1Stedfast [is] the word: If any one the oversight doth long for, a right work he desireth;
1Msemo huu ni wa kweli: mtu akitaka kuwa kiongozi katika kanisa, huyo anatamani kazi nzuri.
2it behoveth, therefore, the overseer to be blameless, of one wife a husband, vigilant, sober, decent, a friend of strangers, apt to teach,
2Basi, kiongozi wa kanisa anapaswa awe mtu asiye na lawama; anapaswa awe na mke mmoja tu, awe mwenye kiasi, nidhamu na utaratibu; ni lazima awe mkarimu na anayeweza kufundisha;
3not given to wine, not a striker, not given to filthy lucre, but gentle, not contentious, not a lover of money,
3asiwe mlevi au mtu wa matata, bali awe mpole, apendaye amani; asiwe mtu wa kupenda fedha;
4his own house leading well, having children in subjection with all gravity,
4anapaswa awe mtu awezaye kuongoza vema nyumba yake, na kuwafanya watoto wake wawe watii kwa heshima yote.
5(and if any one his own house [how] to lead hath not known, how an assembly of God shall he take care of?)
5Maana kama mtu hawezi kuongoza vema nyumba yake, atawezaje kulitunza kanisa la Mungu?
6not a new convert, lest having been puffed up he may fall to a judgment of the devil;
6Mtu ambaye hajakomaa bado katika imani asifanywe kuwa kiongozi katika kanisa, asije akajaa majivuno na kuhukumiwa kama vile Ibilisi alivyohukumiwa.
7and it behoveth him also to have a good testimony from those without, that he may not fall into reproach and a snare of the devil.
7Anapaswa awe mwenye sifa njema kati ya watu walio nje ya kanisa, ili asije akalaumiwa na kuanguka katika mtego wa Ibilisi.
8Ministrants — in like manner grave, not double-tongued, not given to much wine, not given to filthy lucre,
8Wasaidizi katika kanisa wanapaswa pia kuwa watu wenye tabia njema na wanyofu; wasiwe wanywaji mno wa divai au wenye tamaa ya fedha;
9having the secret of the faith in a pure conscience,
9wanapaswa kuzingatia kwa dhamiri njema ukweli wa ndani wa imani.
10and let these also first be proved, then let them minister, being unblameable.
10Ni lazima kwanza wathibitishwe, na wakionekana kuwa wanafaa, basi, watoe huduma yao.
11Women — in like manner grave, not false accusers, vigilant, faithful in all things.
11Wake zao wanapaswa pia kuwa na tabia njema, wasiowasengenya watu, wenye kiasi na waaminifu katika mambo yote.
12Ministrants — let them be of one wife husbands; the children leading well, and their own houses,
12Msaidizi katika kanisa lazima awe na mke moja tu, na awezaye kuongoza vema watoto wake na nyumba yake.
13for those who did minister well a good step to themselves do acquire, and much boldness in faith that [is] in Christ Jesus.
13Maana wasaidizi wanaofanya kazi yao vizuri hujipatia msimamo mzuri, na wanaweza kusema bila hofu juu ya imani yao katika Kristo Yesu.
14These things I write to thee, hoping to come unto thee soon,
14Ninakuandikia barua hii nikiwa na matumaini ya kuja kwako hivi karibuni.
15and if I delay, that thou mayest know how it behoveth [thee] to conduct thyself in the house of God, which is an assembly of the living God — a pillar and foundation of the truth,
15Lakini kama nikicheleweshwa, basi, barua hii itakufahamisha mwenendo tunaopaswa kuwa nao katika nyumba ya Mungu, ambayo ni kanisa la Mungu aliye hai, na ambalo ni nguzo na msingi wa ukweli.
16and, confessedly, great is the secret of piety — God was manifested in flesh, declared righteous in spirit, seen by messengers, preached among nations, believed on in the world, taken up in glory!
16Hakuna mashaka yoyote juu ya ukuu wa siri ya dini yetu: Alionekana katika umbo la kibinadamu alithibitishwa na Roho kuwa ni mwadilifu, akaonekana na malaika. Alihubiriwa kati ya mataifa, aliaminiwa popote ulimwenguni, akachukuliwa juu mbinguni katika utukufu.