1Now concerning the collection for the saints, as I have given order to the churches of Galatia, even so do ye.
1Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
2Upon the first day of the week let every one of you lay by him in store, as God hath prospered him, that there be no gatherings when I come.
2Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
3And when I come, whomsoever ye shall approve by your letters, them will I send to bring your liberality unto Jerusalem.
3Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
4And if it be meet that I go also, they shall go with me.
4Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
5Now I will come unto you, when I shall pass through Macedonia: for I do pass through Macedonia.
5Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia--maana nataraji kupitia Makedonia.
6And it may be that I will abide, yea, and winter with you, that ye may bring me on my journey whithersoever I go.
6Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
7For I will not see you now by the way; but I trust to tarry a while with you, if the Lord permit.
7Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
8But I will tarry at Ephesus until Pentecost.
8Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
9For a great door and effectual is opened unto me, and there are many adversaries.
9Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
10Now if Timotheus come, see that he may be with you without fear: for he worketh the work of the Lord, as I also do.
10Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
11Let no man therefore despise him: but conduct him forth in peace, that he may come unto me: for I look for him with the brethren.
11Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
12As touching our brother Apollos, I greatly desired him to come unto you with the brethren: but his will was not at all to come at this time; but he will come when he shall have convenient time.
12Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
13Watch ye, stand fast in the faith, quit you like men, be strong.
13Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
14Let all your things be done with charity.
14Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
15I beseech you, brethren, (ye know the house of Stephanas, that it is the firstfruits of Achaia, and that they have addicted themselves to the ministry of the saints,)
15Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
16That ye submit yourselves unto such, and to every one that helpeth with us, and laboureth.
16muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
17I am glad of the coming of Stephanas and Fortunatus and Achaicus: for that which was lacking on your part they have supplied.
17Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
18For they have refreshed my spirit and your's: therefore acknowledge ye them that are such.
18Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
19The churches of Asia salute you. Aquila and Priscilla salute you much in the Lord, with the church that is in their house.
19Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
20All the brethren greet you. Greet ye one another with an holy kiss.
20Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
21The salutation of me Paul with mine own hand.
21Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
22If any man love not the Lord Jesus Christ, let him be Anathema Maranatha.
22Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA--BWANA, njoo!
23The grace of our Lord Jesus Christ be with you.
23Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24My love be with you all in Christ Jesus. Amen.
24Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.