼,身边没有别的了。
14Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate; walikuwa na mkate mmoja tu katika mashua.
15耶稣嘱咐他们说:“你们要小心,提防法利赛人的酵和希律的酵!”
15Yesu akawaonya, "Angalieni sana! Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode."
16门徒彼此议论说:“这是因为我们没有饼吧?”
16Wanafunzi wakaanza kujadiliana wao kwa wao, "Anasema hivyo kwa kuwa hatuna mikate."
17耶稣知道了,就说:“为什么议论没有饼这件事呢?你们还不知道,还不明白吗?你们的心还是这么迟钝吗?
17Yesu alitambua hayo, akawaambia, "Mbona mnajadiliana juu ya kutokuwa na mikate? Je, bado hamjafahamu, wala hamjaelewa? Je, mioyo yenu imeshupaa?
18你们有眼不能看,有耳不能听吗?你们不记得吗?
18Je, Mnayo macho na hamwoni? Mnayo masikio na hamsikii? Je, hamkumbuki
19我擘开那五个饼给五千人吃,你们收拾的零碎装满了几个篮子呢?”他们说:“十二个。”
19wakati ule nilipoimega ile mikate mitano na kuwapa watu elfu tano? Mlikusanya vikapu vingapi vya mabaki ya makombo?" Wakamjibu, "Kumi na viwili."
20“那七个饼分给四千人吃,你们收拾的零碎装满了几个大篮子呢?”他们说:“七个。”
20"Na nilipoimega ile mikate saba na kuwapa watu elfu nne, mlikusanya makapu mangapi ya makombo?" Wakamjibu, "Saba."
21耶稣说:“你们还不明白吗?”
21Basi, akawaambia, "Na bado hamjaelewa?"
22治好伯赛大瞎眼的人后来他们到了伯赛大,有人带了一个瞎眼的人到他跟前,求耶稣摸他。
22Yesu alifika Bethsaida pamoja na wanafunzi wake. Huko watu wakamletea kipofu mmoja, wakamwomba amguse.
23耶稣拉着他的手,领他到村外,吐唾沫在他的眼睛上,又用双手按在他的身上,问他:“你看见什么没有?”
23Yesu akamshika mkono huyo kipofu, akampeleka nje ya kijiji. Akamtemea mate machoni, akamwekea mikono, akamwuliza, "Je, unaweza kuona kitu?"
24他往上一看,说:“我看见人了!看见他们好像树走来走去。”
24Huyo kipofu akatazama, akasema, "Ninawaona watu wanaoonekana kama miti inayotembea."
25于是耶稣再按手在他的眼睛上,他定睛一看,就复原了,样样都看得清楚了。
25Kisha Yesu akamwekea tena mikono machoni, naye akakaza macho, uwezo wake wa kuona ukamrudia, akaona kila kitu sawasawa.
26耶稣叫他回家去,说:“连这村子你也不要进去。”
26Yesu akamwambia aende zake nyumbani na kumwamuru, "Usirudi kijijini!"
27彼得承认耶稣是基督(太16:13-16、20;路9:18-21)耶稣和门徒出去,要到该撒利亚.腓立比附近的村庄。在路上他问门徒说:“人说我是谁?”
27Kisha Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika vijiji vya Kaisarea Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu aliwauliza wanafunzi wake, "Watu wanasema mimi ni nani?"
28他们回答:“有人说是施洗的约翰;有人说是以利亚;还有人说是先知里的一位。”
28Wakamjibu, "Wengine wanasema wewe ni Yohane Mbatizaji, wengine Eliya na wengine mmojawapo wa manabii."
29他又问他们说:“那么你们呢?你们说我是谁?”彼得回答:“你就是基督。”
29Naye akawauliza, "Na ninyi je, mnasema mimi ni nani?" Petro akamjibu, "Wewe ndiwe Kristo."
30耶稣郑重地嘱咐他们,不要把他的事告诉人。
30Kisha Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
31耶稣预言受难及复活(太16:21-28;路9:22-27)于是他教导他们,人子必须受许多苦,被长老、祭司长和经学家弃绝、杀害,三天后复活。
31Yesu alianza kuwafundisha wanafunzi wake: "Ni lazima Mwana wa Mtu apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wazee na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Atauawa na baada ya siku tatu atafufuka."
32耶稣坦白地说了这话,彼得就把他拉到一边,责怪他。
32Yesu aliwaambia jambo hilo waziwazi. Basi, Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea.
33耶稣转过身来,望着门徒,斥责彼得说:“撒但,退到我后面去!因为你不思念 神的事,只思念人的事。”
33Lakini Yesu akageuka, akawatazama wanafunzi wake, akamkemea Petro akisema, "Ondoka mbele yangu, Shetani! Fikira zako si za kimungu ila ni za kibinadamu!"
34于是把众人和门徒都叫过来,对他们说:“如果有人愿意跟从我,就应当舍己,背起他的十字架来跟从我。
34Kisha akauita umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, "Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
35凡是想救自己生命的,必丧掉生命;但为我和福音牺牲生命的,必救了生命。
35Maana mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza, lakini mtu atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema, atayaokoa.
36人就是赚得全世界,却赔上自己的生命,有什么好处呢?
36Je, kuna faida gani mtu kuupata ulimwengu wote na kuyapoteza maisha yake?
37人还能用什么换回自己的生命呢?
37Ama mtu atatoa kitu gani badala ya maisha yake?
38在淫乱罪恶的世代,凡把我和我的道当作可耻的,人子在他父的荣耀里,和圣天使一起降临的时候,也必把他当作可耻的。”
38Mtu yeyote katika kizazi hiki kiovu na kisichomjali Mungu anayenionea aibu mimi na mafundisho yangu, Mwana wa Mtu atamwonea aibu mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu."