1求耶稣显神迹(可8:11-13)
1Mafarisayo na Masadukayo walimwendea Yesu, na kwa kumjaribu, wakamwomba afanye ishara itokayo mbinguni.
2耶稣回答:“黄昏的时候,你们说:‘天色通红,明天一定是晴天。’
2Lakini Yesu akawajibu, "Wakati wa jioni ukifika ninyi husema: Hali ya hewa itakuwa nzuri kwa maana anga ni jekundu!
3早上的时候,你们说:‘天色又红又暗,今天一定有风雨。’你们知道分辨天色,却不能分辨时代的征兆吗?
3Na alfajiri mwasema: Leo hali ya hewa itakuwa ya dhoruba, maana anga ni jekundu na tena mawingu yametanda! Basi, ninyi mnajua sana kusoma majira kwa kuangalia anga, lakini kutambua dalili za nyakati hizi hamjui.
4邪恶和淫乱的世代要寻求神迹,除了约拿的神迹之外,不会有什么神迹给它了。”耶稣就离开他们走了。
4Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara, lakini hamtapewa ishara yoyote isipokuwa tu ile ya Yona." Basi, akawaacha, akaenda zake.
5提防法利赛人等的教训(可8:14-21)门徒到了对岸,忘记了带饼。
5Wanafunzi wake walipokwisha vukia upande wa pili wa ziwa, walijikuta wamesahau kuchukua mikate.
6耶稣对他们说:“你们要小心,提防法利赛人和撒都该人的酵。”
6Yesu akawaambia, "Muwe macho na mjihadhari na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo!"
7他们就彼此议论说:“这是因为我们没有带饼吧。”
7Lakini wao wakawa wanajadiliana: "Anasema hivyo kwa kuwa hatukuchukua mikate."
8耶稣知道了,就说:“小信的人,为什么议论没有饼这件事呢?
8Yesu alijua mawazo yao, akawaambia, "Enyi watu wenye imani haba! Mbona mnajadiliana juu ya kutokuwa na mikate?
9你们还不明白吗?你们是不是忘记了那五个饼分给五千人,又装满了多少个篮子呢?
9Je, hamjaelewa bado? Je, hamkumbuki nilipoimega ile mikate mitano kwa ajili ya wale watu elfu tano? Je, mlijaza vikapu vingapi vya makombo?
10还是忘记了那七个饼分给四千人,又装满了多少个大篮子呢?
10Au, ile mikate saba waliyogawiwa wale watu elfu nne, je, mlikusanya vikapu vingapi vya mabaki?
11我对你们讲的不是饼的事,你们为什么不明白?你们要提防法利赛人和撒都该人的酵。”
11Inawezekanaje hamwelewi ya kwamba sikuwa nikisema juu ya mikate? Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo!"
12这时他们才领会耶稣说的不是要提防饼酵,而是要提防法利赛人和撒都该人的教训。
12Hapo wanafunzi wakafahamu kwamba aliwaambia wajihadhari siyo na chachu ya mikate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
13彼得承认耶稣是基督(可8:27-29;路9:18-20)耶稣来到该撒利亚.腓立比的地区,就问自己的门徒:“人说人子是谁?”
13Yesu alipofika pande za Kaisarea Filipi, aliwauliza wanafunzi wake, "Watu wanasema Mwana wa Mtu kuwa ni nani?"
14他们回答:“有人说是施洗的约翰,有人说是以利亚,也有人说是耶利米,或是先知里的一位。”
14Wakamjibu, "Wengine wanasema kuwa ni Yohane mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii."
15他问他们:“你们说我是谁?”
15Yesu akawauliza, "Na ninyi je, mwasema mimi ni nani?"
16西门.彼得回答:“你是基督,是永生 神的儿子。”
16Simoni Petro akajibu, "Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai."
17耶稣对他说:“约拿的儿子西门,你是有福的,因为这不是人(“人”原文作“肉和血”)指示你的,而是我在天上的父启示你的。
17Yesu akasema, "Heri wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana si binadamu aliyekufunulia ukweli huu, ila Baba yangu aliye mbinguni.
18我告诉你,你是彼得,我要在这磐石上建立我的教会,死亡的权势(“死亡的权势”原文作“阴间的门”)不能胜过他。
18Nami nakwambia: wewe ni Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala kifo chenyewe hakitaweza kulishinda.
19我要把天国的钥匙给你,你在地上捆绑的,在天上也被捆绑;你在地上释放的,在天上也被释放。”
19Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni; kila utakachofunga duniani, kitafungwa pia mbinguni; kila utakachofungua duniani, kitafunguliwa pia mbinguni."
20于是耶稣吩咐门徒不可对人说他就是基督。
20Kisha akawaonya wanafunzi wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
21耶稣预言受难及复活(可8:31-9:1;路9:22-27)从那时起,耶稣开始向门徒指出,他必须往耶路撒冷去,受长老、祭司长和经学家许多的苦害,并且被杀,第三天复活。
21Tangu wakati huo Yesu alianza kuwajulisha waziwazi wanafunzi wake: "Ni lazima mimi niende Yerusalemu, na huko nikapate mateso mengi yatakayosababishwa na wazee, makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Nitauawa, na siku ya tatu nitafufuliwa."
22彼得就把他拉到一边,责怪他说:“主啊,千万不可这样,这事一定不会发生在你身上的。”
22Hapo Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea: "Isiwe hivyo Bwana! Jambo hili halitakupata!"
23耶稣转过来对彼得说:“撒但!退到我后面去!你是绊倒我的,因为你不思念 神的事,只思念人的事。”
23Lakini Yesu akageuka, akamwambia Petro, "Ondoka mbele yangu Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Mawazo yako si ya mungu bali ni ya kibinadamu!"
24于是耶稣对门徒说:“如果有人愿意跟从我,就当舍己,背起他的十字架来跟从我。
24Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kama mtu yeyote anataka kuwa mfuasi wangu, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
25凡是想救自己生命的,必丧掉生命;但为我牺牲生命的,必得着生命。
25Maana, mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza;
26人若赚得全世界,却赔上自己的生命,有什么好处呢?人还能用什么换回自己的生命呢?
26lakini mtu anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayapata. Je, mtu atafaidi nini akiupata utajiri wote wa ulimwengu na hali amepoteza maisha yake? Au, mtu atatoa kitu gani kiwe badala ya maisha yake?
27人子要在父的荣耀里和众天使一同降临,那时他要照各人的行为报应各人。
27Maana, Mwana wa Mtu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika wake, na hapo ndipo atakapomlipa kila mtu kadiri ya matendo yake.
28我实在告诉你们,站在这里的,有人在没有尝过死味以前,必要看见人子带着他的国降临。”
28Kweli nawaambieni, wako wengine papahapa ambao hawatakufa kabla ya kumwona Mwana wa Mtu akija katika Ufalme wake."