聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Matthew

2

1占星家朝拜耶稣
1Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu, mkoani Yudea, wakati Herode alipokuwa mfalme. Punde tu baada ya kuzaliwa kwake, wataalamu wa nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu,
2说:“那生下来作犹太人的王的在哪里?我们看见他的星出现,特来朝拜他。”
2wakauliza, "Yuko wapi mtoto, Mfalme wa Wayahudi, aliyezaliwa? Tumeiona nyota yake ilipotokea mashariki, tukaja kumwabudu."
3希律王听见了就心里不安,全耶路撒冷的居民也是这样。
3Mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, yeye pamoja na wakazi wote wa Yerusalemu.
4他就召集所有的祭司长和民间的经学家,问他们基督应该生在哪里。
4Basi akawaita pamoja makuhani wakuu wote na walimu wa Sheria, akawauliza, "Kristo atazaliwa wapi?"
5他们回答:“在犹太的伯利恒。因为有先知在经上这样说:
5Nao wakamjibu, "Mjini Bethlehemu, mkoani Yudea. Ndivyo nabii alivyoandika:
6‘犹大地的伯利恒啊!你在犹大的领袖中,并不是最小的,因为必有一位领袖从你那里出来,牧养我的子民以色列。’”
6Ewe Bethlehemu katika nchi ya Yuda, kwa vyovyote wewe si mdogo kabisa kati ya viongozi wa Yuda; maana kwako atatokea kiongozi atakayewaongoza watu wangu, Israeli."
7希律暗中把占星家召来,仔细查问他们,那颗星什么时候出现,
7Hapo, Herode aliwaita faraghani hao wataalamu wa nyota, akawauliza wakati hasa ile nyota ilipowatokea.
8然后派他们到伯利恒去,说:“你们去细心寻访那小孩,找到了就向我报告,好叫我也去拜他。”
8Kisha akawatuma Bethlehemu akisema, "Nendeni mkachunguze kwa makini habari za mtoto huyo. Mkisha mpata nileteeni habari ili nami niende nikamwabudu."
9他们听命去了。他们在东方看见的那颗星,忽然在他们前头,领他们到那小孩所在的地方,就在上头停住了。
9Baada ya kumsikiliza mfalme, hao wataalamu wa nyota wakaenda. Kumbe ile nyota waliyokuwa wameiona upande wa mashariki iliwatangulia hata ikaenda kusimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto.
10他们看见那颗星,欢喜极了;
10Walipoiona hiyo nyota, walifurahi mno.
11进了房子,看见小孩和他母亲马利亚,就俯伏拜他,并且打开宝盒,把黄金、乳香、没药作礼物献给他。
11Basi, wakaingia nyumbani, wakamwona yule mtoto pamoja na Maria mama yake; wakapiga magoti, wakamsujudia. Kisha wakafungua hazina zao, wakampa zawadi: dhahabu, ubani na manemane.
12后来他们在梦中得着指示不要回到希律那里去,就从别的路回乡去了。
12Mungu aliwaonya katika ndoto wasimrudie Herode; hivyo wakarudi makwao kwa njia nyingine.
13逃往埃及他们走了以后,主的使者在梦中向约瑟显现,说:“起来,带着孩子和他母亲逃到埃及去,留在那里,直到我再指示你,因为希律要寻找这孩子,把他杀掉。”
13Baada ya wale wageni kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto, akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapokwambia, maana Herode anakusudia kumwua huyu mtoto."
14约瑟就起来,连夜带着孩子和他母亲往埃及去,
14Hivyo, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akaondoka usiku, akaenda Misri.
15住在那里,直到希律死了,为的是要应验主借先知所说的:“我从埃及召我的儿子出来。”
15Akakaa huko mpaka Herode alipokufa. Jambo hilo lilifanyika ili neno alilosema Bwana kwa njia ya nabii litimie: "Nilimwita Mwanangu kutoka Misri."
16屠杀婴孩希律见自己被占星家愚弄了,就大怒,于是照着他从占星家所问得的日子,下令把伯利恒和附近地方,两岁以下的小孩全都杀死。
16Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota walikuwa wamemhadaa, alikasirika sana. Akaamuru watoto wote wa kiume mjini Bethlehemu na kandokando yake wenye umri wa miaka miwili na chini yake wauawe. Alifanya hivyo kufuatana na muda aliopata kujua kutoka kwa wale wataalamu wa nyota.
17这就应验了耶利米先知所说的:
17Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Yeremia:
18“在拉玛听见有声音,是痛哭、极大哀号的声音;拉结为她的儿女哀哭,不肯受安慰,因为他们都不在了。”
18"Sauti imesikika mjini Rama, kilio na maombolezo mengi. Raheli anawalilia watoto wake, wala hataki kutulizwa, maana wote wamefariki."
19从埃及回来希律死后,在埃及,主的使者在梦中向约瑟显现,
19Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri,
20说:“那些要杀害这孩子的人已经死了。起来,带着孩子和他母亲回以色列地去吧。”
20akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa."
21约瑟就起来,带着小孩子和他母亲回到以色列地。
21Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli.
22只是听见亚基老接续他父亲希律作了犹太王,他就不敢到犹太地去;又在梦中得了指示,于是往加利利境去,
22Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya,
23来到拿撒勒城住下,这样就应验了先知所说的:“他必称为拿撒勒人。”
23akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: "Ataitwa Mnazare."