1耶稣被押交彼拉多(可15:1;路23:1;约18:28)
1Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
2他们把他绑起来,押去交给总督彼拉多。
2Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
3犹大的结局(参徒1:18-19)那时,出卖耶稣的犹大见耶稣定了罪,就后悔了。他把那三十块银子还给祭司长和长老,说:
3Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
4“我有罪了!我出卖了无辜的人(“人”原文作“血”)!”他们说:“这是你的事,跟我们有什么关系?”
4Akawaambia, "Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe." Lakini wao wakasema, "Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako."
5犹大把银子丢进圣所,然后离开,出去吊死了。
5Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
6祭司长把银子拾起来,说:“这是血钱,不可放在殿库里。”
6Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, "Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu."
7他们商议之后,就用那些钱买了“陶匠的田”,用来作外国人的坟地。
7Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
8所以那田称为“血田”,直到今日。
8Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
9这应验了耶利米先知所说的:“他们拿了三十块银子,就是以色列人给他估定的价钱,
9Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: "Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
10用它买了‘陶匠的田’,正如主所指示我的。”
10wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza."
11彼拉多判耶稣钉十字架(可15:2-15;路23:2、3、18-25;约18:29-19:16)耶稣站在总督面前,总督问他:“你是犹太人的王吗?”耶稣回答:“这是你说的。”
11Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, "Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamwambia, "Wewe umesema."
12祭司长和长老控告他的时候,他却不回答。
12Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
13彼拉多又问他:“他们作证指控你这么多的事,你没有听见吗?”
13Hivyo Pilato akamwuliza, "Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?"
14耶稣一句话也不回答他,令总督非常惊奇。
14Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
15每逢这节期,总督有一个惯例,就是给群众释放一个他们要求释放的囚犯。
15Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
16那时,有个声名狼籍的囚犯,名叫耶数.巴拉巴。
16Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
17群众聚集的时候,彼拉多问他们:“你们要我给你们释放谁?耶数.巴拉巴或是称为基督的耶稣呢?”
17Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, "Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?"
18他知道他们是因为嫉妒才把耶稣交了来。
18Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
19彼拉多坐在审判台上的时候,他的夫人派人来说:“你不要干涉这个义人的事,因为昨夜我在梦中因他受了很多的苦。”
19Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: "Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake."
20祭司长和长老怂恿群众,叫他们去要求释放巴拉巴,除掉耶稣。
20Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
21总督问他们:“这两个人,你们要我给你们释放哪一个?”他们说:“巴拉巴!”
21Mkuu wa mkoa akawauliza, "Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?" Wakamjibu, "Baraba!"
22彼拉多对他们说:“那么,我怎样处置那称为基督的耶稣呢?”他们齐声说:“把他钉十字架!”
22Pilato akawauliza, "Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?" Wote wakasema, "Asulubiwe!"
23彼拉多说:“他作了什么恶事呢?”众人更加大声喊叫:“把他钉十字架!”
23Pilato akauliza, "Kwa nini? Amefanya kosa gani?" Wao wakazidi kupaaza sauti: "Asulubiwe!"
24彼拉多见无济于事,反会引起骚动,就拿水在群众面前洗手,说:“流这人的血,与我无关,你们自己负责吧。”
24Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, "Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe."
25群众回答:“流他的血的责任,归在我们和我们子孙的身上吧。”
25Watu wote wakasema, "Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!"
26于是彼拉多给他们释放了巴拉巴;他把耶稣鞭打了,就交给他们钉十字架。
26Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
27士兵戏弄耶稣(可15:16-20;约19:2-3)总督的士兵把耶稣带到总督府,召集全队士兵到他面前。
27Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
28他们脱去他的衣服,给他披上朱红色的外袍,
28Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
29又用荆棘编成冠冕,戴在他的头上,把一根芦苇放在他的右手,跪在他面前讥笑他说:“犹太人的王万岁!”
29Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, "Shikamoo mfalme wa Wayahudi!"
