1问安
1Kutoka kwangu mimi Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, na mtume niliyeteuliwa na kuitwa kwa ajili ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu.
2这福音是 神借着众先知在圣经上预先所应许的,
2Hapo kale, Mungu aliwaahidia watu hii Habari Njema kwa njia ya manabii wake katika Maandiko Matakatifu.
3就是论到他的儿子我们的主耶稣基督:按肉身说,他是从大卫的后裔生的;
3Hii Habari Njema inamhusu Mwana wa Mungu, Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye mintarafu ubinadamu wake, alikuwa mzawa wa Daudi;
4按圣洁的灵说,因为从死人中复活,显明他是大有能力的、 神的儿子(“显明他是大有能力的、 神的儿子”或译:“以大能显明他是 神的儿子”)。
4mintarafu utakatifu wake wa kimungu, alithibitishwa kwa uwezo mkuu kwamba ni Mwana wa Mungu kwa kufufuliwa kutoka wafu.
5我们从他领受了恩典和使徒的职分,在万族中使人因他的名相信而顺服,
5Kwa njia yake, mimi nimepewa neema ya kuwa mtume, ili kwa ajili yake niwaongoze watu wa mataifa yote wapate kuamini na kutii.
6其中也有你们这蒙耶稣基督所召的人。
6Ninyi ni miongoni mwa watu hao; mmeitwa muwe watu wake Yesu Kristo.
7我写信给各位住在罗马,为 神所爱,蒙召作圣徒的人。愿恩惠平安从我们的父 神和主耶稣基督临到你们。
7Basi, ninawaandikia ninyi nyote mlioko Roma ambao Mungu anawapenda, akawateua muwe watu wake. Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
8保罗渴想到罗马去首先,我靠着耶稣基督,为你们大家感谢我的 神,因为你们的信心传遍天下。
8Awali ya yote, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inasikika duniani kote.
9我在传扬他儿子福音的事上,用心灵事奉的 神,可以作证我是怎样不断地记念你们,
9Mungu, ambaye ninamtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Habari Njema ya Mwanae, ni shahidi wangu kwamba ninawakumbukeni
10常常在祷告中恳切祈求,也许我可以照着他的旨意,终于能够顺利地到你们那里去。
10daima katika sala zangu. Namwomba Mungu akipenda, anipatie nafasi nzuri ya kuja kwenu sasa.
11因为我很想见你们,好把一些属灵的恩赐分给你们,使你们可以坚定;
11Kwa maana ninatamani sana kuwaoneni ili nipate kuwagawieni zawadi ya kiroho na kuwaimarisha.
12也使我在你们中间,借着你我彼此的信心,大家一同得到安慰。
12Ndiyo kusema, tutaimarishana: imani yenu itaniimarisha mimi, na yangu itawaimarisha ninyi.
13弟兄们,我不愿意你们不知道,我好几次预先定好了要到你们那里去,为了要在你们中间也得一些果子,像在其他的民族中间一样,可是直到现在还有阻碍。
13Ndugu zangu, nataka mjue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembeleeni, lakini mpaka sasa nimezuiwa. Ningependa kupata mafanikio mema kati yenu kama nilivyopata kati ya watu wa mataifa mengine.
14无论是希腊人或是未开化的人,聪明的人或是愚笨的人,我都欠他们的债。
14Ninalo jukumu kwa watu wote, waliostaarabika na wasiostaarabika, wenye elimu na wasio na elimu.
15所以,对我来说,我随时都愿意把福音也传给你们在罗马的人。
15Ndiyo maana ninatamani pia kuihubiri Habari Njema kwenu ninyi mlioko huko Roma.
16福音是 神的大能我不以福音为耻;这福音是 神的大能,要救所有相信的,先是犹太人,后是希腊人。
16Sioni aibu kutangaza Habari Njema; yenyewe ni nguvu ya Mungu inayowaokoa wote wanaoamini: Wayahudi kwanza, na wasio Wayahudi pia.
17 神的义就是借着这福音显明出来,本于信而归于信,正如经上所记:“义人必因信得生。”
17Kwa maana Habari Njema inaonyesha wazi jinsi Mungu anavyowakubali watu kuwa waadilifu; jambo hili hufanyika kwa imani, tangu mwanzo mpaka mwisho. Kama ilivyoandikwa: "Mwadilifu kwa imani ataishi."
18人类不尊 神为 神 神的震怒,从天上向所有不虔不义的人显露出来,就是向那些以不义压制真理的人显露出来。
18Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa binadamu ambao kwa njia zao mbaya wanaupinga ukweli usijulikane.
19 神的事情,人所能知道的,在他们里面原是明显的,因为 神已经向他们显明了。
19Kwa maana, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao; maana Mungu mwenyewe ameyadhirisha.
20其实自从创世以来, 神那看不见的事,就如他永恒的大能和神性,都是看得见的,就是从他所造的万物中可以领悟,叫人没有办法推诿。
20Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea!
21因为他们虽然知道 神,却不尊他为 神,也不感谢他,反而心思变为虚妄,愚顽的心就迷糊了。
21Ingawa wanajua kuna Mungu, lakini hawampi heshima anayostahili, wala hawamshukuru. Badala yake, fikira zao zimekuwa batili na akili zao tupu zimejaa giza.
22他们自以为是聪明的,却成了愚蠢的。
22Wanajidai kuwa wenye hekima, kumbe ni wapumbavu.
23他们用必朽坏的人、飞禽、走兽和昆虫的形象,取代了永不朽坏的 神的荣耀。
23Wanaacha kumwabudu Mungu aishiye milele, na badala yake, wanaabudu sanamu zilizo mfano wa binadamu ambaye hufa, mfano wa wanyama, ndege, au wanyama watambaao.
24人类种种的罪恶因此, 神就任凭他们顺着心中的私欲去作污秽的事,以致羞辱自己的身体。
24Kwa sababu hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya za mioyo yao na kufanyiana mambo ya aibu kwa miili yao.
25他们用虚谎取代了 神的真理,敬拜事奉受造之物,却不敬拜事奉造物的主。他是永远可称颂的,阿们。
25Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina.
26因此, 神就任凭他们放纵可耻的情欲:他们的女人把原来的性的功能,变成违反自然的功能;
26Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile.
27同样地,男人也舍弃了女人原来的性功能,彼此欲火攻心,男人与男人作出可耻的事。他们这样妄为,就在自己身上受到应该受的报应。
27Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu.
28他们既然故意不认识 神, 神就任凭他们存着败坏的心,去作那些不正当的事。
28Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya.
29这些人充满了各样的不义、邪恶、贪心、阴险;满怀嫉妒、凶杀、好斗、欺诈、幸灾乐祸;又是好说谗言的、
29Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya,
30毁谤人的、憎恨 神的、凌辱人的、傲慢的、自夸的、制造恶事的、忤逆父母的、
30na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao;
31冥顽不灵的、不守信用的、冷酷无情的、没有恻隐之心的。
31hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine.
32他们虽然明明知道行这些事的人, 神判定他们是该死的,然而他们不单自己去行,也喜欢别人去行。
32Wanajua kwamba Sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.