聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Mark

9

1耶稣又对他们说:“我实在告诉你们,站在这里的,有人在没有尝过死味以前,必定看见 神的国带着能力降临。”
1Yesu akaendelea kuwaambia, "Kweli nawaambieni, wako wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa enzi."
2在山上改变形象(太17:1-13;路9:28-36)过了六天,耶稣带着彼得、雅各、约翰,领他们悄悄地上了高山,在他们面前改变了形象。
2Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane juu ya mlima mrefu peke yao. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao,
3他的衣服闪耀发光,极其洁白,地上漂布的没有能漂得这样白的。
3mavazi yake yakang'aa, yakawa meupe sana, jinsi dobi yeyote duniani asingeweza kuyafanya meupe.
4又有以利亚和摩西向他们显现,并且跟耶稣谈话。
4Eliya na Mose wakawatokea, wakazungumza na Yesu.
5彼得对耶稣说:“拉比,我们在这里真好!我们可以搭三个帐棚,一个为你,一个为摩西,一个为以利亚。”
5Petro akamwambia Yesu, "Mwalimu, ni vizuri sana kwamba tuko hapa. Basi, afadhali tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya."
6彼得不知道该说什么才好,因为他们都非常害怕。
6Yeye na wenzake waliogopa hata hakujua la kusema.
7有一片云彩来,笼罩他们,又有声音从云中出来:“这是我的爱子,你们要听他。”
7Kisha likatokea wingu likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu, "Huyu ni Mwanangu mpendwa, msikilizeni."
8门徒立刻周围观看,再也看不见别的人,只见耶稣单独和他们在一起。
8Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
9他们下山的时候,耶稣吩咐他们,人子从死人中复活之前,不要把所看见的告诉人。
9Walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoyaona, mpaka Mwana wa Mtu atakapokuwa amefufuka kutoka wafu.
10门徒把这句话记在心里,又彼此讨论从死人中复活是什么意思。
10Basi, wakashika agizo hilo, lakini wakawa wanajadiliana wao kwa wao maana ya kufufuka kutoka wafu.
11他们就问耶稣:“经学家为什么说以利亚必须先来呢?”
11Wakamwuliza Yesu, "Mbona walimu wa Sheria wanasema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?"
12耶稣说:“以利亚固然要先来复兴一切,但圣经为什么又记载人子要受许多苦,被人藐视呢?
12Naye akawajibu, "Naam, Eliya anakuja kwanza kutayarisha yote. Hata hivyo, kwa nini basi imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Mwana wa Mtu atapatwa na mateso mengi na kudharauliwa?
13其实我告诉你们,以利亚已经来了,他们却任意待他,正如经上指着他所说的。”
13Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyotaka kama ilivyoandikwa juu yake."
14治好癫痫病的小孩(太17:14-21;路9:37-42)他们回到门徒那里,看见一大群人围着他们,又有经学家和他们辩论。
14Walipowafikia wale wanafunzi wengine, waliona umati mkubwa wa watu hapo. Na baadhi ya walimu wa Sheria walikuwa wanajadiliana nao.
15众人看见了耶稣,都很惊奇,就跑上前去向他问安。
15Mara tu ule umati wa watu ulipomwona, wote walishangaa sana, wakamkimbilia wamsalimu.
16他问他们:“你们和他们辩论什么?”
16Yesu akawauliza, "Mnajadiliana nini nao?"
17群众当中有一个回答他:“老师,我把我的儿子带到你这里来,他被哑巴鬼附着。
17Hapo mtu mmoja katika ule umati wa watu akamjibu, "Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo aliyemfanya kuwa bubu.
18无论在哪里,鬼抓住他,把他摔倒,他就口吐白沫,咬牙切齿,浑身僵硬。我请你的门徒把鬼赶出去,他们却办不到。”
18Kila mara anapomvamia, humwangusha chini na kumfanya atokwe na povu kinywani, akisaga meno na kuwa mkavu mwili wote. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo lakini hawakuweza."
19耶稣回答他们:“唉!不信的世代啊!我跟你们在一起到几时呢?我要忍受你们到几时呢?把他带到我这里来吧。”
19Yesu akawaambia, "Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni kwangu."
20他们就把孩子带到他跟前。那鬼一见耶稣,就立刻使孩子抽了一阵疯,倒在地上,流着唾沫打滚。
20Wakampeleka. Mara tu huyo pepo alipomwona Yesu, alimtia mtoto kifafa, naye mtoto akaanguka chini, akagaagaa na kutoka povu kinywani. Yesu akamwuliza baba yake huyo mtoto,
21耶稣问他父亲:“这事临到他有多久了?”他说:“从小就是这样。
21"Amepatwa na mambo hayo tangu lini?" Naye akamjibu, "Tangu utoto wake.
22鬼常常把他扔在火里水中,要毁灭他。如果你能作什么,求你可怜我们,帮助我们。”
22Na mara nyingi pepo huyo amemwangusha motoni na majini, ili amwangamize kabisa. Basi, ikiwa waweza, utuhurumie na kutusaidia!"
23耶稣对他说:“‘如果你能’(“如果你能”有些抄本作“你若能信”)──对于信的人,什么都能!”
23Yesu akamwambia, "Eti ikiwa waweza! Mambo yote yanawezekana kwa mtu aliye na imani."
24孩子的父亲立刻喊着说:“我信!但我的信心不够,求你帮助我。”
24Hapo, huyo baba akalia kwa sauti, "Naamini! Lakini imani yangu haitoshi, nisaidie!"
25耶稣看见群众围拢了来,就斥责那污鬼说:“聋哑的鬼,我吩咐你从他身上出来,不要再进去。”
25Yesu alipouona umati wa watu unaongezeka upesi mbele yake, alimkemea yule pepo mchafu, "Pepo unayemfanya huyu mtoto kuwa bubu-kiziwi, nakuamuru, mtoke mtoto huyu wala usimwingie tena!"
26那鬼大声喊叫,使孩子重重地抽了一阵疯,就出来了。孩子好像死了一样,所以许多人都说:“他死了!”
26Hapo huyo pepo alipaaza sauti, akamwangusha huyo mtoto chini, kisha akamtoka. Mtoto alionekana kama maiti, hata wengine walisema, "Amekufa!"
27但耶稣拉着他的手,扶他起来,他就站起来了。
27Lakini Yesu akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
28耶稣进了屋子,门徒私下问他说:“为什么我们不能把那污鬼赶出去呢?”
28Yesu alipoingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza kwa faragha, "Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?"
29耶稣对他们说:“这一类的鬼,非用祷告是赶不出去的。”
29Naye akawaambia, "Pepo wa aina hii hawezi kutoka isipokuwa kwa sala tu."
30第二次预言受难及复活(太17:22-23;路9:43-45)他们从那里出去,经过加利利,耶稣不想让人知道,
30Yesu na wanafunzi wake waliondoka hapo, wakaendelea na safari kupitia wilaya ya Galilaya. Yesu hakupenda watu wajue alipokuwa,
31因为他正在教导门徒。他又对他们说:“人子将要被交在人的手里,他们要杀害他,死后三天他要复活。”
31kwa sababu alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, "Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu ambao watamuua; lakini siku ya tatu baada ya kuuawa atafufuka."
32门徒不明白这话,又不敢问他。
32Wanafunzi hawakufahamu jambo hilo. Wakaogopa kumwuliza.
33门徒争论谁最大(太18:1-5;路9:46-48)他们来到迦百农。在屋里的时候,耶稣问他们:“你们在路上争论什么?”
33Basi, walifika Kafarnaumu. Na alipokuwa nyumbani, aliwauliza, "Mlikuwa mnajadiliana nini njiani?"
34门徒一声不响,因为他们在路上彼此争论谁为大。
34Lakini wao wakanyamaza, maana njiani walikuwa wamebishana ni nani aliye mkuu kati yao.
35耶稣坐下,叫十二门徒来,对他们说:“谁想为首,就该作众人中最末的一个,作众人的仆人。”
35Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, "Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na kuwa mtumishi wa wote."
36于是拉过一个小孩子来,叫他站在门徒中间,又把他抱起来,对他们说:
36Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kati yao, akamku mbatia, halafu akawaambia,
37“凡因我的名接待一个这样的小孩子的,就是接待我;凡接待我的,不是接待我,而是接待那差我来的。”
37"Anayempokea mtoto kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi; na anayenipokea mimi, hanipokei mimi tu, bali anampokea yule aliyenituma."
38反对与赞成(路9:49-50)约翰对耶稣说:“老师,我们看见有一个人奉你的名赶鬼,就禁止他,因为他不跟从我们。”
38Yohane akamwambia, "Mwalimu, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako, nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu."
39耶稣说:“不要禁止他,因为没有人能奉我的名行了神迹,又立刻毁谤我。
39Lakini Yesu akasema, "Msimkataze, maana hakuna mtu anayefanya muujiza kwa jina langu, na papo hapo akaweza kusema mabaya juu yangu.
40不反对我们的,就是赞成我们的。
40Maana, asiyepingana nasi, yuko upande wetu.
41无论谁因你们有属基督的名分,给你们一杯水喝的,我实在告诉你们,他决不会失掉赏赐。
41Mtu yeyote atakeyewapeni kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni watu wake Kristo, hakika hatakosa kupata tuzo lake.
42坚拒犯罪(太18:6-9;路17:1-2)“如果有人使一个信我的小弟兄犯罪,倒不如在他的颈项上拴一块大磨石投在海里。
42"Mtu yeyote atakayemfanya mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini atende dhambi, ingekuwa afadhali kwa mtu huyo kufungiwa shingoni mwake jiwe kubwa la kusagia na kutupwa baharini.
43如果你的一只手使你犯罪,就把它砍下来。你身体残废进永生,总比有两只手下到地狱,进入那不灭的火里好得多。
43Mkono wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia kwenye uzima bila mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika moto wa Jehanamu.
44(有些抄本有第44节:“在那里虫是不死的,火是不灭的。”)
44Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
45如果你的一只脚使你犯罪,就把它砍下来。你瘸腿进永生,总比你有两只脚而被丢在地狱里好得多。
45Na mguu wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia katika uzima bila mguu mmoja, kuliko kuwa na miguu yote miwili na kutupwa katika moto wa Jehanamu.
46(有些抄本有第46节:“在那里虫是不死的,火是不灭的。”)
46Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
47如果你的一只眼睛使你犯罪,就把它挖出来。你只有一只眼睛进 神的国,总比你有两只眼睛而被丢在地狱里好得多,
47Na jicho lako likikukosesha, ling'oe! Afadhali kuingia katika utawala wa Mungu ukiwa na jicho moja tu, kuliko kuwa na macho yako yote mawili na kutupwa katika moto wa Jehanamu.
48在那里虫是不死的,火是不灭的。
48Humo wadudu wake hawafi, na moto hauzimiki.
49每一个人必被火当盐来腌。(有些抄本在此有“各祭物必用盐来腌”一句;也有些抄本只有附注的一句,而没有正文的一句)
49"Maana kila mmoja atakolezwa kwa moto.
50盐是好的,但如果失了味,可以用什么使它再咸呢?你们自己里面应当有盐,彼此和睦。”
50Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini? Muwe na chumvi ndani yenu na kudumisha amani kati yenu."