聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Matthew

26

1商议怎样杀害耶稣(可14:1-2;路22:1-2)
1Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
2“你们知道两天之后就是逾越节,人子将要被交给人,钉在十字架上。”
2"Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe."
3那时,祭司长和民间的长老聚集在大祭司该亚法的官邸,
3Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
4商议怎样用诡计逮捕耶稣,把他杀害。
4Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
5不过他们说:“不可在节期下手,免得引起民众暴动。”
5Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
6有女人用香膏膏主(可14:3-9;约12:1-8)耶稣在伯大尼,在患痲风的西门家里的时候,
6Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
7有一个女人拿着一瓶珍贵的香膏,前来把它浇在耶稣的头上。
7mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
8门徒看见了,就很生气,说:“为什么这样浪费呢?
8Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, "Ya nini hasara hii?
9这香膏可以卖很多钱,赒济穷人。”
9Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha."
10耶稣知道了,就说:“为什么难为这个女人呢?她为我作了一件美事。
10Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
11你们常常有穷人跟你们在一起,然而却不常有我。
11Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
12她把这香膏浇在我身上,是为了安葬我而作的。
12Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
13我实在告诉你们,这福音无论传到世界上什么地方,这女人所作的都要传讲,来记念她。”
13Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye."
14犹大出卖耶稣(可14:10-11;路22:3-6)那时,十二门徒中的一个,就是加略人犹大,去见祭司长,说:
14Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
15“如果我把他交给你们,你们愿意给我什么呢?”他们就给了他三十块银子。
15akawaambia, "Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?" Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
16从那时起,他就找机会把耶稣交给他们。
16na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
17最后的晚餐(可14:12-26;路22:7-23;约13:21-30)除酵节的第一天,门徒前来问耶稣:“你要我们在哪里为你预备逾越节的晚餐呢?”
17Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, "Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?"
18他说:“你们到城里去见某人,对他说,老师说:‘我的时候快到了;我要到你那里和我的门徒守逾越节。’”
18Yeye akawajibu, "Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu."
19门徒照耶稣的指示去作,预备好了逾越节的晚餐。
19Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
20到了晚上,耶稣和十二门徒一同吃晚餐。
20Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
21他们吃的时候,耶稣说:“我实在告诉你们,你们中间有一个人要出卖我。”
21Walipokuwa wakila, Yesu akasema, "Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti."
22他们就很忧愁,一个一个地问他:“主啊,是我吗?”
22Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, "Bwana! Je, ni mimi?"
23他回答:“那和我一同把手蘸在盘子里的人,他要出卖我。
23Yesu akajibu, "Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
24正如经上指着人子所说的,他固然要离世,但出卖人子的那人有祸了!他没有生下来倒好。”
24Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa."
25那出卖耶稣的犹大说:“拉比,是我吗?”他说:“这是你说的。”
25Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, "Mwalimu! Je, ni mimi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
26他们吃的时候,耶稣拿起饼来,祝谢了就擘开,递给门徒,说:“你们拿去吃吧,这是我的身体。”
26Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, "Twaeni mle; huu ni mwili wangu."
27耶稣又拿起杯来,祝谢了就递给他们,说:“你们都喝吧,
27Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, "Nyweni nyote;
28这是我的血,是为立约的,为许多人流出来,使罪得赦。
28maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
29我告诉你们,从今以后我必不再喝这葡萄酒,直到我和你们在我父的国里喝新酒的那一天。”
29Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu."
30他们唱完了诗,就出来往橄榄山去。
30Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
31预言彼得不认主(可14:27-31;路22:31-34;约13:36-38)那时,耶稣对他们说:“今天晚上,你们因我的缘故都要后退,因为经上记着:‘我要击打牧人,羊群就分散了。’
31Kisha Yesu akawaambia, "Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
32我复活以后,要比你们先到加利利去。”
32Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya."
33彼得对他说:“就算所有的人都因你的缘故后退,我却永不后退。”
33Petro akamwambia Yesu "Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe."
34耶稣对他说:“我实在告诉你,今天晚上鸡叫以前,你会三次不认我。”
34Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
35彼得对他说:“就算必须与你一同死,我也决不会不认你。”门徒也都这样说。
35Petro akamwambia, "Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe." Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36在客西马尼祷告(可14:32-42;路22:39-46)耶稣和门徒来到一个地方,名叫客西马尼,就对门徒说:“你们坐在这里,我要到那边去祷告。”
36Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, "Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali."
37他带了彼得和西庇太的两个儿子一起去,心里忧愁难过,
37Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
38对他们说:“我的心灵痛苦得快要死了;你们留在这里,与我一同警醒吧。”
38Hapo akawaambia, "Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami."
39他稍往前走,把脸俯伏在地上,祷告说:“我的父啊!可能的话,求你使这杯离开我;但不要照我的意思,只要照你的旨意。”
39Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: "Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe."
40耶稣回到门徒那里,看见他们都睡着了,就对彼得说:“你们连一个小时也不能同我警醒吗?
40Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, "Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
41应当警醒、祷告,免得陷入试探;你们心灵虽然愿意,肉体却是软弱的。”
41Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu."
42他又再次走开,祷告说:“我的父啊!如果这杯不能离开我,一定要我喝,就愿你的旨意成全。”
42Akaenda tena mara ya pili akasali: "Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike."
43他再回来的时候,看见门徒睡着了,因为他们十分疲倦。
43Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
44他又离开他们,第三次去祷告,说的也是同样的话。
44Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
45然后,他回到门徒那里,对他们说:“你们还在睡觉休息吗?看哪,时候到了,人子要被交在罪人的手里了。
45Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, "Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
46起来,我们走吧!出卖我的人来了。”
46Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti."
47耶稣被捕(可14:43-50;路22:47-53;约18:3-11)耶稣还在说话的时候,十二门徒中的犹大,带着一大群拿着刀棒的人来到,他们是祭司长和民间的长老派来的。
47Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
48出卖耶稣的人给他们一个暗号,说:“我跟谁亲嘴,谁就是他;你们可以抓住他。”
48Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: "Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni."
49他立刻前来对耶稣说:“拉比,你好。”跟着就与他亲嘴。
49Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, "Shikamoo, Mwalimu!" Kisha akambusu.
50耶稣对他说:“朋友,你来要作的事,快作吧!”于是那些人上前来,动手拿住耶稣,逮捕了他。
50Yesu akamwambia, "Rafiki, fanya ulichokuja kufanya." Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
51有一个与耶稣在一起的人,伸手拔出刀来,砍了大祭司的仆人一刀,削掉他的一只耳朵。
51Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52耶稣对他说:“把你的刀收回原处!凡动刀的必死在刀下。
52Hapo Yesu akamwambia, "Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
53你以为我不能求我的父,他就马上给我派十二营以上的天使下来吗?
53Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54如果这样,经上预言这事必须发生,怎能应验呢?”
54Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?"
55那时,耶稣对众人说:“你们带着刀棒出来,把我当作强盗捉拿吗?我天天坐在殿里教导人,你们却没有逮捕我。
55Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, "Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
56但这整件事的发生,是要应验先知书上的话。”那时,门徒都离开他逃跑了。
56Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie." Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
57大祭司审问耶稣(可14:53-65;路22:54、66-71;约18:12-13、19-24)那些逮捕了耶稣的人,把他押去见大祭司该亚法。那时经学家和长老已经聚集在那里了。
57Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
58彼得远远地跟着耶稣,直到大祭司的官邸。他进到里面,和差役坐在一起,要看事情怎样了结。
58Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
59祭司长和公议会全体都想找假证供来控告耶稣,好把他处死;
59Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
60虽然有许多人前来作假证供,却找不着证据。最后有两个人前来说:
60lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
61“这人说过:‘我可以拆毁 神的圣所,三日之内又把它建造起来。’”
61wakasema, "Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu."
62大祭司就站起来,对耶稣说:“你为什么不回答?这些人作证,控告你的是什么呢?”
62Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, "Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?"
63耶稣却不作声。大祭司又对他说:“我指着永生的 神要你起誓,告诉我们你是不是基督、 神的儿子。”
63Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, "Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!"
64耶稣回答:“这是你说的;但我告诉你们:从今以后,你们要看见人子,坐在权能者的右边,驾着天上的云降临。”
64Yesu akamwambia, "Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni."
65大祭司就撕开衣服,说:“他说了亵渎的话,我们还要什么证人呢?你们现在听见了这亵渎的话,
65Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, "Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
66认为怎样呢?”他们回答:“他是该死的。”
66Ninyi mwaonaje?" Wao wakamjibu, "Anastahili kufa!"
67于是他们吐唾沫在他的脸上,用拳头打他,也有人用掌掴他,说:
67Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
68“基督啊,向我们说预言吧!是谁打你呢?”
68wakasema, "Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!"
69彼得三次不认主(可14:66-72;路22:55-62;约18:16-18、25-27)彼得坐在外面的院子里,有一个婢女走过来对他说:“你也是和加利利人耶稣一伙的。”
69Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, "Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya."
70彼得却当众否认,说:“我不知道你说什么。”
70Petro akakana mbele ya wote akisema, "Sijui hata unasema nini."
71他出到门口,又有一个婢女看见他,就对那里的人说:“这人是和拿撒勒人耶稣一伙的。”
71Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, "Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti."
72彼得再次否认,并且发誓说:“我不认识那个人。”
72Petro akakana tena kwa kiapo: "Simjui mtu huyo."
73过了一会,站在那里的人前来对他说:“你的确是他们中间的一个,因为一听你的口音就认出来了。”
73Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, "Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha."
74彼得就发咒起誓说:“我不认识那一个人。”立刻鸡就叫了。
74Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, "Simjui mtu huyo!" Mara jogoo akawika.
75彼得想起耶稣所说的话:“鸡叫以前,你会三次不认我”,他就出去痛哭。
75Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: "Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu." Basi, akatoka nje akalia sana.