Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Acts

12

1And about that time, Herod the king put forth his hands, to do evil to certain of those of the assembly,
1Karibu wakati huohuo, mfalme Herode alianza kuwatesa baadhi ya Wakristo.
2and he killed James, the brother of John, with the sword,
2Alimwua kwa upanga Yakobo ndugu yake Yohane.
3and having seen that it is pleasing to the Jews, he added to lay hold of Peter also — and they were the days of the unleavened food —
3Alipoona kuwa kitendo hiki kiliwapendeza Wayahudi, aliendelea, akamkamata Petro. (Hiyo ilifanyika wakati wa sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu.)
4whom also having seized, he did put in prison, having delivered [him] to four quaternions of soldiers to guard him, intending after the passover to bring him forth to the people.
4Baada ya kutiwa nguvuni, Petro alifungwa gerezani, akawekwa chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari wannewanne. Herode alikusudia kumtoa hadharani baada ya sikukuu ya Pasaka.
5Peter, therefore, indeed, was kept in the prison, and fervent prayer was being made by the assembly unto God for him,
5Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.
6and when Herod was about to bring him forth, the same night was Peter sleeping between two soldiers, having been bound with two chains, guards also before the door were keeping the prison,
6Usiku, kabla ya siku ile ambayo Herode angemtoa Petro hadharani, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili. Alikuwa amefungwa minyororo miwili, na walinzi walikuwa wanalinda lango la gereza.
7and lo, a messenger of the Lord stood by, and a light shone in the buildings, and having smitten Peter on the side, he raised him up, saying, `Rise in haste,` and his chains fell from off [his] hands.
7Ghafla, malaika wa Bwana akasimama karibu naye na mwanga ukaangaza kile chumba cha gereza. Malaika akamgusa akisema, "Amka upesi!" Mara ile minyororo ikaanguka kutoka katika mikono yake.
8The messenger also said to him, `Gird thyself, and bind on thy sandals;` and he did so; and he saith to him, `Put thy garment round and be following me;`
8Malaika akamwambia, "Jifunge mshipi wako, vaa viatu vyako." Akafanya hivyo. Kisha huyo malaika akamwambia, "Vaa koti lako, unifuate."
9and having gone forth, he was following him, and he knew not that it is true that which is done through the messenger, and was thinking he saw a vision,
9Petro akamfuata nje lakini hakujua kama hayo yaliyofanywa na huyo malaika yalikuwa ya kweli; alidhani alikuwa anaota ndoto.
10and having passed through a first ward, and a second, they came unto the iron gate that is leading to the city, which of its own accord did open to them, and having gone forth, they went on through one street, and immediately the messenger departed from him.
10Walipita kituo cha kwanza cha ulinzi na cha pili, halafu wakafika kwenye mlango wa chuma wa kuingilia mjini. Huo mlango ukawafungukia wenyewe, nao wakatoka nje. Wakawa wanatembea katika barabara moja na mara yule malaika akamwacha Petro peke yake.
11And Peter having come to himself, said, `Now I have known of a truth that the Lord did sent forth His messenger, and did deliver me out of the hand of Herod, and all the expectation of the people of the Jews;`
11Hapo ndipo Petro alipotambua yaliyotukia, akasema, "Sasa najua kwa hakika kwamba Bwana amemtuma malaika wake akaniokoa kutoka katika mkono wa Herode na kutoka katika mambo yale yote watu wa Israeli waliyotazamia."
12also, having considered, he came unto the house of Mary, the mother of John, who is surnamed Mark, where there were many thronged together and praying.
12Alipotambua hivyo alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Maria mama yake Yohane aitwaye Marko. Humo watu wengi walikuwa wamekusanyika wakisali.
13And Peter having knocked at the door of the porch, there came a damsel to hearken, by name Rhoda,
13Petro alibisha mlango wa nje na mtumishi mmoja msichana aitwaye Roda, akaenda mlangoni kuitikia.
14and having known the voice of Peter, from the joy she did not open the porch, but having run in, told of the standing of Peter before the porch,
14Huyo msichana aliitambua sauti ya Petro akafurahi mno, hata badala ya kuufungua ule mlango, akakimbilia ndani na kuwaambia kwamba Petro alikuwa amesimama nje mlangoni.
15and they said unto her, `Thou art mad;` and she was confidently affirming [it] to be so, and they said, `It is his messenger;`
15Wakamwambia yule msichana, "Una wazimu!" Lakini yeye akasisitiza kwamba ilikuwa kweli. Nao wakamwambia, "Huyo ni malaika wake."
16and Peter was continuing knocking, and having opened, they saw him, and were astonished,
16Wakati huo Petro alikuwa anaendelea kupiga hodi. Mwishowe walifungua mlango, wakamwona, wakashangaa.
17and having beckoned to them with the hand to be silent, he declared to them how the Lord brought him out of the prison, and he said, `Declare to James and to the brethren these things;` and having gone forth, he went on to another place.
17Petro aliwaashiria kwa mkono wakae kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Kisha akawaambia watoe taarifa ya jambo hilo kwa Yakobo na wale ndugu wengine, halafu akatoka akaenda mahali pengine.
18And day having come, there was not a little stir among the soldiers what then was become of Peter,
18Kulipokucha, ulitokea wasiwasi mkubwa kati ya wale askari kuhusu yaliyokuwa yamempata Petro.
19and Herod having sought for him, and not having found, having examined the guards, did command [them] to be led away to punishment, and having gone down from Judea to Cesarea, he was abiding [there].
19Herode aliamuru ufanywe msako lakini hawakuweza kumpata. Hivyo aliamuru wale askari wahojiwe, akatoa amri wauawe. Halafu akatoka huko Yudea akaenda Kaisarea ambako alikaa.
20And Herod was highly displeased with the Tyrians and Sidonians, and with one accord they came unto him, and having made a friend of Blastus, who [is] over the bed-chambers of the king, they were asking peace, because of their country being nourished from the king`s;
20Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
21and on a set day, Herod having arrayed himself in kingly apparel, and having sat down upon the tribunal, was making an oration unto them,
21Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme aliwahutubia watu.
22and the populace were shouting, `The voice of a god, and not of a man;`
22Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, "Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu."
23and presently there smote him a messenger of the Lord, because he did not give the glory to God, and having been eaten of worms, he expired.
23Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa.
24And the word of God did grow and did multiply,
24Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
25and Barnabas and Saul did turn back out of Jerusalem, having fulfilled the ministration, having taken also with [them] John, who was surnamed Mark.
25Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza shughuli zao, walitoka tena Yerusalemu wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.