聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Matthew

11

1约翰派门徒去见耶稣(路7:18-23)
1Yesu alipomaliza kuwapa wanafunzi kumi na wawili maagizo, alitoka hapo, akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
2约翰在监狱里听见基督所作的,就派门徒去问他:
2Yohane mbatizaji akiwa gerezani alipata habari juu ya matendo ya Kristo. Basi, Yohane akawatuma wanafunzi wake,
3“你就是那位要来的,还是我们要等别人呢?”
3wamwulize: "Je, wewe ni yule anayekuja, au tumngoje mwingine?"
4耶稣回答他们:“你们回去,把听见和看见的都告诉约翰,
4Yesu akawajibu, "Nendeni mkamwambie Yohane mambo mnayoyasikia na kuyaona:
5就是瞎的可以看见,瘸的可以走路,患痲风的得到洁净,聋的可以听见,死人复活,穷人有福音听。
5vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa na viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa Habari Njema.
6那不被我绊倒的,就有福了。”
6Heri mtu yule asiyekuwa na mashaka nami."
7耶稣论到约翰(路7:24-35)他们走了之后,耶稣对群众讲起约翰来,说:“你们到旷野去,是要看什么?被风吹动的芦苇吗?
7Basi, hao wajumbe wa Yohane walipokuwa wanakwenda zao, Yesu alianza kuyaambia makundi ya watu habari za Yohane: "Mlikwenda kutazama nini kule jangwani? Je, mlitaka kuona mwanzi unaotikiswa na upepo?
8你们出去到底要看什么?身穿华丽衣裳的人吗?那些穿着华丽衣裳的人,是在王宫里的。
8Lakini mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumtazama mtu aliyevaa mavazi maridadi? Watu wanaovaa mavazi maridadi hukaa katika nyumba za wafalme.
9那么,你们出去要看什么?先知吗?我告诉你们,是的。他比先知重要得多了。
9Basi, mlikwenda kuona nini? Nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.
10经上所记:‘看哪,我差遣我的使者在你面前,他必在你前头预备你的道路。’这句话是指着他说的。
10"Huyu ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu: Tazama, hapa namtuma mjumbe wangu, asema Bwana, akutangulie na kukutayarishia njia yako.
11我实在告诉你们,妇人所生的,没有一个比施洗的约翰更大;然而天国里最小的比他还大。
11Kweli nawaambieni, miongoni mwa watoto wote wa watu, hajatokea aliye mkuu kuliko Yohane mbatizaji. Hata hivyo, yule aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa mbinguni, ni mkubwa kuliko yeye.
12从施洗的约翰的时候直到现在,天国不断遭受猛烈的攻击,强暴的人企图把它夺去。
12Tangu wakati wa Yohane mbatizaji mpaka leo hii, Ufalme wa mbinguni unashambuliwa vikali, na watu wakali wanajaribu kuunyakua kwa nguvu.
13所有的先知和律法,直到约翰为止,都说了预言。
13Mafundisho yote ya manabii na sheria yalibashiri juu ya nyakati hizi.
14如果你们肯接受,约翰就是那要来的以利亚。
14Kama mwaweza kukubali basi, Yohane ndiye Eliya ambaye angekuja.
15有耳的,就应当听。
15Mwenye masikio na asikie!
16“我要把这世代比作什么呢?它好像一些小孩子坐在市中心,呼叫别的小孩子,
16"Basi, nitakifananisha kizazi hiki na kitu gani? Ni kama vijana waliokuwa wamekaa uwanjani, wakawa wakiambiana kikundi kimoja kwa kingine:
17说:‘我们给你们吹笛子,你们却不跳舞;我们唱哀歌,你们也不捶胸。’
17Tumewapigieni ngoma lakini hamkucheza; tumeimba nyimbo za huzuni lakini hamkulia!
18约翰来了,不吃也不喝,人说他是鬼附的;
18Kwa maana Yohane alikuja, akafunga na wala hakunywa divai, nao wakasema: Amepagawa na pepo.
19人子来了,又吃又喝,人却说:‘你看,这人贪食好酒,与税吏和罪人为友。’但智慧借着它所作的,就证实是公义的了。”
19Mwana wa Mtu akaja, anakula na kunywa, nao wakasema: Mtazameni huyu, mlafi na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wahalifu! Hata hivyo, hekima ya Mungu inathibitishwa kuwa njema kutokana na matendo yake."
20责备不肯悔改的城(路10:13-15)那时,耶稣责备那些他曾在那里行过许多神迹的城,因为它们不肯悔改:
20Kisha Yesu akaanza kuilaumu miji ambayo, ingawaje alifanya miujiza mingi humo, watu wake hawakutaka kubadili nia zao mbaya:
21“哥拉逊啊,你有祸了!伯赛大啊,你有祸了!在你们那里行过的神迹,如果行在推罗和西顿,它们早已披麻蒙灰悔改了。
21"Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwisha vaa mavazi ya gunia na kujipaka majivu zamani, ili kuonyesha kwamba wametubu.
22但我告诉你们,在审判的日子,推罗和西顿所受的,比你们还轻呢。
22Hata hivyo nawaambieni, Siku ya hukumu, ninyi mtapata adhabu kubwa kuliko Tiro na Sidoni.
23迦百农啊!你会被高举到天上吗?你必降到阴间。在你那里行过的神迹,如果行在所多玛,那城还会存留到今天。
23Na wewe Kafarnaumu, je, utajikweza mpaka mbinguni? Utaporomoshwa mpaka Kuzimu! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika kule Sodoma, mji huo ungalikuwako mpaka hivi leo.
24但我告诉你们,在审判的日子,所多玛那地方所受的,比你还轻呢。”
24Lakini nawaambieni, Siku ya hukumu itakuwa nafuu zaidi kwa watu wa Sodoma, kuliko kwako wewe."
25劳苦者可得安息(路10:21-22)就在那时候,耶稣说:“父啊,天地的主,我赞美你,因为你把这些事向智慧和聪明的人隐藏起来,却向婴孩显明。
25Wakati huo Yesu alisema, "Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, maana umewaficha wenye hekima mambo haya, ukawafumbulia watoto wadogo.
26父啊,是的,这就是你的美意。
26Naam Baba, ndivyo ilivyokupendeza.
27我父已经把一切交给我;除了父没有人认识子,除了子和子所愿意启示的人,没有人认识父。
27"Baba yangu amenikabidhi vitu vyote. Hakuna amjuaye Mwana ila Baba, wala amjuaye Baba ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana atapenda kumjulisha.
28你们所有劳苦担重担的人哪,到我这里来吧!我必使你们得安息。
28Njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29我心里柔和谦卑,你们应当负我的轭,向我学习,你们就必得着心灵的安息;
29Jifungeni nira yangu, mkajifunze kwangu, maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtatulizwa rohoni mwenu.
30我的轭是容易负的,我的担子是轻省的。”
30Maana, nira niwapayo mimi ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi."