聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Matthew

15

1不可因传统废弃 神的诫命(可7:1-23)
1Kisha Mafarisayo na walimu wa Sheria wakafika kutoka Yerusalemu, wakamwendea Yesu, wakamwuliza,
2“你的门徒为什么违背古人的传统,在饭前不洗手呢?”
2"Kwa nini wanafunzi wako hawajali mapokeo tuliyopokea kutoka kwa wazee wetu? Hawanawi mikono yao kama ipasavyo kabla ya kula!"
3耶稣回答:“你们又为什么因你们的传统,违背 神的诫命呢?
3Yesu akawajibu, "Kwa nini nanyi mnapendelea mapokeo yenu wenyewe na hamuijali Sheria ya Mungu?
4 神说:‘当孝敬父母’,又说:‘咒骂父母的必被处死’。
4Mungu amesema: Waheshimu baba yako na mama yako, na Anayemkashifu baba yake au mama yake, lazima auawe.
5你们却说:‘人若对父母说:“我应该给你们的,已经作了献给 神的礼物”,
5Lakini ninyi mwafundisha ati mtu akiwa na kitu ambacho angeweza kuwasaidia nacho baba au mama yake, lakini akasema: Kitu hiki nimemtolea Mungu,
6他就可以不孝敬父母了。’你们因为你们的传统,就废弃了 神的话。
6basi, hapaswi tena kumheshimu baba yake! Ndivyo mnavyodharau neno la Mungu kwa kufuata mafundisho yenu wenyewe.
7伪君子啊,以赛亚指着你们说的预言说得好:
7Enyi wanafiki! Isaya alitabiri sawa kabisa juu yenu:
8‘这人民用嘴唇尊敬我,心却远离我;
8Watu hawa, asema Mungu, huniheshimu kwa maneno tu, lakini mioyoni mwao wako mbali nami.
9他们把人的规条当作道理去教导人,所以拜我也是徒然。’”
9Kuniabudu kwao hakufai, maana mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu."
10耶稣叫群众前来,对他们说:“你们要听,也要明白。
10Yesu aliuita ule umati wa watu, akawaambia, "Sikilizeni na muelewe!
11进到口里的不能使人污秽,只有从口里出来的,才能使人污秽。”
11Kitu kinachomtia mtu najisi si kile kiingiacho kinywani, bali kile kitokacho kinywani. Hicho ndicho kimtiacho mtu najisi."
12门徒前来告诉他:“法利赛人听了这话很生气,你知道吗?”
12Kisha wanafunzi wakamwendea, wakamwambia, "Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa waliposikia maneno yako?"
13耶稣说:“所有不是我天父栽种的植物,都要连根拔起来。
13Lakini yeye akawajibu, "Kila mmea ambao Baba yangu aliye mbinguni hakuupanda, utang'olewa.
14由得他们吧!他们是瞎眼的,却作了向导;如果瞎子领瞎子,二人都会跌进坑里。”
14Waacheni wenyewe! Wao ni vipofu, viongozi wa vipofu; na kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili hutumbukia shimoni."
15彼得说:“请你给我们解释这个比喻吧。”
15Petro akadakia, "Tufafanulie huo mfano."
16耶稣说:“你们还是不明白吗?
16Yesu akasema, "Hata nyinyi hamwelewi?
17难道不知道一切进到口里的,是进到肚腹,然后排泄到外面去吗?
17Je, hamwelewi kwamba kila kinachoingia kinywani huenda tumboni na baadaye hutupwa nje chooni?
18但从口里出来的,是发自内心,才会使人污秽。
18Lakini yale yatokayo kinywani hutoka moyoni, na hayo ndiyo yanayomtia mtu najisi.
19因为从心里出来的,有恶念、凶杀、奸淫、淫乱、偷盗、假见证和毁谤。
19Maana moyoni hutoka mawazo maovu yanayosababisha uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na kashfa.
20这些才会使人污秽,不洗手吃饭却不会这样。”
20Hayo ndiyo yanayomtia mtu najisi. Lakini kula chakula bila kunawa mikono hakumtii mtu najisi."
21迦南妇人的信心(可7:24-30)耶稣离开那里,来到推罗、西顿境内。
21Yesu aliondoka mahali hapo akaenda kukaa katika sehemu za Tiro na Sidoni.
22有一个迦南的妇人从那地区出来,喊着说:“主啊,大卫的子孙,可怜我吧!我的女儿被鬼附得很苦。”
22Basi, mama mmoja Mkaanani wa nchi hiyo alimjia, akapaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, nionee huruma! Binti yangu anasumbuliwa na pepo."
23耶稣一句话也不回答她。门徒上前求他说:“请叫她走吧,她一直跟在我们后面喊叫。”
23Lakini Yesu hakumjibu neno. Basi, wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, "Mwambie aende zake kwa maana anatufuatafuata akipiga kelele."
24耶稣回答:“我被差遣,只是到以色列家的迷羊那里去。”
24Yesu akajibu, "Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo."
25她来跪在耶稣面前说:“主啊,求你帮助我!”
25Hapo huyo mama akaja, akapiga magoti mbele yake, akasema, "Mheshimiwa, nisaidie."
26耶稣回答:“拿儿女的饼丢给小狗吃是不好的。”
26Yesu akamjibu, "Si sawa kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa."
27她说:“主啊,是的,不过小狗也吃主人桌子上掉下来的碎渣。”
27Huyo mama akajibu, "Ni kweli, Mheshimiwa; lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka meza ya bwana wao."
28于是耶稣对她说:“妇人,你的信心真大,照你所想的给你成就吧!”从那时起,她的女儿就好了。
28Hapo Yesu akamjibu, "Mama, imani yako ni kubwa; basi, ufanyiwe kama unavyotaka." Yule binti yake akapona tangu saa hiyo wakati huohuo.
29治好许多病人(可7:31-37)耶稣离开那里,来到加利利海边,就上山坐下。
29Yesu alitoka hapo akaenda kando ya ziwa Galilaya, akapanda mlimani, akaketi.
30有许多人来到他那里,把瘸腿的、瞎眼的、残废的、哑的和许多别的病人,都带到耶稣跟前,他就医好他们。
30Watu wengi sana wakamjia wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaweka mbele ya miguu yake, naye Yesu akawaponya.
31群众看见哑巴说话,残废的复原,瘸腿的行走,瞎眼的看见,就十分惊奇,于是颂赞以色列的 神。
31Umati ule wa watu ulishangaa sana ulipoona bubu wakiongea, waliokuwa wamelemaa wamepona, viwete wakitembea na vipofu wakiona; wakamsifu Mungu wa Israeli.
32给四千人吃饱的神迹(可8:1-10。参太14:13-21)耶稣叫门徒前来,说:“我怜悯这一群人,因为他们跟我在一起已经有三天,也没有什么吃的;我不想叫他们饿着肚子回去,恐怕他们在路上晕倒。”
32Basi, Yesu aliwaita wanafunzi wake, akasema, "Nawaonea watu hawa huruma kwa sababu kwa siku tatu wamekuwa nami, wala hawana chakula. Sipendi kuwaacha waende bila kula wasije wakazimia njiani."
33门徒对他说:“我们在这旷野地方,哪里有足够的食物给这许多的人吃饱呢?”
33Wanafunzi wakamwambia, "Hapa tuko nyikani; tutapata wapi chakula cha kuwatosha watu wengi hivi?"
34耶稣问他们:“你们有多少饼?”他们说:“七个饼和几条小鱼。”
34Yesu akawauliza, "Mnayo mikate mingapi?" Wakamjibu, "Saba na visamaki vichache."
35他就吩咐群众坐在地上,
35Basi, Yesu akawaamuru watu wakae chini.
36拿起那七个饼和那些鱼,祝谢了,擘开递给门徒,门徒又分给众人。
36Akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi, nao wakawagawia watu.
37大家都吃了,并且吃饱了。他们把剩下的零碎拾起来,装满了七个大篮子。
37Wote wakala, wakashiba. Kisha wakakusanya makombo, wakajaza vikapu saba.
38吃的人,除了妇女和孩子,共有四千。
38Hao waliokula walikuwa wanaume elfu nne, bila kuhesabu wanawake na watoto.
39耶稣解散了群众,就上了船,来到马加丹地区。
39Basi, Yesu akawaaga watu, akapanda mashua, akaenda katika eneo la Magadani.