Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

2 Peter

1

1Simeon Peter, a servant and an apostle of Jesus Christ, to those who did obtain a like precious faith with us in the righteousness of our God and Saviour Jesus Christ:
1Mimi Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo, nawaandikia ninyi ambao, kwa wema wake Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo, mmejaliwa imani ileile ya thamani kuu tuliyojaliwa sisi.
2Grace to you, and peace be multiplied in the acknowledgement of God and of Jesus our Lord!
2Nawatakieni neema na amani tele katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
3As all things to us His divine power (the things pertaining unto life and piety) hath given, through the acknowledgement of him who did call us through glory and worthiness,
3Kwa uwezo wake wa kimungu, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji, ili tuishi maisha ya kumcha Mungu kwa kumjua yeye aliyetuita tuushiriki utukufu na wema wake yeye mwenyewe.
4through which to us the most great and precious promises have been given, that through these ye may become partakers of a divine nature, having escaped from the corruption in the world in desires.
4Kwa namna hiyo ametujalia zawadi kuu na za thamani ambazo alituahidia, ili kwa zawadi hizo mpate kuziepa kabisa tamaa mbaya zilizomo duniani, na mpate kuishiriki hali yake ya kimungu.
5And this same also — all diligence having brought in besides, superadd in your faith the worthiness, and in the worthiness the knowledge,
5Kwa sababu hiyo, fanyeni bidii ya kuongeza fadhila katika imani yenu: ongezeni elimu katika fadhila yenu,
6and in the knowledge the temperance, and in the temperance the endurance, and in the endurance the piety,
6kuwa na kiasi katika elimu yenu, uvumilivu katika kuwa na kiasi, uchaji wa Mungu katika uvumilivu wenu,
7and in the piety the brotherly kindness, and in the brotherly kindness the love;
7udugu katika uchaji wenu, na mapendo katika udugu wenu.
8for these things being to you and abounding, do make [you] neither inert nor unfruitful in regard to the acknowledging of our Lord Jesus Christ,
8Mkiwa na sifa hizo zote kwa wingi, zitawawezesheni kuwa watendaji na kupata faida katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
9for he with whom these things are not present is blind, dim-sighted, having become forgetful of the cleansing of his old sins;
9Lakini mtu asiye na sifa hizo ni kipofu, hawezi kuona na amesahau kwamba alikwisha takaswa dhambi zake za zamani.
10wherefore, the rather, brethren, be diligent to make stedfast your calling and choice, for these things doing, ye may never stumble,
10Kwa hiyo basi, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuufanya huo wito wenu mlioitiwa na Mungu uwe jambo la kudumu katika maisha yenu; kama mkiishi namna hiyo hamtaanguka kamwe.
11for so, richly shall be superadded to you the entrance into the age-during reign of our Lord and Saviour Jesus Christ.
11Kwa namna hiyo mtafaulu kupewa haki kamili ya kuingia katika Utawala wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
12Wherefore, I will not be careless always to remind you concerning these things, though, having known them, and having been established in the present truth,
12Kwa hiyo nitaendelea kuwakumbusheni daima mambo haya, ingawa mmekwisha yafahamu, na mko imara katika ukweli mlioupokea.
13and I think right, so long as I am in this tabernacle, to stir you up in reminding [you],
13Nadhani ni jambo jema kwangu, muda wote niishio hapa duniani, kuwapeni moyo na kuwakumbusheni juu ya mambo haya.
14having known that soon is the laying aside of my tabernacle, even as also our Lord Jesus Christ did shew to me,
14Najua kwamba karibu nitauweka kando mwili huu wenye kufa, kama Bwana alivyoniambia waziwazi.
15and I will be diligent that also at every time ye have, after my outgoing, power to make to yourselves the remembrance of these things.
15Basi, nitajitahidi kuwapatieni njia ya kuyakumbuka mambo haya kila wakati, baada ya kufariki kwangu.
16For, skilfully devised fables not having followed out, we did make known to you the power and presence of our Lord Jesus Christ, but eye-witnesses having become of his majesty —
16Wakati tulipowafundisheni juu ya ukuu wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hatukutegemea hadithi tupu zisizo na msingi. Sisi tuliuona utukufu wake kwa macho yetu wenyewe.
17for having received from God the Father honour and glory, such a voice being borne to him by the excellent glory: `This is My Son — the beloved, in whom I was well pleased;`
17Sisi tulikuwapo wakati alipopewa heshima na kutukuzwa na Mungu Baba, wakati sauti ilipomjia kutoka kwake yeye aliye Utukufu Mkuu, ikisema: "Huyu ni Mwanangu mpenzi, nimependezwa naye."
18and this voice we — we did hear, out of heaven borne, being with him in the holy mount.
18Tena, sisi wenyewe tulisikia sauti hiyo kutoka mbinguni wakati tulipokuwa pamoja naye juu ya ule mlima mtakatifu.
19And we have more firm the prophetic word, to which we do well giving heed, as to a lamp shining in a dark place, till day may dawn, and a morning star may arise — in your hearts;
19Tena, ujumbe wa manabii watuthibitishia jambo hilo; nanyi mwafanya vema kama mkiuzingatia, maana ni kama taa inayoangaza mahali penye giza mpaka Siku ile itakapopambazuka na mwanga wa nyota ya asubuhi utakapong'ara mioyoni mwenu.
20this first knowing, that no prophecy of the Writing doth come of private exposition,
20Zaidi ya hayo, lakini, kumbukeni kwamba hakuna mtu yeyote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu.
21for not by will of man did ever prophecy come, but by the Holy Spirit borne on holy men of God spake.
21Maana hakuna ujumbe wa kinabii unaotokana na matakwa ya binadamu, bali watu walinena ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.