1And the apostles and the brethren who are in Judea heard that also the nations did receive the word of God,
1Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2and when Peter came up to Jerusalem, those of the circumcision were contending with him,
2Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3saying — `Unto men uncircumcised thou didst go in, and didst eat with them!`
3"Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4And Peter having begun, did expound to them in order saying,
4Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5`I was in the city of Joppa praying, and I saw in a trance a vision, a certain vessel coming down, as a great sheet by four corners being let down out of the heaven, and it came unto me;
5"Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6at which having looked stedfastly, I was considering, and I saw the four-footed beasts of the earth, and the wild beasts, and the creeping things, and the fowls of heaven;
6Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7and I heard a voice saying to me, Having risen, Peter, slay and eat;
7Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8and I said, Not so, Lord; because anything common or unclean hath at no time entered into my mouth;
8Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9and a voice did answer me a second time out of the heaven, What God did cleanse, thou — declare not thou common.
9Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10`And this happened thrice, and again was all drawn up to the heaven,
10Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11and, lo, immediately, three men stood at the house in which I was, having been sent from Cesarea unto me,
11Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12and the Spirit said to me to go with them, nothing doubting, and these six brethren also went with me, and we did enter into the house of the man,
12Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13he declared also to us how he saw the messenger in his house standing, and saying to him, Send men to Joppa, and call for Simon, who is surnamed Peter,
13Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14who shall speak sayings by which thou shalt be saved, thou and all thy house.
14Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15`And in my beginning to speak, the Holy Spirit did fall upon them, even as also upon us in the beginning,
15Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16and I remembered the saying of the Lord, how he said, John indeed did baptize with water, and ye shall be baptized with the Holy Spirit;
16Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17if then the equal gift God did give to them as also to us, having believed upon the Lord Jesus Christ, I — how was I able to withstand God?`
17Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?"
18And they, having heard these things, were silent, and were glorifying God, saying, `Then, indeed, also to the nations did God give the reformation to life.`
18Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, "Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!"
19Those, indeed, therefore, having been scattered abroad, from the tribulation that came after Stephen, went through unto Phenice, and Cyprus, and Antioch, speaking the word to none except to Jews only;
19Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20and there were certain of them men of Cyprus and Cyrene, who having entered into Antioch, were speaking unto the Hellenists, proclaiming good news — the Lord Jesus,
20Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21and the hand of the Lord was with them, a great number also, having believed, did turn unto the Lord.
21Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22And the account was heard in the ears of the assembly that [is] in Jerusalem concerning them, and they sent forth Barnabas to go through unto Antioch,
22Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23who, having come, and having seen the grace of God, was glad, and was exhorting all with purpose of heart to cleave to the Lord,
23Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24because he was a good man, and full of the Holy Spirit, and of faith, and a great multitude was added to the Lord.
24Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25And Barnabas went forth to Tarsus, to seek for Saul,
25Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26and having found him, he brought him to Antioch, and it came to pass that they a whole year did assemble together in the assembly, and taught a great multitude, the disciples also were divinely called first in Antioch Christians.
26Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27And in those days there came from Jerusalem prophets to Antioch,
27Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28and one of them, by name Agabus, having stood up, did signify through the Spirit a great dearth is about to be throughout all the world — which also came to pass in the time of Claudius Caesar —
28Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29and the disciples, according as any one was prospering, determined each of them to send for ministration to the brethren dwelling in Judea,
29Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30which also they did, having sent unto the elders by the hand of Barnabas and Saul.
30Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.