King James Version

Swahili: New Testament

1 Corinthians

15

1Moreover, brethren, I declare unto you the gospel which I preached unto you, which also ye have received, and wherein ye stand;
1Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
2By which also ye are saved, if ye keep in memory what I preached unto you, unless ye have believed in vain.
2Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
3For I delivered unto you first of all that which I also received, how that Christ died for our sins according to the scriptures;
3Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
4And that he was buried, and that he rose again the third day according to the scriptures:
4kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
5And that he was seen of Cephas, then of the twelve:
5kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
6After that, he was seen of above five hundred brethren at once; of whom the greater part remain unto this present, but some are fallen asleep.
6Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
7After that, he was seen of James; then of all the apostles.
7Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
8And last of all he was seen of me also, as of one born out of due time.
8Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
9For I am the least of the apostles, that am not meet to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
9Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
10But by the grace of God I am what I am: and his grace which was bestowed upon me was not in vain; but I laboured more abundantly than they all: yet not I, but the grace of God which was with me.
10Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
11Therefore whether it were I or they, so we preach, and so ye believed.
11Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
12Now if Christ be preached that he rose from the dead, how say some among you that there is no resurrection of the dead?
12Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
13But if there be no resurrection of the dead, then is Christ not risen:
13Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
14And if Christ be not risen, then is our preaching vain, and your faith is also vain.
14na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
15Yea, and we are found false witnesses of God; because we have testified of God that he raised up Christ: whom he raised not up, if so be that the dead rise not.
15Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua--kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
16For if the dead rise not, then is not Christ raised:
16Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
17And if Christ be not raised, your faith is vain; ye are yet in your sins.
17Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
18Then they also which are fallen asleep in Christ are perished.
18Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
19If in this life only we have hope in Christ, we are of all men most miserable.
19Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
20But now is Christ risen from the dead, and become the firstfruits of them that slept.
20Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
21For since by man came death, by man came also the resurrection of the dead.
21Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
22For as in Adam all die, even so in Christ shall all be made alive.
22Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
23But every man in his own order: Christ the firstfruits; afterward they that are Christ's at his coming.
23Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
24Then cometh the end, when he shall have delivered up the kingdom to God, even the Father; when he shall have put down all rule and all authority and power.
24Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
25For he must reign, till he hath put all enemies under his feet.
25Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
26The last enemy that shall be destroyed is death.
26Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
27For he hath put all things under his feet. But when he saith all things are put under him, it is manifest that he is excepted, which did put all things under him.
27Maana, Maandiko yasema: "Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake." Lakini, Maandiko yanaposema: "Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale" ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
28And when all things shall be subdued unto him, then shall the Son also himself be subject unto him that put all things under him, that God may be all in all.
28Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
29Else what shall they do which are baptized for the dead, if the dead rise not at all? why are they then baptized for the dead?
29Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
30And why stand we in jeopardy every hour?
30Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
31I protest by your rejoicing which I have in Christ Jesus our Lord, I die daily.
31Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
32If after the manner of men I have fought with beasts at Ephesus, what advantageth it me, if the dead rise not? let us eat and drink; for to morrow we die.
32Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, "Tule na tunywe, maana kesho tutakufa."
33Be not deceived: evil communications corrupt good manners.
33Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
34Awake to righteousness, and sin not; for some have not the knowledge of God: I speak this to your shame.
34Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
35But some man will say, How are the dead raised up? and with what body do they come?
35Lakini mtu anaweza kuuliza: "Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?"
36Thou fool, that which thou sowest is not quickened, except it die:
36Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
37And that which thou sowest, thou sowest not that body that shall be, but bare grain, it may chance of wheat, or of some other grain:
37Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
38But God giveth it a body as it hath pleased him, and to every seed his own body.
38Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
39All flesh is not the same flesh: but there is one kind of flesh of men, another flesh of beasts, another of fishes, and another of birds.
39Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
40There are also celestial bodies, and bodies terrestrial: but the glory of the celestial is one, and the glory of the terrestrial is another.
40Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
41There is one glory of the sun, and another glory of the moon, and another glory of the stars: for one star differeth from another star in glory.
41Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
42So also is the resurrection of the dead. It is sown in corruption; it is raised in incorruption:
42Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
43It is sown in dishonour; it is raised in glory: it is sown in weakness; it is raised in power:
43Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
44It is sown a natural body; it is raised a spiritual body. There is a natural body, and there is a spiritual body.
44Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
45And so it is written, The first man Adam was made a living soul; the last Adam was made a quickening spirit.
45Maana Maandiko yasema: "Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;" lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
46Howbeit that was not first which is spiritual, but that which is natural; and afterward that which is spiritual.
46Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
47The first man is of the earth, earthy; the second man is the Lord from heaven.
47Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
48As is the earthy, such are they also that are earthy: and as is the heavenly, such are they also that are heavenly.
48Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
49And as we have borne the image of the earthy, we shall also bear the image of the heavenly.
49Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
50Now this I say, brethren, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God; neither doth corruption inherit incorruption.
50Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
51Behold, I shew you a mystery; We shall not all sleep, but we shall all be changed,
51Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
52In a moment, in the twinkling of an eye, at the last trump: for the trumpet shall sound, and the dead shall be raised incorruptible, and we shall be changed.
52wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
53For this corruptible must put on incorruption, and this mortal must put on immortality.
53Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
54So when this corruptible shall have put on incorruption, and this mortal shall have put on immortality, then shall be brought to pass the saying that is written, Death is swallowed up in victory.
54Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: "Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!"
55O death, where is thy sting? O grave, where is thy victory?
55"Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?"
56The sting of death is sin; and the strength of sin is the law.
56Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
57But thanks be to God, which giveth us the victory through our Lord Jesus Christ.
57Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58Therefore, my beloved brethren, be ye stedfast, unmoveable, always abounding in the work of the Lord, forasmuch as ye know that your labour is not in vain in the Lord.
58Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.