Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

John

21

1After these things did Jesus manifest himself again to the disciples on the sea of Tiberias, and he did manifest himself thus:
1Baada ya hayo Yesu aliwatokea tena wanafunzi wake kando ya ziwa Tiberia. Aliwatokea hivi:
2There were together Simon Peter, and Thomas who is called Didymus, and Nathanael from Cana of Galilee, and the [sons] of Zebedee, and two others of his disciples.
2Simoni Petro, Thoma (aitwaye Pacha), na Nathanieli mwenyeji wa Kana Galilaya, wana wawili wa Zebedayo na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa wote pamoja.
3Simon Peter saith to them, `I go away to fish;` they say to him, `We go — we also — with thee;` they went forth and entered into the boat immediately, and on that night they caught nothing.
3Simoni Petro aliwaambia, "Nakwenda kuvua samaki." Nao wakamwambia, "Nasi tutafuatana nawe." Basi, wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakupata chochote.
4And morning being now come, Jesus stood at the shore, yet indeed the disciples did not know that it is Jesus;
4Kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya ziwa, lakini wanafunzi hawakujua kwamba alikuwa yeye.
5Jesus, therefore, saith to them, `Lads, have ye any meat?`
5Basi, Yesu akawauliza, "Vijana, hamjapata samaki wowote sio?" Wao wakamjibu, "La! Hatujapata kitu."
6they answered him, `No;` and he said to them, `Cast the net at the right side of the boat, and ye shall find;` they cast, therefore, and no longer were they able to draw it, from the multitude of the fishes.
6Yesu akawaambia, "Tupeni wavu upande wa kulia wa mashua nanyi mtapata samaki." Basi, wakatupa wavu lakini sasa hawakuweza kuuvuta tena kwa wingi wa samaki.
7That disciple, therefore, whom Jesus was loving saith to Peter, `The Lord it is!` Simon Peter, therefore, having heard that it is the Lord, did gird on the outer coat, (for he was naked,) and did cast himself into the sea;
7Hapo yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, "Ni Bwana!" Simoni Petro aliposikia ya kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa), akarukia majini.
8and the other disciples came by the little boat, for they were not far from the land, but as it were about two hundred cubits off, dragging the net of the fishes;
8Lakini wale wanafunzi wengine walikuja pwani kwa mashua huku wanauvuta wavu uliojaa samaki; hawakuwa mbali na nchi kavu, ila walikuwa yapata mita mia moja kutoka ukingoni.
9when, therefore, they came to the land, they behold a fire of coals lying, and a fish lying on it, and bread.
9Walipofika nchi kavu waliona moto wa makaa umewashwa na juu yake pamewekwa samaki na mkate.
10Jesus saith to them, `Bring ye from the fishes that ye caught now;`
10Yesu akawaambia, "Leteni hapa baadhi ya samaki mliovua."
11Simon Peter went up, and drew the net up on the land, full of great fishes, an hundred fifty and three, and though they were so many, the net was not rent.
11Basi, Simoni Petro akapanda mashuani, akavuta hadi nchi kavu ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa mia moja na hamsini na watatu. Na ingawa walikuwa wengi hivyo wavu haukukatika.
12Jesus saith to them, `Come ye, dine;` and none of the disciples was venturing to inquire of him, `Who art thou?` knowing that it is the Lord;
12Yesu akawaambia, "Njoni mkafungue kinywa." Hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumwuliza: "Wewe ni nani?" Maana walijua alikuwa Bwana.
13Jesus, therefore, doth come and take the bread and give to them, and the fish in like manner;
13Yesu akaja, akatwaa mkate akawapa; akafanya vivyo hivyo na wale samaki.
14this [is] now a third time Jesus was manifested to his disciples, having been raised from the dead.
14Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada ya kufufuka kutoka wafu.
15When, therefore, they dined, Jesus saith to Simon Peter, `Simon, [son] of Jonas, dost thou love me more than these?` he saith to him, `Yes, Lord; thou hast known that I dearly love thee;` he saith to him, `Feed my lambs.`
15Walipokwisha kula, Yesu alimwuliza Simoni Petro, "Simoni, mwana wa Yohane! Je, wanipenda mimi zaidi kuliko hawa?" Naye akajibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza wana kondoo wangu."
16He saith to him again, a second time, `Simon, [son] of Jonas, dost thou love me?` he saith to him, `Yes, Lord; thou hast known that I dearly love thee;` he saith to him, `Tend my sheep.`
16Kisha akamwambia mara ya pili, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Petro akamjibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu."
17He saith to him the third time, `Simon, [son] of Jonas, dost thou dearly love me?` Peter was grieved that he said to him the third time, `Dost thou dearly love me?` and he said to him, `Lord, thou hast known all things; thou dost know that I dearly love thee.` Jesus saith to him, `Feed my sheep;
17Akamwuliza mara ya tatu, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Hapo Petro akahuzunika kwa sababu alimwuliza mara ya tatu: "Wanipenda?" akamwambia, "Bwana, wewe wajua yote; wewe wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu!
18verily, verily, I say to thee, When thou wast younger, thou wast girding thyself and wast walking whither thou didst will, but when thou mayest be old, thou shalt stretch forth thy hands, and another will gird thee, and shall carry [thee] whither thou dost not will;`
18Kweli nakwambia, ulipokuwa kijana ulizoea kujifunga mshipi na kwenda kokote ulikotaka. Lakini utakapokuwa mzee utanyosha mikono yako, na mtu mwingine atakufunga na kukupeleka usikopenda kwenda."
19and this he said, signifying by what death he shall glorify God; and having said this, he saith to him, `Be following me.`
19(Kwa kusema hivyo, alionyesha jinsi Petro atakavyokufa na kumtukuza Mungu.) Kisha akamwambia, "Nifuate."
20And Peter having turned about doth see the disciple whom Jesus was loving following, (who also reclined in the supper on his breast, and said, `Sir, who is he who is delivering thee up?`)
20Hapo Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda, anafuata (Huyu mwanafunzi ndiye yule ambaye wakati wa chakula cha jioni, alikaa karibu sana na Yesu na kumwuliza: "Bwana ni nani atakayekusaliti?")
21Peter having seen this one, saith to Jesus, `Lord, and what of this one?`
21Basi, Petro alipomwona huyo akamwuliza Yesu, "Bwana, na huyu je?"
22Jesus saith to him, `If him I will to remain till I come, what — to thee? be thou following me.` This word, therefore, went forth to the brethren that that disciple doth not die,
22Yesu akamjibu, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini? Wewe nifuate mimi."
23yet Jesus did not say to him, that he doth not die, but, `If him I will to remain till I come, what — to thee?`
23Basi, habari hiyo ikaenea miongoni mwa wale ndugu kwamba mwanafunzi huyo hafi. Lakini Yesu hakumwambia kwamba mwanafunzi huyo hafi, ila, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini?"
24this is the disciple who is testifying concerning these things, and he wrote these things, and we have known that his testimony is true.
24Huyo ndiye yule aliyeshuhudia mambo haya na kuyaandika. Nasi twajua kwamba aliyoyasema ni kweli.
25And there are also many other things — as many as Jesus did — which, if they may be written one by one, not even the world itself I think to have place for the books written. Amen.
25Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.