聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Matthew

17

1在山上改变形象(可9:2-13;路9:28-36)
1Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu.
2耶稣在他们面前改变了形象,脸好像太阳一样照耀,衣服洁白像光。
2Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3忽然,摩西和以利亚向他们显现,跟耶稣谈话。
3Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye.
4彼得对耶稣说:“主啊,我们在这里真好。如果你愿意,我就在这里搭三个帐棚,一个为你,一个为摩西,一个为以利亚。”
4Hapo Petro akamwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya."
5彼得还说话的时候,有一朵明亮的云彩笼罩他们,云中有声音说:“这是我的爱子,我所喜悦的,你们要听他。”
5Alipokuwa bado anasema hivyo, wingu jeupe likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye, msikilizeni."
6门徒听见了,就俯伏在地上,非常害怕。
6Wanafunzi waliposikia hivyo wakaanguka kifudifudi, wakaogopa sana.
7耶稣前来,摸着他们说:“起来,不用怕。”
7Yesu akawaendea, akawagusa, akasema, "Simameni, msiogope!"
8他们抬起头来,看见只有耶稣自己,没有别的人。
8Walipoinua macho yao hawakumwona mtu, ila Yesu peke yake.
9他们下山的时候,耶稣吩咐他们:“人子从死人中复活以前,你们不要把所看见的异象告诉人。”
9Basi, walipokuwa wanashuka mlimani, Yesu akawaonya: "Msimwambie mtu mambo mliyoyaona mpaka Mwana wa Mtu atakapofufuliwa kutoka wafu."
10门徒就问他:“那么经学家为什么说,以利亚必须先来呢?”
10Kisha wanafunzi wakamwuliza, "Mbona walimu wa Sheria wanasema ati ni lazima kwanza Eliya aje?"
11他回答:“以利亚当然要来,并且复兴一切。
11Yesu akawajibu, "Kweli, Eliya atakuja kutayarisha mambo yote.
12但我告诉你们,以利亚已经来了,可是人们却不认识他,反而任意待他。照样,人子也要这样被他们苦待。”
12Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja nao hawakumtambua, bali walimtendea jinsi walivyotaka. Mwana wa Mtu atateswa vivyo hivyo mikononi mwao."
13这时门徒才领悟,耶稣是指着施洗的约翰说的。
13Hapo hao wanafunzi wakafahamu kwamba alikuwa akiwaambia juu ya Yohane mbatizaji.
14治好癫痫病的小孩(可9:14-29;路9:37-42)耶稣和门徒来到群众那里,有一个人前来,跪下对耶稣说:
14Walipojiunga tena na ule umati wa watu, mtu mmoja alimwendea Yesu, akampigia magoti,
15“主啊,可怜我的儿子吧,他患了癫痫病,非常痛苦,好几次掉进火里和水中。
15akasema, "Mheshimiwa, mwonee huruma mwanangu kwa kuwa ana kifafa, tena anateseka sana; mara nyingi yeye huanguka motoni na majini.
16我带他去见你的门徒,他们却不能医好他。”
16Nilimleta kwa wanafunzi wako lakini hawakuweza kumponya."
17耶稣说:“唉!这又不信又乖谬的世代啊!我要跟你们在一起到几时呢?我要忍受你们到几时呢?把孩子带到我这里来吧。”
17Yesu akajibu, "Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia ninyi mpaka lini? Mleteni hapa huyo mtoto."
18耶稣斥责那鬼,鬼就从孩子身上出来;从那时起,孩子就好了。
18Basi, Yesu akamkemea huyo pepo, naye akamtoka, na yule mtoto akapona wakati huohuo.
19门徒悄悄地前来问耶稣:“为什么我们不能把鬼赶出去呢?”
19Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha, wakamwuliza, "Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa yule pepo?"
20他说:“因为你们的信心太小了。我实在告诉你们,只要你们的信心像一粒芥菜种,就是对这山说:‘从这里移到那里’,它也必移开。没有什么是你们不能作的。”
20Yesu akawajibu, "Kwa sababu ya imani yenu haba. Nawaambieni kweli, kama tu mkiwa na imani, hata iwe ndogo kama mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu: Toka hapa uende pale, nao utakwenda. Hakuna chochote ambacho hakingewezekana kwenu."
21(有些抄本有第21节:“这一类的鬼,如果不靠祷告和禁食,是赶不出来的。”)
21"Pepo wa namna hii hawezi kuondolewa ila kwa sala na kufunga."
22第二次预言受难及复活(可9:30-32;路9:43-45)他们聚集在加利利的时候,耶稣对门徒说:“人子将要被交在人的手里,
22Walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu aliwaambia, "Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu.
23他们要杀害他,第三天他要复活。”他们就很忧愁。
23Watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa." Wanafunzi wakahuzunika mno.
24缴纳殿税他们来到迦百农,收殿税的人前来对彼得说:“你们的老师不纳税吗?”
24Walipofika Kafarnaumu watu wenye kukusanya fedha ya zaka ya Hekalu walimwendea Petro, wakamwuliza, "Je, mwalimu wenu hulipa fedha ya zaka?"
25他说:“纳。”他进到屋子里,耶稣先问他:“西门,你认为怎样?地上的君王向谁征收关税和丁税?向自己的儿子还是外人呢?”
25Petro akajibu, "Naam, hulipa." Basi, Petro alipoingia ndani ya nyumba, kabla hata hajasema neno, Yesu akamwuliza, "Simoni, wewe unaonaje? Wafalme wa dunia hukusanya ushuru au kodi kutoka kwa kina nani? Kutoka kwa wananchi ama kutoka kwa wageni?"
26他回答:“外人。”耶稣对他说:“这样,儿子就可以免税了。
26Petro akajibu, "Kutoka kwa wageni." Yesu akamwambia, "Haya basi, wananchi hawahusiki.
27但为了避免触犯他们,你要到海边去钓鱼;把第一条钓上来的鱼拿起来,打开鱼的嘴,你就会找到一个大银币。你可以拿去交给他们作你我的殿税。”
27Lakini kusudi tusiwakwaze, nenda ziwani ukatupe ndoana; chukua samaki wa kwanza atakayenaswa, fungua kinywa chake, na ndani utakuta fedha taslimu ya zaka. Ichukue ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako."