1要传讲纯正的道理
1Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho safi.
2劝老年人要有节制、庄重、自律,在信心、爱心、忍耐上都要健全。
2Waambie wazee kwamba wanapaswa kuwa na kiasi, wawe na busara na wataratibu; wanapaswa kuwa timamu katika imani yao, upendo na uvumilivu.
3照样,劝年老的妇女要生活敬虔,不说谗言,不被酒奴役,用善道教导人,
3Hali kadhalika waambie wanawake wazee wawe na mwenendo wa uchaji wa Mungu; wasiwe wachongezi, au watumwa wa pombe. Wanapaswa kufundisha mambo mema,
4好提醒年轻的妇女爱丈夫爱儿女,
4ili wawazoeze kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto,
5并且自律、贞洁、理家、善良、顺从自己的丈夫,免得 神的道受毁谤。
5wawe na kiasi na safi, waangalie vizuri mambo ya nyumbani, na wawatii waume zao, ili ujumbe wa Mungu usije ukadharauliwa.
6照样,劝年轻的男子要自律。
6Kadhalika, wahimize vijana wawe na kiasi.
7无论在什么事上你都要显出好行为的榜样,在教导上要纯全,要庄重,
7Katika mambo yote wewe mwenyewe unapaswa kuwa mfano wa matendo mema. Uwe mnyofu na uwe na uzito katika mafundisho yako.
8言词要纯正,无可指摘,使反对的人因为无从毁谤,就自觉惭愧。
8Maneno yako yasiwe na hitilafu yoyote ili adui zako waaibike wasipopata chochote kibaya cha kusema juu yetu.
9劝仆人要凡事顺服自己的主人,讨他欢喜,不要顶嘴。
9Watumwa wanapaswa kuwatii wakuu wao na kuwapendeza katika mambo yote. Wasibishane nao,
10不要私取财物,却要显示绝对的诚实,好使我们救主 神的道理,在凡事上都得着尊荣。
10au kuiba vitu vyao. Badala yake wanapaswa kuonyesha kwamba wao ni wema na waaminifu daima, ili, kwa matendo yao yote, wayapatie sifa njema mafundisho juu ya Mungu, Mwokozi wetu.
11 神拯救万人的恩典已经显明出来了。
11Maana neema ya Mungu imedhihirishwa kwa ajili ya wokovu wa watu wote.
12这恩典训练我们除去不敬虔的心,和属世的私欲,在今生过着自律、公正、敬虔的生活,
12Neema hiyo yatufunza kuachana na uovu wote na tamaa za kidunia; tuwe na kiasi, tuishi maisha adili na ya kumcha Mungu katika ulimwengu huu wa sasa,
13等候那有福的盼望,就是我们伟大的 神,救主耶稣基督荣耀的显现。
13tukiwa tunangojea siku ile ya heri tunayoitumainia, wakati utakapotokea utukufu wa Mungu Mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
14他为我们舍己,为的是要救赎我们脱离一切不法的事,并且洁净我们作他自己的子民,热心善工。
14Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili atukomboe kutoka katika uovu wote na kutufanya watu safi walio wake yeye mwenyewe, watu walio na hamu ya kutenda mema.
15你要传讲这些事,运用各样的权柄去劝戒人,责备人;不要让人轻看你。
15Basi, fundisha mambo hayo na tumia mamlaka yako yote ukiwahimiza na kuwaonya wasikilizaji wako. Mtu yeyote na asikudharau.