Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

John

20

1And on the first of the sabbaths, Mary the Magdalene doth come early (there being yet darkness) to the tomb, and she seeth the stone having been taken away out of the tomb,
1Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.
2she runneth, therefore, and cometh unto Simon Peter, and unto the other disciple whom Jesus was loving, and saith to them, `They took away the Lord out of the tomb, and we have not known where they laid him.`
2Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, "Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka."
3Peter, therefore, went forth, and the other disciple, and they were coming to the tomb,
3Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.
4and the two were running together, and the other disciple did run forward more quickly than Peter, and came first to the tomb,
4Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5and having stooped down, seeth the linen clothes lying, yet, indeed, he entered not.
5Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.
6Simon Peter, therefore, cometh, following him, and he entered into the tomb, and beholdeth the linen clothes lying,
6Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,
7and the napkin that was upon his head, not lying with the linen clothes, but apart, having been folded up, in one place;
7na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.
8then, therefore, entered also the other disciple who came first unto the tomb, and he saw, and did believe;
8Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
9for not yet did they know the Writing, that it behoveth him out of the dead to rise again.
9(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
10The disciples therefore went away again unto their own friends,
10Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
11and Mary was standing near the tomb, weeping without; as she was weeping, then, she stooped down to the tomb, and beholdeth two messengers in white, sitting,
11Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,
12one at the head, and one at the feet, where the body of Jesus had been laid.
12akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.
13And they say to her, `Woman, why dost thou weep?` she saith to them, `Because they took away my Lord, and I have not known where they laid him;`
13Hao malaika wakamwuliza, "Mama, kwa nini unalia?" Naye akawaambia, "Wamemwondoa Bwana wangu, na wala sijui walikomweka!"
14and these things having said, she turned backward, and seeth Jesus standing, and she had not known that it is Jesus.
14Baada ya kusema hayo, aligeuka nyuma, akamwona Yesu amesimama hapo, lakini asitambue ya kuwa ni Yesu.
15Jesus saith to her, `Woman, why dost thou weep? whom dost thou seek;` she, supposing that he is the gardener, saith to him, `Sir, if thou didst carry him away, tell me where thou didst lay him, and I will take him away;`
15Yesu akamwuliza, "Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?" Maria, akidhani kwamba huyo ni mtunza bustani, akamwambia, "Mheshimiwa, kama ni wewe umemwondoa, niambie ulikomweka, nami nitamchukua."
16Jesus saith to her, `Mary!` having turned, she saith to him, `Rabbouni;` that is to say, `Teacher.`
16Yesu akamwambia, "Maria!" Naye Maria akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, "Raboni" (yaani "Mwalimu").
17Jesus saith to her, `Be not touching me, for I have not yet ascended unto my Father; and be going on to my brethren, and say to them, I ascend unto my Father, and your Father, and to my God, and to your God.`
17Yesu akamwambia, "Usinishike; sijakwenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu."
18Mary the Magdalene cometh, telling to the disciples that she hath seen the Lord, and [that] these things he said to her.
18Hivyo Maria Magdalene akaenda akawapa habari wale wanafunzi kuwa amemwona Bwana, na kwamba alikuwa amemwambia hivyo.
19It being, therefore, evening, on that day, the first of the sabbaths, and the doors having been shut where the disciples were assembled, through fear of the Jews, Jesus came and stood in the midst, and saith to them, `Peace to you;`
19Ilikuwa jioni ya siku hiyo ya Jumapili. Wanafunzi walikuwa wamekutana pamoja ndani ya nyumba, na milango ilikuwa imefungwa kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Basi, Yesu akaja, akasimama kati yao, akawaambia, "Amani kwenu!"
20and this having said, he shewed them his hands and side; the disciples, therefore, rejoiced, having seen the Lord.
20Alipokwisha sema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi, hao wanafunzi wakafurahi mno kumwona Bwana.
21Jesus, therefore, said to them again, `Peace to you; according as the Father hath sent me, I also send you;`
21Yesu akawaambia tena, "Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi."
22and this having said, he breathed on [them], and saith to them, `Receive the Holy Spirit;
22Alipokwisha sema hayo, akawapulizia na kuwaambia, "Pokeeni Roho Mtakatifu.
23if of any ye may loose the sins, they are loosed to them; if of any ye may retain, they have been retained.`
23Mkiwasamehe watu dhambi zao, wamesamehewa; msipowaondolea, hawasamehewi."
24And Thomas, one of the twelve, who is called Didymus, was not with them when Jesus came;
24Thoma mmoja wa wale kumi na wawili (aitwaye Pacha), hakuwa pamoja nao wakati Yesu alipokuja.
25the other disciples, therefore, said to him, `We have seen the Lord;` and he said to them, `If I may not see in his hands the mark of the nails, and may put my finger to the mark of the nails, and may put my hand to his side, I will not believe.`
25Basi, wale wanafunzi wengine wakamwambia, "Tumemwona Bwana." Thoma akawaambia, "Nisipoona mikononi mwake alama za misumari, na kutia kidole changu katika kovu hizo, na kutia mkono wangu ubavuni mwake, sitasadiki."
26And after eight days, again were his disciples within, and Thomas with them; Jesus cometh, the doors having been shut, and he stood in the midst, and said, `Peace to you!`
26Basi, baada ya siku nane hao wanafunzi walikuwa tena pamoja mle ndani, na Thoma alikuwa pamoja nao. Milango ilikuwa imefungwa, lakini Yesu akaja, akasimama kati yao, akasema, "Amani kwenu!"
27then he saith to Thomas, `Bring thy finger hither, and see my hands, and bring thy hand, and put [it] to my side, and become not unbelieving, but believing.`
27Kisha akamwambia Thoma, "Lete kidole chako hapa uitazame mikono yangu; lete mkono wako ukautie ubavuni mwangu. Usiwe na mashaka, ila amini!"
28And Thomas answered and said to him, `My Lord and my God;`
28Thoma akamjibu, "Bwana wangu na Mungu wangu!"
29Jesus saith to him, `Because thou hast seen me, Thomas, thou hast believed; happy those not having seen, and having believed.`
29Yesu akamwambia, "Je, unaamini kwa kuwa umeniona? Heri yao wale ambao hawajaona, lakini wameamini."
30Many indeed, therefore, other signs also did Jesus before his disciples, that are not written in this book;
30Yesu alifanya mbele ya wanafunzi wake ishara nyingine nyingi ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki.
31and these have been written that ye may believe that Jesus is the Christ, the Son of God, and that believing ye may have life in his name.`
31Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mpate kuwa na uzima kwa nguvu ya jina lake.