聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Romans

2

1 神照各人所作的报应各人
1Basi, rafiki, kama unawahukumu wengine, huwezi kamwe kujitetea haidhuru wewe ni nani. Kwa maana, kwa kuwahukumu wengine, unajilaani wewe mwenyewe kwa vile nawe unayafanya mambo yaleyale unayohukumu.
2我们知道, 神必照着真理审判行这些事的人。
2Tunajua kwamba hukumu ya Mungu kwa wale wanaofanya mambo kama hayo ni hukumu ya haki.
3你这个人,你判断行这些事的人,自己所行的却是一样,你以为能逃脱 神的审判吗?
3Lakini wewe, rafiki, unayewahukumu wale wanaofanya mambo kama hayo bali wewe pia unayafanya, je unadhani utaiepa hukumu ya Mungu?
4还是你藐视 神丰富的恩慈、宽容和忍耐,不晓得他的恩慈是要领你悔改的吗?
4Au labda unaudharau wema wake mkuu, uvumilivu wake na saburi yake, bila kutambua kwamba wema wake huo una shabaha ya kukuongoza upate kutubu?
5可是你一直硬着心肠,不肯悔改,为自己积蓄 神的忿怒,就是他彰显公义审判的那天所要发的忿怒。
5Lakini unao ugumu na ukaidi wa moyo, na hivyo unajilundikia adhabu kwa Siku ile ambayo ghadhabu ya Mungu na hukumu zake za haki vitadhihirishwa.
6 神必照各人所作的报应各人:
6Siku hiyo Mungu atamlipa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
7以永生报答那些耐心行善、寻求荣耀尊贵和不朽的人,
7Wale wanaozingatia kutenda mema, kutafuta utukufu na heshima ya Mungu na kutokufa, watapata uzima wa milele.
8却以震怒和愤恨报应那些自私自利、不顺从真理而顺从不义的人;
8Lakini wale wengine wenye ubinafsi, wenye kukataa mambo ya haki na kufuata uovu, wataangukiwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
9把患难和愁苦加给所有作恶的人,先是犹太人,后是希腊人,
9Mateso na maumivu yatampata binadamu yeyote atendaye uovu. Yatawapata Wayahudi kwanza, na watu wa mataifa mengine pia.
10却把荣耀、尊贵与平安赐给所有行善的人,先是犹太人,后是希腊人。
10Lakini Mungu atawapa utukufu, heshima na amani wale wanaotenda mema; Wayahudi kwanza, na watu wa mataifa mengine pia.
11因为 神并不偏待人。
11Maana Mungu hambagui mtu yeyote.
12律法的作用刻在人心凡不在律法之下犯了罪的,将不按律法而灭亡;凡在律法之下犯了罪的,将按律法受审判。
12Wale wanaotenda dhambi bila kuijua Sheria ya Mose wataangamia ingawaje hawajui Sheria. Na wale wanaotenda dhambi wakiwa wanaijua Sheria watahukumiwa kisheria.
13因为在 神面前,不是听律法的为义,而是行律法的得称为义。
13Mtu hafanywi kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuisikia Sheria, bali kwa kuitii Sheria.
14没有律法的外族人,如果按本性行律法上的事,他们虽然没有律法,自己就是自己的律法;
14Mathalan: watu wa mataifa mengine hawana Sheria ya Mose; lakini kila wanapotimiza matakwa ya Sheria wakiongozwa na dhamiri zao, wao wenyewe wanakuwa kipimo cha Sheria ingawa hawaijui Sheria.
15这就表明律法的作用是刻在他们的心里,有他们的良心一同作证,他们的思想互相较量,或作控告、或作辩护。
15Mwenendo wao unaonyesha kwamba matakwa ya Sheria yameandikwa mioyoni mwao. Dhamiri zao zinashuhudia pia jambo hilo, maana fikira zao mara nyingine huwashtaki, na mara nyingine huwatetea.
16这也要照着我所传的福音,在 神借着耶稣基督审判各人隐情的那一天,彰显出来。
16Hivyo, kufuatana na hii Habari Njema ninayohubiri, ndivyo itakavyokuwa wakati Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya binadamu kwa njia ya Yesu Kristo.
17内心作犹太人的才是犹太人你身为犹太人,倚靠律法,仗着 神夸口,
17Na wewe, je? Wewe mwenyewe unajiita Myahudi; unaitumainia Sheria na kujivunia kuwa wa Mungu;
18而且明白他的旨意,又从律法得了教导,能够辨别什么是好的,
18kwa njia ya Sheria unajua matakwa ya Mungu na unaweza kuchagua jambo jema;
19自信是瞎子的向导,在黑暗中的人的光,
19wewe unajiona kuwa kiongozi wa vipofu na mwanga kwa wale walio gizani;
20愚昧人的导师,小孩子的教师,在律法上得了整套的知识和真理;
20unajiona kuwa mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa wale wasiokomaa bado. Unayo katika Sheria picha kamili ya elimu na ukweli.
21你既然教导别人,难道不教导自己吗?你传讲不可偷窃,自己却偷窃吗?
21Basi, wewe unawafundisha wengine; kwa nini hujifundishi wewe mwenyewe? Unawahubiria wengine wasiibe, lakini kumbe wewe mwenyewe unaiba.
22你说不可奸淫,自己却奸淫吗?你憎恶偶像,自己却劫掠庙宇吗?
22Unasema: "Msizini," na huku wewe unazini; unachukia sanamu za miungu hali wewe unajitajirisha kwa kuiba katika nyumba za miungu.
23你既然以律法夸口,自己却因犯律法而羞辱 神吗?
23Kwa kujigamba ati unayo Sheria ya Mungu, je huoni kwamba kwa kuivunja Sheria unamdharau Mungu?
24正如经上所说的:“ 神的名,因你们的缘故在列邦中被亵渎。”
24Kama vile Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Watu wa mataifa mengine wamelikufuru jina la Mungu kwa sababu yenu ninyi Wayahudi!"
25你若遵行律法,割礼固然有益处;但你若是犯律法的,你的割礼就不是割礼了。
25Kutahiriwa kwako kutakuwa na maana kama ukiitii Sheria. Lakini kama unaivunja Sheria, basi, ni afadhali ungalibaki bila kutahiriwa.
26这样,没有受割礼的人,如果遵守律法所规定的,他虽然没有受过割礼,不也算是受过割礼的吗?
26Kama mtu wa mataifa mengine ambaye hakutahiriwa akitimiza matakwa ya Sheria, hakika atafikiriwa kana kwamba ametahiriwa.
27那本来没有受割礼却遵守律法的人,就要审判你这有仪文和割礼而犯律法的人。
27Watu wa mataifa mengine watakuhukumu wewe Myahudi kama ukiivunja Sheria, ingawaje unayo maandishi ya Sheria na umetahiriwa, hali wao wanaitii Sheria ingawa hawakutahiriwa.
28因为表面上作犹太人的并不是犹太人,在肉身上表面的割礼也不是割礼。
28Ndiyo kusema, si kila anayeonekana kwa nje kuwa Myahudi ni Myahudi wa kweli, wala mtu hawi Myahudi wa kweli ati kwa kuwa ametahiriwa kimwili.
29唯有在内心作犹太人的才是犹太人;割礼也是心里的,是靠着圣灵而不是靠着仪文。这样的人所受的称赞,不是从人来的,而是从 神来的。
29Myahudi wa kweli ni yule aliye Myahudi kwa ndani, yaani yule ambaye ametahiriwa moyoni. Hili ni jambo la Roho, na si jambo la maandishi ya Sheria. Mtu wa namna hiyo anapata sifa, si kutoka kwa watu, bali kutoka kwa Mungu.