聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Matthew

25

1十个童女的比喻
1"Wakati huo, Ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.
2她们中间有五个是愚蠢的,五个是聪明的。
2Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
3那些愚蠢的拿着灯,却没有带油;
3Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.
4但那些聪明的拿着灯,也把油装在瓶里带来。
4Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.
5新郎很晚还没有到,她们都打瞌睡,而且睡着了。
5Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wanawali wote wote walisinzia, wakalala.
6半夜,有人喊叫:‘新郎来了,快出来迎接他。’
6Usiku wa manane kukawa na kelele: Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.
7那些童女都醒过来,整理她们的灯。
7Hapo wale wanawali wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.
8愚蠢的对聪明的说:‘请把你们的油分一点给我们,我们的灯快要灭了。’
8Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.
9聪明的回答:‘这些恐怕不够我们大家用,不如你们自己到卖油的地方去买吧!’
9Lakini wale wenye busara wakawaambia, Hayatatutosha sisi na ninyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!
10她们去买油的时候,新郎来了;准备好了的童女就和他一同进去参加婚筵,门就关上了。
10Basi, wale wanawali wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la arusi, kisha mlango ukafungwa.
11后来,其余的童女也来到,说:‘主啊,主啊,给我们开门吧!’
11Baadaye wale wanawali wengine wakaja, wakaita: Bwana, bwana, tufungulie!
12新郎却回答:‘我实在告诉你们,我不认识你们。’
12Lakini yeye akawajibu, Nawaambieni kweli, siwajui ninyi."
13所以你们要警醒,因为不知道那日子和那时间。
13Kisha Yesu akasema, "Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14三个仆人的比喻(路19:12-27)“天国又像一个人要出外远行,就叫自己的仆人来,把产业交给他们。
14"Itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ng'ambo: aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15他按照各人的才干,一个给三万个银币,一个给一万二千个银币,一个给六千个银币(原文作“五个,二个,一个他连得”;一个他连得等于六千个银币),然后就远行去了。
15Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.
16那领了三万的马上去做生意,另外赚了三万。
16Mara yule aliyekabidhiwa talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.
17那领了一万二千的也是这样,另赚了一万二千。
17Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.
18但那领了六千的,却去把地挖开,把主人的钱藏起来。
18Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaenda akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.
19过了很久,那些仆人的主人回来了,要和他们算帐。
19"Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi, akaanza kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.
20那领了三万个银币的,带着另外的三万前来,说:‘主啊,你交了三万给我,你看,我又赚了三万。’
20Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano akaja amechukua zile talanta tano faida, akamwambia, Bwana, ulinikabidhi talanta tano, hapa pana talanta tano zaidi faida niliyopata.
21主人对他说:‘又良善又忠心的仆人哪,你作得好!你既然在不多的事上忠心,我要派你管理许多的事。进来,享受你主人的快乐吧!’
21Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
22那领了一万二千的也前来,说:‘主啊,你交了一万二千给我,你看,我又赚了一万二千。’
22"Mtumishi aliyekabidhiwa talanta mbili akaja, akatoa talanta mbili faida, akisema, Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Chukua talanta mbili zaidi faida niliyopata.
23主人对他说:‘又良善又忠心的仆人哪,你作得好!你既然在不多的事上忠心,我要派你管理许多的事。进来,享受你主人的快乐吧!’
23Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo, nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
24那领了六千的也前来,说:‘主啊,我知道你是个严厉的人,没有撒种的地方,你要收割;没有散播的地方,你要收聚。
24"Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaja, akasema, Bwana, najua wewe ni mtu mgumu; wewe huvuna pale ambapo hukupanda, na kukusanya pale ambapo hukutawanya.
25所以,我就害怕起来,去把你的钱藏在地里。你看,你的钱还在这里。’
25Niliogopa, nikaificha fedha yako katika ardhi. Chukua basi mali yako.
26可是主人对他说:‘你这个又可恶又懒惰的仆人,你既然知道我要在没有撒种的地方收割,在没有散播的地方收聚,
26"Bwana wake akamwambia, Wewe ni mtumishi mwovu na mvivu! Unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikupanda, na hukusanya pale ambapo sikutawanya.
27那你就应该把我的钱存入银行,到我回来的时候,可以连本带利收回。
27Ilikupasa basi, kuiweka fedha yangu katika benki, nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake!
28你们把他的六千银币拿去,交给那个有六万的。
28Basi, mnyang'anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.
29因为凡是有的,还要给他,他就充足有余;凡是没有的,就算他有什么也要拿去。
29Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
30把这没有用的仆人丢在外面的黑暗里,在那里必要哀哭切齿。’
30Na kuhusu huyu mtumishi asiye na faida, mtupeni nje gizani! Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.
31人子必审判万族“当人子在他的荣耀里,带着所有的使者降临的时候,他要坐在荣耀的宝座上。
31"Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye, hapo ataketi juu ya kiti chake cha enzi kitukufu,
32万族要聚集在他面前,他要把他们彼此分开,好像牧羊人把绵羊和山羊分开一样:
32na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.
33把绵羊放在右边,山羊放在左边。
33Atawaweka kondoo upande wake wa kulia na mbuzi upande wake wa kushoto.
34那时,王要对右边的说:‘蒙我父赐福的,来承受创世以来为你们预备好的国吧。
34"Kisha Mfalme atawaambia wale walio upande wake wa kulia, Njoni enyi mliobarikiwa na Baba yangu; pokeeni Ufalme mliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
35因为我饿了,你们给我吃;我渴了,你们给我喝;我作旅客,你们接待我;
35Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;
36我赤身露体,你们给我衣服穿;我病了,你们看顾我;我在监里,你们来看我。’
36nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.
37义人就回答:‘主啊,我们什么时候见你饿了就给你吃,渴了就给你喝呢?
37Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme Bwana, ni lini tulikuona mwenye njaa nasi tukakupa chakula, au ukiwa na kiu nasi tukakunywesha maji?
38又什么时候见你作旅客就接待你,赤身露体就给你衣服穿呢?
38Ni lini tulikuona ukiwa mgeni nasi tukakukaribisha, au bila nguo nasi tukakuvika?
39或者什么时候见你病了,或在监里就来看你呢?’
39Ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au mfungwa nasi tukaja kukutazama?
40王要回答他们:‘我实在告诉你们,你们所作的,只要是作在我一个最小的弟兄身上,就是作在我的身上了。’
40Mfalme atawajibu, Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.
41“王也要对左边的说:‘你们这被咒诅的,离开我,到为魔鬼和他的使者所预备的永火里去吧!
41"Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake.
42因为我饿了,你们没有给我吃;我渴了,你们没有给我喝;
42Maana nilikuwa na njaa nanyi hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji.
43我作旅客,你们没有接待我;我赤身露体,你们没有给我衣服穿;我病了,我在监里,你们没有看顾我。’
43Nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha; nilikuwa mgonjwa na mfungwa nanyi hamkuja kunitazama.
44他们就回答:‘主啊,我们什么时候见你饿了、渴了、作旅客、赤身露体、病了,或在监里,却没有服事你呢?’
44"Hapo nao watajibu, Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukuja kukuhudumia?
45王要回答他们:‘我实在告诉你们,这些事你们既然没有作在一个最小的身上,就是没有作在我的身上了。’
45Naye atawajibu, Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi.
46他们要进入永远的刑罚,义人却要进入永生。”
46Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele."