1施洗约翰被杀(可6:14-29)
1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
2就对臣仆说:“这人是施洗的约翰,他从死人中复活,所以他身上有行神迹的能力。”
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
3原来希律为了他弟弟腓力的妻子希罗底的缘故,拘捕了约翰,把他捆绑,关在监里,
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
4因为约翰多次告诉他:“你占有她是不合理的。”
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
5他想杀约翰,但又害怕群众,因为他们都认为约翰是个先知。
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
6到了希律生日的那天,希罗底的女儿在众人面前跳舞,希律非常高兴,
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
7就起誓答应她,无论求什么都给她。
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
8她在母亲的怂恿之下,说:“请把施洗的约翰的头放在盘子上给我。”
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
9王就忧愁,但因为誓言和在座的宾客,就下令给她。
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
10他派人去,在监里斩了约翰的头,
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
11把头放在盘子上,拿来给那女孩子,她又带给母亲。
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
12约翰的门徒前来,领了尸体,把它埋葬,然后去告诉耶稣。
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
13给五千人吃饱的神迹(可6:32-44;路9:10-17;约6:1-13。参太15:32-38)耶稣听见了,就离开那里,独自坐船到旷野去。群众听见了,就从各城步行来跟随他。
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
14耶稣上了岸,看见一大群人,就怜悯他们,医好了他们的病人。
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
15黄昏的时候,门徒前来对他说:“这是旷野的地方,时间也不早了,请叫群众散开,好让他们往村里去,买自己的食物吧。”
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
16耶稣回答:“他们用不着离开,你们给他们吃吧!”
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
17但门徒说:“我们这里除了五个饼和两条鱼,什么也没有。”
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
18他说:“拿过来给我。”
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
19于是吩咐群众坐在草地上,拿起那五个饼两条鱼,望着天,祝谢了;然后把饼擘开,递给门徒,门徒又分给群众。
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
20大家都吃了,并且吃饱了,他们把剩下的零碎拾起来,装满了十二个篮子。
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21吃的人,除了妇女和孩子,约有五千。
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22耶稣在海面上行走(可6:45-52;约6:15-21)耶稣立刻催门徒上船,叫他们先到对岸去,他却留下来叫群众散开。
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
23他解散了群众,就独自上山去祷告。到了晚上,他还是独自一人在那里。
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
24那时门徒的船已经离岸数公里,因为逆风,被波浪冲击。
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
25天快亮的时候(“天快亮的时候”原文作“夜里四更天”),耶稣在海面上向他们走过去。
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
26门徒见他在海面上行走,就很惊慌,说:“有鬼啊!”并且恐惧得大叫起来。
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
27耶稣立刻对他们说:“放心吧!是我,不要怕。”
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
28彼得对他说:“主啊,如果是你,让我在水面上到你那里去。”
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
29他说:“来吧!”彼得就从船上下来,行在水面上,走向耶稣那里去。
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
30但他一见风浪就害怕,快要沉下去的时候,就呼叫:“主啊!救我!”
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
31耶稣马上伸手拉住他,对他说:“小信的人哪,为什么疑惑?”
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
32他们上了船,风就平静了。
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
33船上的人都拜他,说:“你真是 神的儿子。”
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
34治好革尼撒勒的病人(可6:53-56)他们过到对岸,来到革尼撒勒的地区。
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
35那地的人认出是耶稣,就把消息传遍了那一带。众人把一切有病的人都带来,
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
36求耶稣让他们只摸一摸他衣服的繸子,摸着的人就都痊愈了。
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.