1差遣十二使徒(可3:13-19,6:8-13;路6:12-16,9:1-5。参路10:4-12;徒1:13)
1Yesu aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa uwezo wa kutoa pepo wachafu na kuponya magonjwa na maradhi yote.
2十二使徒的名字如下:为首的是西门(又名彼得),西门的弟弟安得烈,西庇太的儿子雅各,雅各的弟弟约翰,
2Majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya: wa kwanza ni Simoni aitwae Petro, na Andrea ndugu yake; Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohane ndugu yake;
3腓力,巴多罗迈,多马,税吏马太,亚勒腓的儿子雅各,达太,
3Filipo na Bartholomayo, Thoma na Mathayo aliyekuwa mtoza ushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo;
4激进派的西门,和出卖耶稣的加略人犹大。
4Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
5耶稣差遣这十二个人出去,并且嘱咐他们:“外族人的路,你们不要走,撒玛利亚人的城,你们也不要进;
5Yesu aliwatuma hao kumi na wawili na kuwapa maagizo haya: "Msiende kwa watu wa mataifa mengine, wala msiingie katika mji wa Wasamaria.
6却要到以色列家的迷羊那里去。
6Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.
7你们要一边走一边宣扬说:‘天国近了。’
7Mnapokwenda hubirini hivi: Ufalme wa mbinguni umekaribia.
8要医治有病的,叫死人复活,洁净患痲风的,赶出污鬼。你们白白地得来,也应当白白地给人。
8Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.
9你们腰袋里不要带金、银、铜钱;
9Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.
10路上不要带行囊,也不要带两件衣裳,不要带鞋或手杖,因为作工的理当得到供应。
10Msichukue mkoba wa kuombea njiani, wala koti la ziada, wala viatu, wala fimbo. Maana mfanyakazi anastahili riziki yake.
11你们无论进哪一座城哪一个村,都要打听谁配接待你们,就住在那里,直到离去。
11"Mkiingia katika mji wowote au kijiji, tafuteni humo mtu yeyote aliye tayari kuwakaribisheni, na kaeni naye mpaka mtakapoondoka mahali hapo.
12到他家里的时候,要向他们问安;
12Mnapoingia nyumbani wasalimuni wenyeji wake.
13如果这家是配得的,你们的平安就必临到他们;如果这家不配得,你们的平安仍归你们。
13Kama wenyeji wa nyumba hiyo wakiipokea salamu hiyo, basi, amani yenu itakaa pamoja nao. Lakini ikiwa hawaipokei, basi amani yenu itawarudia ninyi.
14如果有人不接待你们,不听你们的话,你们离开那一家那一城的时候,就要把脚上的灰尘跺下去。
14Kama mtu yeyote atakataa kuwakaribisheni au kuwasikilizeni, basi mtokapo katika nyumba hiyo au mji huo, yakung'uteni mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao.
15我实在告诉你们,在审判的日子,所多玛和蛾摩拉所受的,比那城还轻呢。
15Kweli nawaambieni, Siku ya hukumu mji huo utapata adhabu kubwa kuliko ile iliyoipata miji ya Sodoma na Gomora.
16使徒会遭受迫害(可13:11-13;路21:12-17)“现在,我差派你们出去,好像羊进到狼群中间;所以你们要像蛇一样机警,像鸽子一样纯洁。
16"Sasa, mimi nawatuma ninyi kama kondoo kati ya mbwa mwitu. Muwe na busara kama nyoka, na wapole kama njiwa.
17你们要小心,因为有人要把你们送交公议会,并要在会堂里鞭打你们;
17Jihadharini na watu, maana watawapeleka ninyi mahakamani na kuwapiga viboko katika masunagogi yao.
18你们为我的缘故,也要被带到统治者和君王面前,向他们和外族人作见证。
18Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu, mpate kutangaza Habari Njema kwao na kwa mataifa.
19你们被捕的时候,用不着担心说什么和怎么说,因为那时你们必得着当说的话;
19Basi, watakapowapeleka ninyi mahakamani, msiwe na wasiwasi mtasema nini au namna gani; wakati utakapofika, mtapewa la kusema.
20因为说话的不是你们,而是你们的父的灵,是他在你们里面说话。
20Maana si ninyi mtakaosema, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.
21弟兄要出卖弟兄,父亲要出卖儿子,甚至把他们置于死地;儿女要悖逆父母,害死他们。
21"Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe, na baba atamsaliti mwanawe, nao watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.
22你们为我的名,要被众人恨恶,然而坚忍到底的必然得救。
22Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokolewa.
