1耶稣受试探(可1:12-13;路4:1-13)
1Kisha Roho alimwongoza Yesu mpaka jangwani ili ajaribiwe na Ibilisi.
2耶稣禁食了四十昼夜,就饿了,
2Akafunga siku arubaini mchana na usiku, na mwishowe akaona njaa.
3试探者前来对他说:“你若是 神的儿子,就吩咐这些石头变成食物吧!”
3Basi, mshawishi akamjia, akamwambia, "Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate."
4耶稣回答:“经上记着:‘人活着,不是单靠食物,更要靠 神口里所出的一切话。’”
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: Binadamu hataishi kwa mikate tu, ila kwa kila neno asemalo Mungu."
5随后,魔鬼带耶稣进了圣城,使他站在殿顶上,
5Kisha Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, mji mtakatifu, akamweka juu ya mnara wa hekalu,
6对他说:“你若是 神的儿子,就跳下去吧!因为经上记着:‘ 神为了你,会吩咐自己的使者用手托住你,免得你的脚碰到石头。’”
6akamwambia, "Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini; maana imeandikwa: Mungu atawaamuru malaika wake kwa ajili yako; watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa kwenye jiwe."
7耶稣对他说:“经上又记着:‘不可试探主你的 神。’”
7Yesu akamwambia, "Imeandikwa pia: Usimjaribu Bwana, Mungu wako."
8最后,魔鬼带耶稣上了一座极高的山,把世界各国和各国的荣华都指给他看。
8Kisha Ibilisi akamchukua mpaka juu ya mlima mrefu, akamwonyesha falme zote za ulimwengu na fahari zake,
9并且对他说:“你只要跪下来拜我,我就把这一切都给你。”
9akamwambia, "Hivi vyote nitakupa kama tu ukipiga magoti na kuniabudu."
10但耶稣说:“撒但,走开!经上记着:‘当拜主你的 神,单要事奉他。’”
10Hapo, Yesu akamwambia, "Nenda zako Shetani! Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia yeye peke yake."
11于是魔鬼离开了耶稣,有天使前来服事他。
11Basi, Ibilisi akamwacha, na malaika wakaja, wakamhudumia.
12耶稣在加利利传道(可1:14-20;路4:14-15,5:1-11,6:17-19;约1:35-42)耶稣听见约翰被捕,就往加利利去。
12Yesu aliposikia kwamba Yohane ametiwa gerezani alikwenda Galilaya.
13他又离开拿撒勒,往西布伦和拿弗他利境内近海的迦百农去,住在那里,
13Aliondoka Nazareti, akaenda Kafarnaumu, mji ulio kando ya bahari ya Genesareti, mpakani mwa wilaya za Zabuloni na Naftali, akakaa huko.
14为了要应验以赛亚先知所说的:
14Ndivyo lilivyotimia lile neno lililosemwa kwa njia ya nabii Isaya:
15“西布伦地、拿弗他利地,沿海之路,约旦河外,外族人的加利利啊!
15"Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kuelekea baharini ng'ambo ya mto Yordani, Galilaya nchi ya watu wa Mataifa!
16住在黑暗中的人民,看见了大光;死亡幽暗之地的居民,有光照亮他们。”
16Watu waliokaa gizani wameona mwanga mkubwa. Nao walioishi katika nchi ya giza na kivuli cha kifo, mwanga umewaangazia!"
17从那时起,耶稣就开始传道,说:“天国近了,你们应当悔改。”
17Tangu wakati huo Yesu alianza kuhubiri akisema, "Tubuni, maana ufalme wa mbinguni umekaribia!"
18耶稣在加利利海边行走的时候,看见兄弟二人,就是名叫彼得的西门和他的弟弟安得烈,正在把网撒到海里去;他们是渔夫。
18Yesu alipokuwa anatembea kando ya ziwa Galilaya, aliwaona ndugu wawili wavuvi; Simoni (aitwae Petro) na Andrea, ndugu yake; walikuwa wakivua samaki kwa nyavu ziwani.
19耶稣就对他们说:“来跟从我,我要使你们作得人的渔夫。”
19Basi, akawaambia, "Nifuateni, nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
20他们立刻撇下网,跟从了他。
20Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
21耶稣又往前走,看见另一对兄弟,就是西庇太的儿子雅各和约翰,正和父亲西庇太在船上整理鱼网,他就呼召他们。
21Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona ndugu wengine wawili: Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Hao walikuwa ndani ya mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Basi Yesu akawaita,
22他们立刻离了船,别了父亲,跟从了耶稣。
22nao mara wakaiacha mashua pamoja na baba yao, wakamfuata.
23耶稣走遍加利利,在各会堂里教导人,宣扬天国的福音,医治民间各种疾病、各种病症。
23Yesu alikuwa anakwenda kila mahali wilayani Galilaya, akifundisha katika masunagogi na kuhubiri Habari Njema juu ya ufalme wa Mungu. Aliponya kila namna ya maradhi na magonjwa waliyokuwa nayo watu.
24他的名声传遍了叙利亚全地,人们就把一切患病的,就是患各种疾病、疼痛、鬼附、癫痫、瘫痪的,都带到他面前,他就医好他们。
24Habari zake zikaenea katika mkoa wote wa Siria. Wagonjwa wote wenye maradhi ya kila namna na wale waliosumbuliwa na kila namna ya taabu: waliopagawa na pepo, wenye kifafa na watu waliokuwa wamelemaa, walipelekwa kwake; naye akawaponya wote.
25于是有许多人从加利利、低加波利、耶路撒冷、犹太和约旦河东来跟从耶稣。
25Makundi mengi ya watu kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Yudea na ng'ambo ya mto Yordani, walimfuata.