King James Version

Swahili: New Testament

Luke

2

1And it came to pass in those days, that there went out a decree from Caesar Augustus that all the world should be taxed.
1Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2(And this taxing was first made when Cyrenius was governor of Syria.)
2Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
3And all went to be taxed, every one into his own city.
3Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
4And Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, into Judaea, unto the city of David, which is called Bethlehem; (because he was of the house and lineage of David:)
4Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
5To be taxed with Mary his espoused wife, being great with child.
5Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
6And so it was, that, while they were there, the days were accomplished that she should be delivered.
6Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
7And she brought forth her firstborn son, and wrapped him in swaddling clothes, and laid him in a manger; because there was no room for them in the inn.
7akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
8And there were in the same country shepherds abiding in the field, keeping watch over their flock by night.
8Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
9And, lo, the angel of the Lord came upon them, and the glory of the Lord shone round about them: and they were sore afraid.
9Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
10And the angel said unto them, Fear not: for, behold, I bring you good tidings of great joy, which shall be to all people.
10Malaika akawaambia, "Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
11For unto you is born this day in the city of David a Saviour, which is Christ the Lord.
11Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
12And this shall be a sign unto you; Ye shall find the babe wrapped in swaddling clothes, lying in a manger.
12Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini."
13And suddenly there was with the angel a multitude of the heavenly host praising God, and saying,
13Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
14Glory to God in the highest, and on earth peace, good will toward men.
14"Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!"
15And it came to pass, as the angels were gone away from them into heaven, the shepherds said one to another, Let us now go even unto Bethlehem, and see this thing which is come to pass, which the Lord hath made known unto us.
15Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: "Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha."
16And they came with haste, and found Mary, and Joseph, and the babe lying in a manger.
16Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
17And when they had seen it, they made known abroad the saying which was told them concerning this child.
17Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
18And all they that heard it wondered at those things which were told them by the shepherds.
18Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
19But Mary kept all these things, and pondered them in her heart.
19Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
20And the shepherds returned, glorifying and praising God for all the things that they had heard and seen, as it was told unto them.
20Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
21And when eight days were accomplished for the circumcising of the child, his name was called JESUS, which was so named of the angel before he was conceived in the womb.
21Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
22And when the days of her purification according to the law of Moses were accomplished, they brought him to Jerusalem, to present him to the Lord;
22Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
23(As it is written in the law of the LORD, Every male that openeth the womb shall be called holy to the Lord;)
23Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: "Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana."
24And to offer a sacrifice according to that which is said in the law of the Lord, A pair of turtledoves, or two young pigeons.
24Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
25And, behold, there was a man in Jerusalem, whose name was Simeon; and the same man was just and devout, waiting for the consolation of Israel: and the Holy Ghost was upon him.
25Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
26And it was revealed unto him by the Holy Ghost, that he should not see death, before he had seen the Lord's Christ.
26Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
27And he came by the Spirit into the temple: and when the parents brought in the child Jesus, to do for him after the custom of the law,
27Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
28Then took he him up in his arms, and blessed God, and said,
28Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
29Lord, now lettest thou thy servant depart in peace, according to thy word:
29"Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30For mine eyes have seen thy salvation,
30Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
31Which thou hast prepared before the face of all people;
31ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
32A light to lighten the Gentiles, and the glory of thy people Israel.
32Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli."
33And Joseph and his mother marvelled at those things which were spoken of him.
33Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
34And Simeon blessed them, and said unto Mary his mother, Behold, this child is set for the fall and rising again of many in Israel; and for a sign which shall be spoken against;
34Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, "Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
35(Yea, a sword shall pierce through thy own soul also,) that the thoughts of many hearts may be revealed.
35na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako."
36And there was one Anna, a prophetess, the daughter of Phanuel, of the tribe of Aser: she was of a great age, and had lived with an husband seven years from her virginity;
36Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
37And she was a widow of about fourscore and four years, which departed not from the temple, but served God with fastings and prayers night and day.
37Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
38And she coming in that instant gave thanks likewise unto the Lord, and spake of him to all them that looked for redemption in Jerusalem.
38Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
39And when they had performed all things according to the law of the Lord, they returned into Galilee, to their own city Nazareth.
39Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
40And the child grew, and waxed strong in spirit, filled with wisdom: and the grace of God was upon him.
40Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
41Now his parents went to Jerusalem every year at the feast of the passover.
41Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42And when he was twelve years old, they went up to Jerusalem after the custom of the feast.
42Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43And when they had fulfilled the days, as they returned, the child Jesus tarried behind in Jerusalem; and Joseph and his mother knew not of it.
43Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
44But they, supposing him to have been in the company, went a day's journey; and they sought him among their kinsfolk and acquaintance.
44Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
45And when they found him not, they turned back again to Jerusalem, seeking him.
45Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
46And it came to pass, that after three days they found him in the temple, sitting in the midst of the doctors, both hearing them, and asking them questions.
46Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47And all that heard him were astonished at his understanding and answers.
47Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
48And when they saw him, they were amazed: and his mother said unto him, Son, why hast thou thus dealt with us? behold, thy father and I have sought thee sorrowing.
48Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, "Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni."
49And he said unto them, How is it that ye sought me? wist ye not that I must be about my Father's business?
49Yeye akawajibu, "Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?"
50And they understood not the saying which he spake unto them.
50Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
51And he went down with them, and came to Nazareth, and was subject unto them: but his mother kept all these sayings in her heart.
51Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
52And Jesus increased in wisdom and stature, and in favour with God and man.
52Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.