23如果有人在这城迫害你们,就逃到别的城去。我实在告诉你们,你们还没有走遍以色列的各城,人子就来到了。
23"Watu wakiwadhulumu katika mji mmoja, kimbilieni mji mwingine. Kweli nawaambieni, hamtamaliza ziara yenu katika miji yote ya Israeli kabla Mwana wa Mtu hajafika.
24“学生不能胜过老师,奴仆也不能胜过主人。
24"Mwanafunzi si mkuu kuliko mwalimu wake, wala mtumishi si mkuu kuliko bwana wake.
25学生若能像老师一样,奴仆若能像主人一样,也就够了。如果一家之主也被称为别西卜(“别西卜”是鬼王的名字),何况他的家人呢?
25Yatosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumishi kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mkubwa wa jamaa Beelzebuli, je hawatawaita watu wengine wa jamaa hiyo majina mabaya zaidi?
26应该怕谁(路12:2-9)“所以不要怕他们。没有什么掩盖的事不被揭露,也没有什么秘密是人不知道的。
26"Basi, msiwaogope watu hao. Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, na kila kilichofichwa kitafichuliwa.
27我在暗处告诉你们的,你们要在明处讲出来;你们听见的耳语,要在房顶上宣扬出来。
27Ninalowaambieni ninyi katika giza, lisemeni katika mwanga; na jambo mlilosikia likinong'onezwa, litangazeni hadharani.
28那些杀身体却不能杀灵魂的,不要怕他们;倒要怕那位能把灵魂和身体都投入地狱里的。
28Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Afadhali zaidi kumwogopa yule awezaye kuuangamiza mwili pamoja na roho katika moto wa Jehanamu.
29两只麻雀不是卖一个大钱吗?但你们的父若不许可,一只也不会掉在地上。
29Shomoro wawili huuzwa kwa senti tano. Lakini hata mmoja wao haanguki chini bila kibali cha Baba yenu.
30甚至你们的头发都一一数过了。
30Lakini kwa upande wenu, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.
31所以不要怕,你们比许多麻雀贵重得多呢。
31Kwa hiyo msiogope; ninyi mu wa thamani kuliko shomoro wengi.
32“凡在人面前承认我的,我在我天父面前也要承认他;
32"Kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, mimi pia nitamkiri mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.
33在人面前不认我的,我在我天父面前也要不认他。
33Lakini yeyote atakayenikana hadharani, nami nitamkana mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.
34作门徒的代价(路12:51-53)“你们不要以为我来了,是要给地上带来和平;我并没有带来和平,却带来刀剑,
34"Msidhani kwamba nimekuja kuleta amani duniani. Sikuja kuleta amani bali upanga.
35因为我来了是要叫人分裂:人与父亲作对,女儿与母亲作对,媳妇与婆婆作对,
35Maana nimekuja kuleta mafarakano kati ya mtu na baba yake, kati ya binti na mama yake, kati ya mkwe na mkwe wake.
36人的仇敌就是自己的家人。
36Na maadui wa mtu ni watu wa nyumbani mwake.
37爱父母过于爱我的,不配作属我的;爱儿女过于爱我的,不配作属我的;
37"Ampendaye baba au mama yake kuliko anipendavyo mimi, hanistahili. Ampendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38凡不背起自己的十字架来跟从我的,也不配作属我的。
38Mtu asiyechukua msalaba wake na kunifuata, hanistahili.
39顾惜自己生命的,必要丧掉生命;但为我牺牲生命的,必要得着生命。
39Anayeyashikilia maisha yake, atayapoteza; lakini anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayapata.
40得赏赐(可9:41)“接待你们的,就是接待我;接待我的,就是接待那差我来的。
40"Anayewakaribisha ninyi, ananikaribisha mimi; na anayenikaribisha mimi, anamkaribisha yule aliyenituma.
41因先知的名接待先知的,必得先知所得的赏赐;因义人的名接待义人的,必得义人所得的赏赐。
41Anayemkaribisha nabii kwa sababu ni nabii, atapokea tuzo la nabii. Anayemkaribisha mtu mwema kwa sababu ni mtu mwema, atapokea tuzo la mtu mwema.
42无论谁因门徒的名,只把一杯凉水给这些微不足道的人中的一个喝,我实在告诉你们,他决不会得不到他的赏赐。”
42Kweli nawaambieni, yeyote atakayempa mmojawapo wa wadogo hawa kikombe cha maji baridi kwa sababu ni mfuasi wangu, hatakosa kamwe kupata tuzo lake."