聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Romans

10

1弟兄们,我心里切切盼望的,并且为以色列人向 神祈求的,是要他们得救。
1Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.
2我可以为他们作证,他们对 神有热心,但不是按着真见识;
2Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli.
3他们既然不明白 神的义,而又企图建立自己的义,就不服 神的义了。
3Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe, na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu.
4因为律法的终极就是基督,使所有信的人都得着义。
4Maana kwa kuja kwake Kristo, Sheria imefikia kikomo chake, ili kila mtu anayeamini akubaliwe kuwa mwadilifu.
5求告主名的都必得救论到出于律法的义,摩西写着说:“遵行这些事的人就必因这些事而活。”
5Kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, Mose aliandika hivi: "Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya Sheria ataishi."
6但那出于信心的义却这样说:“你心里不要说:‘谁要升到天上去呢?’(就是要把基督领下来,)
6Lakini, kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: "Usiseme moyoni mwako: Nani atapanda mpaka mbinguni? (yaani, kumleta Kristo chini);
7或是说:‘谁要下到深渊去呢?’(就是要把基督从死人中领上来。)”
7wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu)."
8然而那出于信心的义还说什么呢?”这话与你相近,在你口里,也在你心里。”这话就是我们所传信心的信息。
8Maandiko Matakatifu yesema hivi, "Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako" nao ndio ile imani tunayoihubiri.
9你若口里认耶稣为主,心里信 神使他从死人中复活,就必得救;
9Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.
10因为心里相信就必称义,用口承认就必得救。
10Maana tunaamini kwa moyo na kukubaliwa kuwa waadilifu; na tunakiri kwa midomo yetu na kuokolewa.
11经上说:“所有信靠他的人,必不致失望。”
11Maandiko Matakatifu yasema: "Kila amwaminiye hatakuwa na sababu ya kuaibika."
12其实并不分犹太人和希腊人,因为大家同有一位主;他厚待所有求告他的人,
12Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao.
13因为“凡求告主名的,都必得救。”
13Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa."
14然而,人还没有信他,怎能求告他呢?没有听见他,怎能信他呢?没有人传扬,怎能听见呢?
14Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?
15如果没有蒙差遣,怎能传扬呢?如经上所记:“那些传美事报喜讯的人,他们的脚踪多么美!”
15Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!"
16但并不是所有的人都顺从福音,因为以赛亚说:“主啊,我们所传的,有谁信呢?”
16Lakini wote hawakuipokea hiyo Habari Njema. Maana Isaya alisema: "Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?"
17可见信心是从所听的道来的,所听的道是借着基督的话来的。
17Hivyo basi, imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
18但是我要说,他们没有听见吗?他们的确听见了,如经上所记:“他们的声音传遍全地,他们的言语传到地极。”
18Lakini nauliza: je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Sauti yao imeenea duniani kote; maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu."
19我再说:以色列人真的不明白吗?首先,摩西说:“我要使你们对那不是子民的生嫉妒,对那无知的民族起忿怒。”
19Tena nauliza: je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni kwa kwanza kujibu: "Nitawafanyeni mwaonee wivu watu ambao si taifa; nitawafanyeni muwe na hasira juu ya taifa la watu wapumbavu."
20后来,以赛亚也放胆地说:“没有寻找我的,我让他们找到;没有求问我的,我向他们显现。”
20Tena Isaya anathubutu hata kusema: "Wale ambao hawakunitafuta wamenipata; nimejionyesha kwao wasiouliza habari zangu."
21论到以色列人,他却说:“我整天向那悖逆顶嘴的子民伸开双手。”
21Lakini kuhusu Israeli anasema: "Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii."