1耶稣基督的启示
1Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
2约翰把 神的道,和耶稣基督的见证,凡是自己所看见的,都见证出来了。
2naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
3读这书上预言的人,和那些听见这预言并且遵守书中记载的人,都是有福的!因为时候近了。
3Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
4问候七教会约翰写信给在亚西亚的七个教会。愿恩惠平安,从那位今在、昔在、以后永在的 神,从他宝座前的七灵,
4Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
5又从那信实的见证人、死人中首先复生的、地上众君王的统治者耶稣基督临到你们。他爱我们,用自己的血把我们从我们的罪中释放出来,
5na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
6又使我们成为国度,作他父 神的祭司。愿荣耀权能都归给他,直到永永远远。阿们。
6akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina.
7看哪,他驾着云降临,每一个人都要看见他,连那些刺过他的人也要看见他,地上的万族都要因他捶胸。这是必定的,阿们。
7Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
8主 神说:“我是阿拉法,我是俄梅格;我是今在、昔在、以后永在,全能的 神。”
8"Mimi ni Alfa na Omega," asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
9基督向约翰显现我约翰,就是你们的弟兄,在耶稣里跟你们一同分享患难、国度和忍耐的,为了 神的道和耶稣的见证,曾经在那名叫拔摩的海岛上。
9Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
10有一个主日,我在灵里,听见在我后边有一个大声音,好像号筒的响声,
10Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
11说:“你所看见的,要写在书上,也要寄给以弗所、士每拿、别迦摩、推雅推拉、撒狄、非拉铁非、老底嘉七个教会。”
11Nayo ilisema, "Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea."
12我转过身来要看看那跟我说话的声音是谁发的;一转过来,就看见七个金灯台。
12Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
13灯台中间有一位好像人子的,身上穿着直垂到脚的长衣,胸间束着金带。
13na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
14他的头和头发像白羊毛、像雪一样洁白,他的眼睛好像火焰,
14Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
15他的两脚好像在炉中精炼过的发光的铜,他的声音好像众水的声音。
15miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
16他的右手拿着七星,有一把两刃的利剑从他口中吐出来;他的脸发光好像正午的烈日。
16Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
17我看见了他,就仆倒在他脚前,像死了一样。他用右手按着我,说:“不要怕!我是首先的,我是末后的,
17Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, "Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
18又是永活的;我曾经死过,看哪,现在又活着,直活到永永远远,并且拿着死亡和阴间的钥匙。
18Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu.
19所以,你要把所看见的,现在的,和今后将要发生的事都写下来。
19Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
20你所看见在我右手中的七星和七个金灯台的奥秘就是这样:七星是七个教会的使者,七灯台是七个教会。”
20Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.