30然后向他吐唾沫,又拿起芦苇打他的头。
30Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
31戏弄完了,就脱下他的外袍,给他穿回衣服,带去钉十字架。
31Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
32耶稣被钉十字架(可15:22-32;路23:33-43;约19:17-24)他们出来的时候,遇见一个古利奈人,名叫西门,就强迫他背耶稣的十字架。
32Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
33到了一个地方,名叫各各他,就是“髑髅地”的意思,
33Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la kichwa,"
34他们把苦胆调和的酒给他喝,他尝了却不肯喝。
34wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
35士兵把他钉了十字架,就抽签分他的衣服,
35Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
36然后坐在那里看守他。
36Wakaketi, wakawa wanamchunga.
37他们在耶稣的头以上,钉了一块牌子,写着他的罪状:“这是犹太人的王耶稣”。
37Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, "Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi."
38当时,有两个强盗和他一同钉十字架,一个在右,一个在左。
38Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
39过路的人嘲笑他,摇着头说:
39Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
40“你这个想拆毁圣所,三日之内又把它建造起来的,救救自己吧!如果你是 神的儿子,从十字架上下来吧!”
40"Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!"
41祭司长、经学家和长老也同样讥笑他,说:
41Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
42“他救了别人,却不能救自己。如果他是以色列的王,现在可以从十字架上下来,我们就信他。
42"Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
43他信靠 神;如果 神喜悦他,就让 神现在救他吧,因为他说自己是 神的儿子。”
43Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka."
44和他一同钉十字架的强盗也都这样侮辱他。
44Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
45耶稣死时的情形(可15:33-41;路23:44-49;约19:28-30)从正午到下午三点钟,遍地都黑暗了。
45Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
46大约三点钟,耶稣大声呼叫:“以利,以利,拉马撒巴各大尼?”意思是“我的 神,我的 神,你为什么离弃我?”
46Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eli, Eli, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
47有几个站在那里的人,听见了就说:“这个人在呼叫以利亚呢。”
47Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, "Anamwita Eliya."
48有一个人马上跑去拿海绵蘸满了酸酒,用芦苇递给他喝。
48Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
49但其他的人说:“等一等,我们看看以利亚来不来救他。”
49Wengine wakasema, "Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa."
50耶稣再大声呼叫,气就断了。
50Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
51忽然,圣所里的幔子从上到下裂成两半;地面震动,石头崩裂;
51Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52而且坟墓开了,许多睡了的圣徒的身体也复活了,
52makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
53从坟墓里出来;到了耶稣复活之后,他们进到圣城向许多人显现。
53nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
54百夫长和跟他一起看守耶稣的士兵,看见了地震和所发生的事情,就十分惧怕,说:“这个人真是 神的儿子。”
54Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, "Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu."
55有许多妇女在那里远远地观看;她们是从加利利开始跟随耶稣服事他的。
55Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
56她们中间有抹大拉的马利亚、雅各和约西的母亲马利亚,以及西庇太的儿子的母亲。
56Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
57耶稣葬在新坟墓里(可15:42-47;路23:50-56;约19:38-42)到了晚上,有一个亚利马太的富翁来到,他名叫约瑟,是耶稣的门徒。
57Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58这个人去见彼拉多,请求领取耶稣的身体,彼拉多就吩咐给他。
58Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
59约瑟领了耶稣的身体,用干净的细麻布裹好,
59Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
60放在自己的新坟墓里,就是在磐石里凿出来的。他辊了一块大石头来挡住墓门,然后才离开。
60akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
61抹大拉的马利亚和另一个马利亚都在那里,对着坟墓坐着。
61Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
62卫兵严密看守坟墓第二天,就是过了“预备日”的那一天,祭司长和法利赛人去见彼拉多,说:
62Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
63“大人,我们想起那个骗子,生前说过:‘三天之后,我要复活。’
63Wakasema, "Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
64所以请你下令把坟墓严密看守,直到第三天,免得他的门徒来把他偷去,然后对民众说:‘他从死人中复活了。’这样,日后的骗局比起初的就更大了。”
64Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali."
65彼拉多对他们说:“你们带着卫兵,尽你们所能的去严密看守吧。”
65Pilato akawaambia, "Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo."
66他们就去把墓前的石封好,又派卫兵把守,严密地守住坟墓。
66Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.