1施洗约翰(可1:3-8;路3:2-17;约1:19-28)
1Siku hizo Yohane Mbatizaji alitokea, akaanza kuhubiri katika jangwa la Yudea:
2说:“天国近了,你们应当悔改。”
2"Tubuni, maana Ufalme wa mbinguni umekaribia."
3以赛亚先知所说:“在旷野有呼喊者的声音:‘预备主的道,修直他的路!’”就是指着这约翰说的。
3Huyu Yohane ndiye yule ambaye nabii Isaya alinena juu yake aliposema: "Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni vijia vyake."
4约翰身穿骆驼毛的衣服,腰束皮带,吃的是蝗虫和野蜜。
4Yohane alivaa vazi lililoshonwa kwa manyoya ya ngamia, na ukanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
5耶路撒冷、犹太全地和约旦河一带的人都出来到他那里去,
5Basi, watu kutoka Yerusalemu, kutoka mkoa wote wa Yudea na sehemu zote za kandokando ya mto Yordani, walimwendea,
6承认自己的罪,在约旦河里受了他的洗。
6wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
7约翰看见许多法利赛人和撒都该人也来受他的洗,就对他们说:“毒蛇所生的啊,谁指示你们逃避那将要来的忿怒呢?
7Lakini alipowaona Mafarisayo wengi na Masadukayo wanamjia ili awabatize, aliwaambia, "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mnaweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
8应当结出果子来,与悔改的心相称。
8Onyesheni basi kwa matendo, kwamba mmetubu kweli.
9你们心里不要以为:‘我们有亚伯拉罕作我们的祖宗。’我告诉你们, 神能从这些石头中给亚伯拉罕兴起后裔来。
9Msidhani kwamba mtaweza kujitetea kwa kusema, Baba yetu ni Abrahamu! Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyafanya mawe haya yawe watoto wa Abrahamu.
10现在斧头已经放在树根上,所有不结好果子的树,就砍下来,丢在火里。
10Basi, shoka liko tayari kuikata mizizi ya miti; hivyo, kila mti usiozaa matunda mazuri, utakatwa na kutupwa motoni.
11我用水给你们施洗,表示你们悔改;但在我以后要来的那一位,能力比我更大,我就是替他提鞋也没有资格。他要用圣灵与火给你们施洗。
11Mimi ninawabatizeni kwa maji kuonyesha kwamba mmetubu. Lakini yule anayekuja baada yangu ana uwezo kuliko mimi. Mimi sistahili hata kubeba viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
12他手里拿着簸箕,要扬净麦场,把麦子收进仓里,却用不灭的火把糠秕烧尽。”
12Yeye anashika mkononi chombo cha kupuria nafaka, ili aipure nafaka yake; akusanye ngano ghalani, na makapi ayachome kwa moto usiozimika."
13耶稣受洗(可1:9-11;路3:21-22)那时,耶稣从加利利来到约旦河约翰那里,要受他的洗。
13Wakati huo Yesu alitoka Galilaya akafika katika mto Yordani, akamwendea Yohane ili abatizwe naye.
14约翰想要阻止他,说:“我应该受你的洗,你却到我这里来吗?”
14Lakini Yohane alijaribu kumzuia akisema, "Je, wewe unakuja kwangu? Mimi hasa ndiye ninayehitaji kubatizwa nawe."
15耶稣回答:“暂且这样作吧。我们理当这样履行全部的义。”于是约翰答应了他。
15Lakini Yesu akamjibu, "Acha tu iwe hivyo kwa sasa, maana kwa namna hii inafaa tuyatekeleze yale yote Mungu anayotaka." Hapo Yohane akakubali.
16耶稣受了洗,立刻从水中上来;忽然,天为他开了,他看见 神的灵,好像鸽子降下来,落在他身上;
16Mara tu Yesu alipokwisha batizwa, alitoka majini; na ghafla mbingu zikafunguka, akaona Roho wa Mungu akishuka kama njiwa na kutua juu yake.
17又有声音从天上来,说:“这是我的爱子,我所喜悦的。”
17Sauti kutoka mbinguni ikasema, "Huyu ndiye Mwanangu mpendwa, nimependezwa naye."