1耶稣复活(可16:1-10;路24:1-12;约20:1-10)
1Baada ya Sabato, karibu na mapambazuko ya siku ile ya Jumapili, Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikwenda kutazama lile kaburi.
2忽然,地震得很厉害;主的使者从天上下来,把石头辊开,坐在上面。
2Ghafla kutatokea tetemeko kubwa la nchi; malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akalivingirisha lile jiwe, akalikalia.
3他的样子好像闪电,衣服洁白如雪。
3Alionekana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.
4看守的人因为害怕他,就浑身战抖,好像死了一样。
4Walinzi wa lile kaburi wakatetemeka kwa hofu kubwa, hata wakawa kama wamekufa.
5那使者对妇女们说:“你们不要怕,我知道你们在找被钉十字架的耶稣。
5Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, "Ninyi msiogope! Najua kwamba mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa.
6他不在这里,已经照他所说的复活了。你们来看安放他的地方吧。
6Hayupo hapa maana amefufuka kama alivyosema. Njoni mkaone mahali alipokuwa amelala.
7快去告诉他的门徒:‘他已经从死人中复活了。他会比你们先到加利利去,你们在那里必看见他。’现在我已经告诉你们了。”
7Basi, nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba amefufuka kutoka wafu, na sasa anawatangulieni kule Galilaya; huko mtamwona. Haya, mimi nimekwisha waambieni."
8她们立刻离开坟墓,又害怕,又十分欢喜,跑去告诉耶稣的门徒。
8Wakiwa wenye hofu na furaha kubwa, hao wanawake walitoka upesi kaburini, wakakimbia kwenda kuwaambia wanafunzi wake.
9忽然,耶稣向她们迎面而来,说:“你们好。”她们就上前,抱住他的脚拜他。
9Mara, Yesu akakutana nao, akawasalimu: "Salamu." Hao wanawake wakamwendea, wakapiga magoti mbele yake, wakashika miguu yake.
10耶稣对她们说:“不要怕,去告诉我的弟兄,叫他们到加利利去,他们在那里必看见我。”
10Kisha Yesu akawaambia, "Msiogope! Nendeni mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, na huko wataniona."
11卫兵受贿造谣她们去的时候,有些卫兵进了城,把一切所发生的事向祭司长报告。
11Wale wanawake walipokuwa wanakwenda zao, baadhi ya walinzi wa lile kaburi walikwenda mjini kutoa taarifa kwa makuhani wakuu juu ya mambo yote yaliyotukia.
12祭司长就和长老聚集在一起商量,然后拿许多钱给士兵,
12Basi, wakakutana pamoja na wazee, na baada ya kushauriana, wakawapa wale askari kiasi kikubwa cha fedha
13说:“你们要这样说:‘他的门徒晚上来了,趁我们睡着的时候,把他偷走了。’
13wakisema, "Ninyi mtasema hivi: Wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba sisi tukiwa tumelala.
14如果总督知道了这件事,我们会说服他,不会牵连你们。”
14Na kama mkuu wa mkoa akijua jambo hili, sisi tutasema naye na kuhakikisha kuwa ninyi hamtapata matatizo."
15士兵收了钱,就照着祭司长和长老的指使去作。这种说法直到今日还流传在犹太人当中。
15Wale walinzi wakazichukua zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Habari hiyo imeenea kati ya Wayahudi mpaka leo.
16主交给门徒的使命(可16:14-18;路24:36-49;约20:19-23。参徒1:6-8)十一个门徒往加利利去,到了耶稣指定的山上。
16Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya kwenye ule mlima aliowaagiza Yesu.
17他们看见耶稣就拜他,但仍然有些人怀疑。
17Walipomwona, wakamwabudu, ingawa wengine walikuwa na mashaka.
18耶稣上前来,对他们说:“天上地上一切权柄都赐给我了。
18Yesu akaja karibu, akawaambia, "Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
19所以,你们要去使万民作我的门徒,奉父子圣灵的名,给他们施洗(“奉父子圣灵的名,给他们施洗”或译:“给他们施洗,归入父子圣灵的名”),
19Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu; mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
20我吩咐你们的一切,都要教导他们遵守。这样,我就常常与你们同在,直到这世代的终结。”
20Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwisho wa nyakati."