聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Romans

9

1 神拣选以色列人
1Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2我大大忧愁,心里常常伤痛。
2Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3为我的同胞,就是我骨肉之亲,就算自己受咒诅,与基督隔绝,我也甘心。
3kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4他们是以色列人:嗣子的名分、荣耀、众约、律法、敬拜的礼仪和各样的应许,都是他们的。
4Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5蒙拣选的列祖也是他们的祖宗;按肉身来说,基督也是出自他们这一族。其实,他是在万有之上,永远受称颂的 神。阿们。
5Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina.
6当然,这不是说 神的话落了空,因为出自以色列的,不都是以色列人;
6Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7也不因为他们是亚伯拉罕的后裔,就都成为他的儿女,只有“以撒生的,才可以称为你的后裔”,
7Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Wazao wake watatokana na Isaka."
8这就是说,肉身生的儿女并不是 神的儿女,只有凭着应许生的儿女才算是后裔。
8Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9因为所应许的话是这样:“明年这个时候我要来,撒拉必定生一个儿子。”
9Maana ahadi yenyewe ni hii: "Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto."
10不但如此,利百加也是这样:既然从一个人,就是从我们的祖宗以撒怀了孕,
10Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11双生子还没有生下来,善恶也没有行出来(为要坚定 神拣选人的旨意,
11Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12不是由于行为,而是由于那呼召者), 神就对她说:“将来大的要服事小的。”
12Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13正如经上所记的:“我爱雅各,却恶以扫。”
13Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia."
14既是这样,我们可以说什么呢? 神不公平吗?绝对不会!
14Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15因为他对摩西说:“我要怜悯谁,就怜悯谁;我要恩待谁,就恩待谁。”
15Maana alimwambia Mose: "Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka."
16这样看来,既不是出于人意,也不是由于人为,只在于那怜悯人的 神。
16Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17经上有话对法老说:“我把你兴起来,是要借着你显出我的大能,并且使我的名传遍全地。”
17Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: "Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani."
18这样看来,他愿意怜悯谁就怜悯谁,愿意谁刚硬就使谁刚硬。
18Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 神显出忿怒又施行怜悯这样,你会对我说:“那么他为什么责怪人呢?有谁抗拒他的旨意呢?”
19Labda utaniuliza: "Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?"
20你这个人哪,你是谁,竟敢跟 神顶嘴呢?被造的怎么可以对造他的说:“你为什么把我做成这个样子呢?”
20Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: "Kwa nini umenitengeneza namna hii?"
21陶匠难道没有权用同一团的泥,又做贵重的、又做卑贱的器皿吗?
21Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22如果 神有意要显明他的忿怒,彰显他的大能,而多多容忍那可怒、预备遭毁灭的器皿,
22Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23为了要使他丰盛的荣耀,彰显在那蒙恩、早已预备要得荣耀的器皿上,这又有什么不可呢?
23Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24这器皿就是我们这些不但从犹太人中,也从外族人中蒙召的人。
24Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25就如 神在何西阿书上说的:“我要称那不是我子民的为我的子民,那不蒙爱的为蒙爱的;
25Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: "Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26从前在什么地方对他们说:你们不是我的子民,将来就在那里称他们为永活 神的儿子。”
26Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai."
27以赛亚指着以色列人大声说:“以色列子孙的数目虽然多如海沙,得救的不过是剩下的余数;
27Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: "Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28因为主必在地上迅速而彻底地成就他的话。”
28maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote."
29又如以赛亚早已说过的:“如果不是万军之主给我们存留后裔,我们早就像所多玛和蛾摩拉一样了。”
29Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: "Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora."
30以色列人因为不信而绊倒既是这样,我们还有什么可说的呢?那不追求义的外族人却得了义,就是因信而得的义。
30Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31但以色列人追求律法的义(“律法的义”原文作“义的律法”),却达不到律法的要求。
31hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32这是什么缘故呢?因为他们不凭信心,只靠行为。他们绊倒在那绊脚石上,
32Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33正如经上所记:“看哪,我在锡安放了一块绊脚石,是绊倒人的磐石;信靠他的人,必不致失望。”
33kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: "Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!"